ABEDNEGO
Senior Member
- Aug 20, 2009
- 109
- 30
Ni saba saba day, nimeenda kwenye vituo tofauti tofauti vya mafuta(Petrol stations) nikitaka diesel kwa ajili ya ka-generator kangu nikijihami na mgao wa umeme,Sasa niliyoyakuta huko ndo yananifanya niwaulize wana-JF wenzangu.Nilikuwa na vidumu viwili vya lita tano tano,Sasa kila kituo nilichoenda naambiwa hawajazi diesel kwenye vidumu(Eti sheria mpya ya EWURA) Sikuamini maneno ya wahudumu kuanzia Mbezi Louis hadi Ubungo Plaza kituo cha Engen(Vituo 9) ndo walikubali kunipa kwa shingo upande!!! Kwa kuwa nilihitaji lita kumi tu dumu la kwanza lilijaa la pili kama lita tatu hivi.Maana yake nilipata lita nane kwa gharama za lita kumi.Hapo nikaelewa maana ya kukataa vidumu vyenye ujazo unaoeleweka.Kwa hali hiyo vituo vya mafuta Jijini Dar vinatuibia sana!!EWURA wanalijua hili au wako zaidi kwenye uchakachuaji tu?