kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
Kuna ule wimbo wa Msondo Ngoma ''ukiona mtu mzima analia, ujue kuna jambo''
nimezidi kuuelewa huo wimbo jana jioni wakati narejea nyumbani.
Nilikuwa natokea IFM kupitia Shaaban Robert street, muda kama saa mbili hivi usiku, pale kwenye kona ya International House kuelekea Umoja House nilipishana na gari nyingine iliyokuwa inakuja kasi sana bila kujali yale matuta ya barabara. Nikahisi jambo ila sina uhakika.
Baada ya kuendelea mbele nikakutana na jamaa anafukuza mbio huku anapiga kelele na kulia. Nilihisi huruma nikasimama ili nimuulize. Alinijibu kuna gari ilikuwa imepaki Ohio street wakati anavuka barabara kuja Garden Avenue hiyo gari ikakunja kuelekea aliko na ilimsogelea sana akadhani ni watu anaowafahamu labda watampa lift, haikuwa hivyo mmoja wa seat ya nyuma akachomoza na kukwapua bag lake likiwa na laptop tena mpya, kilichomfanya alie ni kwa vile laptop hiyo si yake na ina mafaili muhimu sana ya watu, masikini!
Kwa kuwa ile gari hatukuona muelekeo wake hapakuwa na jinsi ila nilimpeleka kituo cha Police pale Gym Khana, baada ya maelezo Polisi altujulisha kuwa sio tukio la kwanza la namna hiyo mitaa ile, hivyo nawajulisha kuwa maeneo yale Samora, Ohio, Garden mpaka Posta si mazuri sana hasa usiku unapokuwa na bag linaloonesha umebeba laptop, tahadhari kwa Wanafunzi IFM, Wafanyakazi wa ofisi za maeneo hayo wawe japo hata wawili inaweza kusaidia wasiporwe.
Wajulisheni wengine tafadhali.
nimezidi kuuelewa huo wimbo jana jioni wakati narejea nyumbani.
Nilikuwa natokea IFM kupitia Shaaban Robert street, muda kama saa mbili hivi usiku, pale kwenye kona ya International House kuelekea Umoja House nilipishana na gari nyingine iliyokuwa inakuja kasi sana bila kujali yale matuta ya barabara. Nikahisi jambo ila sina uhakika.
Baada ya kuendelea mbele nikakutana na jamaa anafukuza mbio huku anapiga kelele na kulia. Nilihisi huruma nikasimama ili nimuulize. Alinijibu kuna gari ilikuwa imepaki Ohio street wakati anavuka barabara kuja Garden Avenue hiyo gari ikakunja kuelekea aliko na ilimsogelea sana akadhani ni watu anaowafahamu labda watampa lift, haikuwa hivyo mmoja wa seat ya nyuma akachomoza na kukwapua bag lake likiwa na laptop tena mpya, kilichomfanya alie ni kwa vile laptop hiyo si yake na ina mafaili muhimu sana ya watu, masikini!
Kwa kuwa ile gari hatukuona muelekeo wake hapakuwa na jinsi ila nilimpeleka kituo cha Police pale Gym Khana, baada ya maelezo Polisi altujulisha kuwa sio tukio la kwanza la namna hiyo mitaa ile, hivyo nawajulisha kuwa maeneo yale Samora, Ohio, Garden mpaka Posta si mazuri sana hasa usiku unapokuwa na bag linaloonesha umebeba laptop, tahadhari kwa Wanafunzi IFM, Wafanyakazi wa ofisi za maeneo hayo wawe japo hata wawili inaweza kusaidia wasiporwe.
Wajulisheni wengine tafadhali.