wizara ya maliasili na utalii

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,887
3,412
tunashangazwa sana na kitendo cha wizara hiyo kushindwa kuhamasisha watanzania umuhimu wa kupigia kura mlima kilimanjaro,
kwa kweli inasikitisha kwa sababu watanzania wengi wameshindwa kujua nini kinaendelea na nini kinatakiwa kufanywa,
kura zilizopigwa mpaka sasa hivi ailimia 75% ni wazungu na watu waishio nje ya tanzania wasio watanzania,
ukilinganisha na africa kusini kupigia kura mlima wao asilia m85% ni waafrica kusini bila kushirikisha sana wageni,
nataka kuwauliza swali wizara,kazi ndogo namna hiyo kuhamasisha watanzania mnashindwa?
waziri tukuweke kwenye kundi gani?kazi imekushinda?hata kuingilia kati swala muhimu kama hili unashindwa mkuu?
najua ulikula kitabu pale mzumbe na una qualification lakini kumbe kitabu na kazi ni vitu viwili tofauti?
mbona kila siku mnafatilia pet cash?mnahindwa kukodi watoto wa pale manzese wenye maspika kwenda kutangaza kila kona?
watanzania ailimia 50% wana uwezo wa kutumia internet na simu,je mngehamasisha kiasi cha kutosha si tungepata hiyo nafasi?
mashavu yaliyojaa manyama choma na ugali ndio mnahamsisha??kila mchana kupata bia inakusaidia au inazidi kukumaliza?
hivi kuna haja ya kuangalia IQ ya mtu kabla hajapewa kazi???
 
Back
Top Bottom