Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Kaka Mtenga

JF-Expert Member
Feb 25, 2013
347
87
Wanajf
Wizara zingine ni ulaji tu.

Eti WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA NA WATOTO.

1:MAENDELEO YA JAMII-Hayo maendeleo ni jamii gani iliyokusudiwa? Mbona jamii kubwa ya Watz hawana maendeleo kabisa wakati Sofia Simba kakabidhiwa mamilioni ya kodi ya walalahoi?



2:JINSIA- Ni jinsia ipi ambayo Sofia anaihudumia? Au ni harusi ya shoga yake Anna Kilango niliyoina kwenye magazeti? Leo hii Anna+Sofia jibu ni MSIBA.Hayo yanasababishwa na kiburi cha Fungu la kodi zetu eti "Lowassa ni mwanaume wa shoka"
Kwanini Anna hukumuuluza kama anamzidi Malecela? Hizo ni hela za jinsia zinapondwa.

3:WATOTO-Watoto wepi wanaohudumiwa na hii kodi yetu? Naomba mambo mengine wawe wanakuwa wazi kwa wananchi.

Sijawahi kusikia au kuona hata kwenye vyombo vya habari jinsi hii Wizara inavyohudumia jamii ya watz. Wakishapewa fedha basi huwaoni popote mpaka bunge lingine la budget kuja kusomba tena kodi yetu.

Leo ni Wizara ya Sofia lakini zipo wizara nyenza zenye sura kama hiyo na ndio maana tunahitaji Baraza dogo la Mawaziri lenye tija.

Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom