Wivu wetu uko kwenye kitu gani hasa?

Wivu ni udhaifu halafu ni hisia hasi,haujawahi kuleta matokeo chanya wakati au mahali popote!
 
Maisha ni kupigania na kupata mafanikio na mafanikio mengine zaidi. Wote tumeumbwa na uhitaji kwa kujitahidi tufanikiwe na kufanikiwa zaidi. Amazing enough tumeumbwa na feelinga za kutaka kuwa sawa kimaisha kwa watu ambao tunaona tuko kwenye level moja. Then again roho ya kustand out from the rest! Unapoona wewe hufanikiwi unahisi hapa pagumu, kisha anakuja mwenzio anapapita unaingiwa na inferiority complex na kuanza kuogopa macho ya watu. It would have been fine if huyo mwenzio asingepavuka, sasa wewe unaona ili iwe sawa kwako ni bora ufanye namna asipavuke.
Ndio maana kama una rafiki na yuko chini kimaisha unamsaidia kupigana ili muwe sawa...akianza kukupita mnagombana because deep down u always want them to be under you.
PetCash hauja muelewa mtoa hoja. Mwenzio anazungumzia wivu katika mapenzi wakati wewe unazungumzia wivu katika masuala ya maendeleo. Msome vizuri.
 
wivu katika mapenzi ni muhimu jaman...hata kama ni kwa asilimia 1,but kama unampenda kwa dhat mwandan wako..aaaah,kawivu lazima katakuwepo.
 
wivu katika mapenzi ni muhimu jaman...hata kama ni kwa asilimia 1,but kama unampenda kwa dhat mwandan wako..aaaah,kawivu lazima katakuwepo.

Hebu niambie wivu maana yake nini na nini umuhimu wake!
 
Ukipenda daima utajenga dhana fulani ya umilikishi yaani kujenga mawazo ya kana kwamba yule mtu ni wa kwako tu..na haupo tayari kumwona akiwa karibu na mwingine! Wivu upo katika many aspects, si kwa wapenzi tu hata marafiki..
 
Salaam zenu wanajamii. Miongoni mwa vitu vinavyotufanya tupendane ni mahaba, ukuruba (feeling to each other) maumbile (beauty), maingiliano ya kimwili (sex), matarajio (expectations) na mengine mengi.

Sasa wenzangu tunapoona wivu juu ya wenzetu wa karibu yaani mke/mume au boyriend/girlfriend huwa tunaona wivu wa kitu gani maalum kati ya vitu vinavyofanya tupendane?

Hapo kwenye bold, tunachoonea wivu ni ile haki yangu ya penzi juu ya yule nimpendae hususan kama kuna dalili ya kuitoa haki hiyo kwa mtu asiye mhusika!!!
 
PetCash hauja muelewa mtoa hoja. Mwenzio anazungumzia wivu katika mapenzi wakati wewe unazungumzia wivu katika masuala ya maendeleo. Msome vizuri.
Litty asante, Ila kuwa na a great love life ni maendeleo. Sema tu mimi nimeamua kuwa general.
 
Last edited by a moderator:
Wivu muhimu kwa umpendae hasa pale unapohisi kuna mtu anakuibia usingizi unakosa....
 
Hapo kwenye bold, tunachoonea wivu ni ile haki yangu ya penzi juu ya yule nimpendae hususan kama kuna dalili ya kuitoa haki hiyo kwa mtu asiye mhusika!!!

Unajuwa HP, kinachonishangaza mimi kuwa kuna wengi wenye wivu kwa watu wao iwe mke au mume lakini huwa wanakwenda kwa watu wengine ambao inawezekana wao wenyewe wanakiri kuwa watu wao wana vitu vizuri zaidi kuliko wanavyovifatia nje. Kibaya ukiwauliza wanakwambia wanawapenda watu wao na inawezekana wanawapenda kweli.
 
Wivu ni udhaifu halafu ni hisia hasi,haujawahi kuleta matokeo chanya wakati au mahali popote!

Mimi siamini kuwa wivu ni udhaifu bali ni njia moja ya kujali chako, of course kila kitu kikienda extreme ni kibaya!
 
wivu katika mapenzi ni muhimu jaman...hata kama ni kwa asilimia 1,but kama unampenda kwa dhat mwandan wako..aaaah,kawivu lazima katakuwepo.

Katika mapenzi huwa tunashare mahusiano yetu na wanaotuzunguka, sasa huku kushare tunashare mpaka wapi na kuanzia wapi wivu (Hisia ya kukimiliki peke yako) unaanzia?
 
Ukipenda daima utajenga dhana fulani ya umilikishi yaani kujenga mawazo ya kana kwamba yule mtu ni wa kwako tu..na haupo tayari kumwona akiwa karibu na mwingine! Wivu upo katika many aspects, si kwa wapenzi tu hata marafiki..

Kwa upande wako Da Amina umiliki wako peke yako kwa shemeji unaanzia wapi? Nasema hivyo kwani shemeji ana watu wanamzunguka ambao atawapa sehemu mahusiano yake.
 
Hapo kwenye bold, tunachoonea wivu ni ile haki yangu ya penzi juu ya yule nimpendae hususan kama kuna dalili ya kuitoa haki hiyo kwa mtu asiye mhusika!!!

Unajuwa HP, kinachonishangaza mimi kuwa kuna wengi wenye wivu kwa watu wao iwe mke au mume lakini huwa wanakwenda kwa watu wengine ambao inawezekana wao wenyewe wanakiri kuwa watu wao wana vitu vizuri zaidi kuliko wanavyovifatia nje. Kibaya ukiwauliza wanakwambia wanawapenda watu wao na inawezekana wanawapenda kweli.

Kiongozi ukiona hivyo, ujue ni suala la tamaa za mwili linakuwa limechukua nafasi yake. Unakuta mtu ana mke anayempenda, akapita mtu mwingine mwenye figure ya kuvutia akashikwa na tamaa akamtokea na kutembea naye wakati moyoni mwake hampendi, anafanya hivyo kukidhi mahitaji ya mwili kwa wakati huo!
 
Back
Top Bottom