Wivu Umemuua!!

ANAITWA Flora nani, sema basi tujue ni kwa jinsi gani tutamuwajibisha mumewe
Duh! nikuelekeze ulipo msiba uje? So far ndugu zake kwa miaka zaidi ya 20 walishasamehe ila sina hakika kama watasahau.
 
U a wrong Lizzy. Jamaa yuko Kitaa na anafanya biashara ya Hardware mitaa ya Kariakoo. Hajawahi hata kukamatwa kwa kosa hilo. Kitu pekee ninachokijua aliubeba mzigo wa matibabu ya mkewe hadi mwisho. Kuanzia Malago Hospitali Kuu ya Uganda hadi Kwa T.B. Joshua gharama zote hizo pamoja na zile za Blood Detoxification (280,000 Kwa wiki) jamaa alizibeba yeye. Hapo katikati alizaa mtoto na mwanamke mwingine!!

Mikono ya sheria haikuwahi kumfikia!!

Basi pengine mke wake hakuona haja ya kumshtaki au walikubaliana anyamaze apate msaada.
 
Basi pengine mke wake hakuona haja ya kumshtaki au walikubaliana anyamaze apate msaada.
mwanzoni alidhani atapona haraka na kurudia maisha yake ya zamani. Lakini baada ya juhudi zote za kumtibia wakiwa wanaishi Bukoba kushindikana na kupelekwa Uganda kwa matibabu. Hatimaye naona akakubali "kumsamehe" mumewe na kukubali kuishi kama alivyo. Shida ilikuja pale ilipogundulika kwamba damu yake imechafuliwa sana na madawa.
 
Hadithi yako inatufundisha nini?
this is not fictional story my bros, this is a real life. Kama unabisha fika hapa Mitaa ya kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Kijitonyama ulizia utaletwa msibani!!
 
Ndugu zangu adui wa mtu ni roho zitokazo kuzimu zenye kuleta mtafaruku ktk ya jamii, huyo jamaa najua alijutia wivu juu ya yule mama wakati anajua wazi kuwa yeye nimkosaji mkuu, Christo alisema asiye na kosa awe wa kwanza kumpiga jiwe, yeye akajifanya hafanyi kosa akampiga mama wa watu nakumpa kilema, na sasa kapoteza uhai kwa uchungu mkubwa, ole wake na wote wenye tabia kama hiyo, inatulazimu waname tuwe wenyekupima nakujiangalia je cc hatufanyi hayo?
Nawapa pole watoto kwa kumkosa mama japo ameondoka tayari wamekuwa wakubwa.
 
Leo kwenye makaburi ya Ukoo Dada yetu Mpendwa Flora anazikwa na kupumzika baada ya miaka zaidi ya 20 tangu alemazwe na mumewe!!
 
Ni kisa cha kweli kabisa kilichomtokea mtu ninayemfahamu kwa miaka mingi sana. Msiba uko Kijitonyama nyumbani kwake. Nimetumia neno "dada" kwa sababu nilimheshimu hivyo siku zote na yeye alinichukulia hivyo hivyo kuwa ni kaka yake. Ameacha watoto wawili wa kiume mmoja yuko Chuo Kikuu na mwingine anatarajia kusomea Comm. Dev pale kijitonyama.

Huyo mumewe alichukuliwa hatua gani?
 
Masikini dada wa watu.... RIP Florah..... na hii iwaendee wale wote wanaojing'ang'aniza kwa ndoa zilizo jaa violence.
nashukuru nimejichomoa kwa hiyo ndoa, siku moja yangenikuta haya.
 
RIP dear Flora. Na huyo Bwana Mungu ampatilize kwa mabayaaliyotenda, malipo ni hapa hapa duniani
 
Huyo mumewe alichukuliwa hatua gani?
Hakuna alichofanywa kwani wanandugu waliona kwamba jamaa "kajutia" alichokifanya!! Flora ndiye alionyesha moyo wa kishujaa kabisa kwani pamoja na kuwa na hali dhaifu kwa miaka yote alikuwa anajitahidi kusimamia maisha yake na ya familia yake!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom