Bikirembwe
JF-Expert Member
- Feb 13, 2008
- 250
- 7
Wakati mwingine jukwaa hili linakuwa kama klabu cha pombe! analysis zingine zinazotolewa hapa ni tepe tepe sana,kwa mfano si lazima iwe ccm au chama kingine chochote rais ajaye lazima akubalike zanzibar! vigezo vya hivi haviwezi kutupa rais bora! anayechaguliwa na rais wa jamhuri ya tanzania!
Pengine kubwa la kutizama na linalotuunganisha watanzania wote ni kama candidate anaiweza kazi! kwa maana ya uzoefu,uaminifu,hekima,ujuzi,uthabiti nk, bahati mbaya sana watanzania wengi wanaochangia hapajf wanaiona kazi hii kama rahisi tu!!! ndio maana wanasikika wengine wakisema aje kijana next time!
Lakini ukweli kabisa kwa sasa hakuna kijana iwe kwa wale walio ktk uongozi sasa au walio nje anaweza kuwa rais mzr wa tz! pengine wengi wanavutwa kwa kutaka kuiga tu, kutaka nchi zingine zenye marais vijana.kwa tz ni vigumu!kwa sababu structuire ya malezi katika familia zetu ni mbovu kabisa siku hizi!!! hazimjengi mtoto au kijana kuwa kiongozi mzuri!! zinamjenga kuwa mbinafsi,mpenda anasa,mchoyo,mbaguzi,mnafiki nk. kwa maana hiyo bado tunahitaji sana kuwa na vongozi wa umri kama wa salim,shein,mwandosya,sitta, nk kwenye nafasi ya urais na makamu ili kutunza tunu za taifa letu,AMANI,UTULIVU,KUHESHIMIANA,UPENDO nk.
Mifano ipo mingi lakin ni vzr tunapojadili watz wanaoweza kufanya hii kazi tuongozwe na sifa ya UWEZO na siyo kutanguliza uwepo wa mizengwe au cjui mtandao hiyo ni fanatism tu haina nguvu sasa hivi,lkn mwisho kabisa yupo mwenyezi Mungu nayye ana hesabu zake! our choise is not ABSOLUTE!! it can be changed!!
Mkuu umechemsha ukweli ni huo uloelezwa na haupingiki makundi yapo, CCM Znz wanampiga vita SAS nk, sasa wewe unaleta picha ya nchi ilo na raia wanaijua demokrasia na ambayo haiendeshwi kwa mizengwe.