Wito kwa engineers tulio graduate UDSM mwaka 2002.

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
Nimekaa nikawaza kwamba kwa wale wahandisi tuliomaliza UDSM na wengine watakao penda kujiunga/kushiriki tujipange tuanzishe walau ka kampuni kadogo ka ufundi ili tuweze kukopa pesa benki na kuzalisha japo simple wind mills ambazo tunaweza kuzitumia ku-generate umeme na hata kusukumia maji vijijini.

Sijawa na proposal as such lakini ni wazo tu na siyo wind mills peke yake we can produce so many engineering products lakini lazima tuwe na kitu cha kuanza nacho. Ingawa kwa sasa sipo bongo lakini walioko jamani tuanze sasa.

We have to show that we gained something from the then FOE.
 
hivi kweli JF hakuna wahandisi au hoja yangu haina mashiko??
 
hivi kweli JF hakuna wahandisi au hoja yangu haina mashiko??

Nafikiri ni brilliant idea ila approach yako ndo inawalakini, mzee kama unawakumbuka hao Engineer wenzako alumni wa 2002 wasiliana nao mjipange, hapa JF wengine tumesomea mahoka msaada unaweza kuwa mdogo na issue ya annonymity ina complicate zaidi.
 
Nimekaa nikawaza kwamba kwa wale wahandisi tuliomaliza UDSM mwaka 2002 na wengine watakao penda kujiunga/kushiriki tujipange tuanzishe walau ka kampuni kadogo ka ufundi ili tuweze kukopa pesa benki na kuzalisha japo simple wind mills ambazo tunaweza kuzitumia ku-generate umeme na hata kusukumia maji vijijini.

Sijawa na proposal as such lakini ni wazo tu na siyo wind mills peke yake we can produce so many engineering products lakini lazima tuwe na kitu cha kuanza nacho. Ingawa kwa sasa sipo bongo lakini walioko jamani tuanze sasa.

We have to show that we gained something from the then FOE.

Very good idea mkuu, mi nadhani isiwekwe limit ya graduates wa 2002 maana suala kama hili ni kwa Mhandisi yeyote anayejiskia kushiriki kuliendeleza taifa.

Suala la kugenerate umeme ni muhimu sana na hata maji, nisingependa kushea idea yangu in details hapa ila we can discuss this further kwa PM. Check PM yako in the next 30min.
 
Vijana wa FOE/CoET tuko wengi. Nimeanzisha mail group ya google inaitwa engineertz@googlegroups.com ili engineers tukutane na kujadili mambo mbalimbali.

Idea yako ni nzuri.Na kwa nchi kama yetu na kilimo kwanza we need to add value kwenye agricultural products.
 
idea ni nzuri sana ila unajuwa tena kila mtu atajiunga kwa mtazamo wa tumbo lake. Ni vizuri sio pekee Engineers ni lazima mshirikishe na wanasheria, wahasibu na wataalamu wa Biashara ili waweze kuwaandikia business plan ambayo itawasaidia kupa mkopo na hata kuendesha biashara.

Ila mimi ningekushauri sana mjiunge Engineers katika makundi madogo madogo kama watano mpaka kumi max na sio wote. Kwani mkiwa wengi utawala wake utakuwa mzito sana.

Huo ni ushauri wangu.
 
Wazo lako ni zuri na linataka seriousness in execution. Engineers tumekuwa watazamaji mno badala ya drivers wa mambo ambayo ni muhimu kweli kwa ustawi wa Taifa letu. Lazima kuwepo na mwelekeo ili mambo yasiishie kuwa story tu kama tulivyozoea.
Kuna mambo mengi ambayo yanahitajika kwenye jamii yetu na hatufanyi lolote kwa sasa. Kuanzia mashirika yanayoendesha kisiasa kuliko kitaalamu, huduma za maji ambazo bila kuwa na mikakati ya kueleweka, kuna siku maji yatakuwa shida kubwa kupatikana maana sources zake zinaharibiwa wakati matumizi yake yanaongezeka kutokana na mahitaji kukua.
Tusisahau pia, baada ya Telecom na physics era ambayo inatamba sasa mbele yetu suala la biotech linakuja na kwa kweli hatujajiandaa vilivyo kuhakikisha tuna benefit nalo.
Kama azimio la sasa ni kilimo kwanza then bio tech itahitajika tena sana. Wahandisi tunatakiwa kutoa michango yetu hapo.
Tupe way forward mkuu ili mambo yawe yanaenda kiukweliukweli na ningeomba suala la muda gani mtu amegraduate likae pembeni maana kuna kina kengele halau sijui itakuwaje
 
Magezi

Hilo ni wazo zuri.Je una design yoyote ya windmill? Kwa sababu kama una idea/ drawing ya aina yoyote tunaweza kujiunga na kutengeneza prototype, mimi nilikuwa na wazo kama hilo. Wasiliana na mimi email, yangu ni onset09@gmail.com
 
Magezi

Hilo ni wazo zuri.Je una design yoyote ya windmill? Kwa sababu kama una idea/ drawing ya aina yoyote tunaweza kujiunga na kutengeneza prototype, mimi nilikuwa na wazo kama hilo. Wasiliana na mimi email, yangu ni onset09@gmail.com

Nimekupata mkuu ntawasiliana nawe punde
 
Very good idea mkuu, mi nadhani isiwekwe limit ya graduates wa 2002 maana suala kama hili ni kwa Mhandisi yeyote anayejiskia kushiriki kuliendeleza taifa.

Suala la kugenerate umeme ni muhimu sana na hata maji, nisingependa kushea idea yangu in details hapa ila we can discuss this further kwa PM. Check PM yako in the next 30min.

Nasahihisha hilo la limit ili tupeane mawazo pamoja as wahandisi.
 
Jifunzeni kutoka kwa huyo kijana wa Malawi. Kuzungumza na kupanga kusikoisha hakuleti mafanikio yoyote. Kuwa na picha kamili ya tatizo na kufikiria jinsi ya kulimaliza ndipo pa kuanzia. Huyo kijana hakuwa engineer ila alikuwa na msukumo wa kumaliza tatizo lililoikabili familia na jamii yake. Keep us posted on the progress or on the debate if you never go beyond debating.
 
Magezi una hoja muhimu sana
m ni mmoja wapo kwa kweli baya zaidi hawa wazee
wameamua kuwaambukiza hadi watoto na vijana hili
tatizo la ufisadi...embu tusaidie tukiungana tukaja kumalizana
wapi tutapata dhamana....??
 
Nimekaa nikawaza kwamba kwa wale wahandisi tuliomaliza UDSM na wengine watakao penda kujiunga/kushiriki tujipange tuanzishe walau ka kampuni kadogo ka ufundi ili tuweze kukopa pesa benki na kuzalisha japo simple wind mills ambazo tunaweza kuzitumia ku-generate umeme na hata kusukumia maji vijijini.

Sijawa na proposal as such lakini ni wazo tu na siyo wind mills peke yake we can produce so many engineering products lakini lazima tuwe na kitu cha kuanza nacho. Ingawa kwa sasa sipo bongo lakini walioko jamani tuanze sasa.

We have to show that we gained something from the then FOE.

Wazo lako mkuu Magezi zuri sana.
Hata hivyo lina hatari ya kufa kabla hata halijaona dunia-stillborn.
Hapa umeongelea masuala karibu matatu kwa mpigo, masuala hayo yote yana matatizo.
KWANZA Wahandisi mliomaliza mwaka 2002, sasa sijui niwepi, wa Civil, mechanical,elecrical au Process au wote tu kwa mpigo.Nafikiri wahandisi wana taaluma tofauti na hivyo basi conception ya project lazima iwe na wahusika wakuu
PILI Sioni jinsi unavyoweza kuwakusanya hao wahandisi na kufanya kazi pamoja unless kuna a legal and profitable entity ya kuwepo kwake na kuanzisha na hapa namaanisha kuwepo na kampuni itakayoweza kuwaweka pamoja na kufanya kazi kibiashara.

TATU Initial funding ya mradi utakuwaje, na hii ni baada ya kuanzisha hiyo kampuni yenu.Si rahisi kwend kukopa benki ukiwa na wazo tu.Benki watakuulizia collateral kwa ajili ya mkopo utakao chukua.

Mradi uliofikiria ni mzuri sana na una uhakika wa kuleta manufaa kwa nchi nzima , mimi nina windmill ya 3KW ni ya kichina.Hata hivyo inahitaji maintainance kila wakati, hakika tungekuwa na za kwetu hapa ningenunua hza hapahapa.
 
Ushauri wangu ni kwamba build a prototype, then use it to convince\attractive investors with.

In general, sisi wabongo tunafikiria mradi sio kwamba to solve a particular problem or to provide service in a niche market. No. Bali tunaona ni opportunity ya kupewa pesa za dezo kutoka kwa wafadhili/benki. Matokeo yake pesa zinaliwa - umasikini unaendelea. Mtafanikiwa mkiepukaneni na hayo!

Yule kijana wa Malawi (William Kamkwamba) awe mfano wenu....


 
Hey guys mi nimesoma bcom pale,sasa huwezi kuamini i was thinkin of the same thing kabla bwana Magezi hajapost.nina wazo ambalo litapush hii project bila hata kuomba mkopo bank.Naomba bwana magezi tuwasiliane through 0713743898..Na tupange siku watu wote tukutane kudiscuss swala hili cos wasomi nchi hii wameonekana hawana faida kabisa watu tunasoma ili tuajiriwe tu at the end of the day talents na taaluma zetu zinapotea
 
NATOA ONYO/ANGALIZO KWA WAHANDISI WA KITANZANIA....dunia ya leo unaongelea kukutana watu 200 wenye degree za university kutengeneza windmill iliyogunduliwa 1800's????....naona mnakosa U-SERIOUSNESS HAPA....au peo zenu za kufikiria zipo mbali sana na dunia ya leo....

nchi za asian TIGER ECONOMY...watoto wa VETA ndio wanatengeneza electronics devices zote...ENGINEERZ kama nyie wapo bussy na researches na new INVENTIONS....wenzenu china wanarusha satellites angani na kuzi-bomoa zikiwa kwenye orbits...hapo irani wenzenu wanaongelea vinu vya nucklia...nyie mnasahau kuwa tunayo haphapa nyumbani URANIUM.....vijana mkuwe ki-dunia ya sasa...

u must thing ahead of your tymes...mambo ya wind millz ni ya watoto wa shule za msingi na veta.

haya sasa...ndio mnataka kuungana...je majibu ya haya maswali yangu mnayo tayari..au mnaungana kula pombe na kuondoka mmepeana namba za simu bila matendo
1. KWANINI MNAUNGANA KAMA FOE 2002 GRADUATES?
2. MUUNGANO WENU UNA-OBJECTIVES ZIPI?
3. KAMA NI WA KI-BIASHARA...JE MNAELEWA POLICY NA TARATIBU ZA NCHI KATIKA SUALA ZIMA LA KUUZA UMEME?
4. KAMA SIO MUUNGANO WA KIBIASHARA..MTAPATA WAPI CAPITAL ZA KUTENGENEZEA HIZO PLANTS/MILLS?
5. KAMA HAKUNA MAJIBU YA HAYO MASWALI HAPO JUU, JE HUONI KAMA UNATAKIWA KUJIPANGA UPYA KABLA YA KULETA HII MADA HAPA KWETU.

Vijana naomba mujipange sawasawa haya mambo ni mazito sana na kwa kutambua uzito wake tutakuwa tayari kuwapa support ya kutosha kwa kuwa serikali imeshindwa kuinvest kwa wataalamu na ndio maana hatuendelea...tunaishia kutafuta wawekezaji.

NAWAKILISHA HOJA
 
brother from jupiter planet you are right but u dont know if we are all aware of all you are trying to say...Acha kuanza kucrash pasipo kujua unacrash nini pengine ungekuwa wa kwanza kuleta hoja lakini Mr.magezi ameleta hili kwetu tunamshukuru kwani ameonesha mwanga na njia ya wasomi wa nchi yetu kuangana,they say 'a tree doesnt make a forest' sisi hatutaki kufanya biashara bali ni kusaidia taifa letu kwani ndio maana halisi ya elimu tunayoitafuta lakini wengi hili wamelisahau.Speaking of veta unasema wao ndo wanatengeneza ni lini na wapi wametengeneza zikasaidia vijiji vyetu,kwani gas za magari kwetu hapa zitazinduliwa december,kwa developed countries zimegunduliwa mwaka gani??na hao wachina na wairan unaowazungumzia kwanini wapange kwenda kwenye space sasa wakati urusi ilifanya hivyo mwaka 1969? Ni kwasababu kila kitu kina mwanzo,mtoto hawezi kutembea kabla hajatambaa..Unazungumzia shule za msingi ndo wanatengeza embu jaribu kumuliza mtoto wa shule ya msingi wind mills ni nini utapata jibu.Hapa nchini kwetu suala la inventions and discovery halina misingi wala support na ndo maana tunataka kutengeneza grounds kwanza then yote yatafata kwasababu kila mmoja ana mawazo yake na yanahitaji kuunganishwa kwani hilo si wazo pekee la kudiscuss.
'Penye nia pana njia'
 
Nimekaa nikawaza kwamba kwa wale wahandisi tuliomaliza UDSM na wengine watakao penda kujiunga/kushiriki tujipange tuanzishe walau ka kampuni kadogo ka ufundi ili tuweze kukopa pesa benki na kuzalisha japo simple wind mills ambazo tunaweza kuzitumia ku-generate umeme na hata kusukumia maji vijijini.

Sijawa na proposal as such lakini ni wazo tu na siyo wind mills peke yake we can produce so many engineering products lakini lazima tuwe na kitu cha kuanza nacho. Ingawa kwa sasa sipo bongo lakini walioko jamani tuanze sasa.

We have to show that we gained something from the then FOE.

Mkuu mimi ni Telecom systems Engineer graduate from Westminister University - UK 2000 je naweza kujiunga nanyi katika hili ama mnataka graduate 2002 UDSM tu?.
 
Mkuu mimi ni Telecom systems Engineer graduate from Westminister University - UK 2000 je naweza kujiunga nanyi katika hili ama mnataka graduate 2002 UDSM tu?.


unauliza quran msikitini
 
Back
Top Bottom