Wito ;kesho ni muhimu sana ukawepo wewe binafsi kwenye tukio hili.

Kiranja

JF-Expert Member
May 19, 2007
751
336
WITO KUSHIRIKI KWENYE MJADALA WA WAZI WA MUSWADA WA KATIBA KESHO KARMJEE HALL .

Wito unatolewa kwa kila mpenda maendeleo na mpenda Nchi yetu kesho tarehe 07/04/2011 ahakikishe kuwa anawezaa kutenga muda wake na kushiriki katika mjadala wa wazi (public hjearing) utakaofanywa na kamati ya Bunge ya katiba na sheria katika ukumbi wa Karimjee kwa DSM na ukumbi wa Msekwa kule Dodoma .Kwa upande wa Zanzibar bado haijajulikana ukumbi utakuwa wapi ila sehemu ya kamati ya bunge wajumbe wake wataenda Zanzibar .

Ni muhimu sana kushiriki zoezi hili na tuache kulalamika kwenye maandishi yetu kwani ikumbukwe kuwa sheria zote mbaya za Nchi hii zilipitishwa kwa hati ya dharura kuwasilishwa bungeni , najata baadhi ya sheria hizo;
1. Sheria ya hati za Muungano
2. Sheria ya kuweka watu kizuizini
3. Sheria ya wahujumu uchumi
4. Mabadiliko ya katiba ya mwaka 1977
5. Sheria ya gharama za uchaguzi.
Ukiangalia mifano ya hizo sheria utaona wazi kuwa kama serikali inataka kuficha ama kuweka jambo ambalo halina manufaa kwa wananchi ila kwa watawala utaona wazi kuwa wanawasilisha sheria chini ya hati ya dharura.
Kushiriki kwako kesho utaweza kusaidia kuifanya serikali ikasikiliza kwani wingi wa watu utawafanya wajue kuwa wananchi wako serious kwenye jambo hilo, na ikizingatiwa kuwa kesho ni sikukuu hakuna haja ya hata mmoja wetu kukosa fursa hii adimu kwani ni muhimu kwa nchi yetu sote.
Wito wangu kama uko DSM na Dodoma hebu tenga muda wako kesho kuanzia saa tatu asubuhi ukashiriki kuelezea hisia zako na hata kama hutasema ni bora tukawepo wengi ili kulilazimisha Bunge na Serikali kuongeza muda wa kutusikiliza.
Bunge na wabunge lazima wajue kuwa wao ni wawakilishi wa wananchi , hivyo jambo kubwa kama hili wanapaswa kuwashirikisha kwanza wananchi , waende majimboni wakawaulize waliowatuma wanataka mchakato uwe wa aina gani, na sio kutuburuza.
Hivyo , nawaomba wale wote kesho tukutane kwenye kutoa maoni yetu ili nsiku zijazo tusiishie kusema kuwa hatukushiriki wakati fursa ndio hii.
Msimamo wangu ni kuwa hakuna haja ya kujadiliwa kwa dharura sheria muhimu kama hii, tuna muda, wabunge waje wakatusikilize ndipo wapeleke maoni yetu ndani ya Bunge na sio mawazo yao kama wanavyotaka kufanya sasa.
Ewe mwana JF hii ni fursa ya wewe kuchangia katika kuleta mabadiliko unayotaka kuyaona , tuache kulalamika na muda wa kuchukua hatua ni sasa.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Ni kweli nami nakuunga mkono.Kama ilivyofanyika mijadala miwili chuo kikuu mlimani basi watu wengi wajitokeze kesho na keshokutwa hata kama hutapata nafasi ya kuongea, lakini ni muhimu ukawepo ili tu serikali ijue kuwa kuna wananchi wanafuatilia suala zima la katiba. Shime wananchi tujitokeze kwa wingi. Ndugu zetu wa Asasi za kiraia jitoleeni kuwatangazia wananchi mitaani kwa spika na vipeperushi, vyama vya upinzani wahimizeni wanachama wenu wote kesho wajitokeze kwa wingi. Tukumbuke hii ni harakati kama ile ya kudai uhuru toka kwa mkoloni mwingereza.
 
Hakuna muda kwa CCM Project huko Karimjee; wakachukue minutes za Public Hearing ya wananchi kutoka pake Nkuruma Hall, UDSM na wana si wana-CCM kuitana kichochoroni Magogoni juu ya Katiba ya Wadau kibao nchini.
 
Tuhakkikishiwe na mchango wa maoni ya udsm ya juzi yamewekwa ndani.
 
Hakuna muda kwa CCM Project huko Karimjee; wakachukue minutes za Public Hearing ya wananchi kutoka pake Nkuruma Hall, UDSM na wana si wana-CCM kuitana kichochoroni Magogoni juu ya Katiba ya Wadau kibao nchini.

Uwezo unao kumbe huwezi kupambana?!! Mbinu ya kuwin ni kujua mbinu zao sasa kama hujaenda ndio nini? wewe siunajiamini una mawazo muhimu na matamu ya kuisaidia nchi yetu? basi nenda pale na siyo ubaki kuandamana tu. Katiba siyo isue ya chama kwa hiyo ushabiki wako peleka kwenu. Mambo ya ccm, cdm, cuf ... kwenye mijadala ya katiba hatuitaki.Na kama unaona ni isue ya kichama basi ccm,cuf,cdm,tlp,nccr,udp tafuteni sehem mkae muibadilishe vile mnavyopenda iwanufaishe kichama, na kama siyo ivo basi acha ushabiki kwenye isue critical kama ambayo wengine imetuumiza toka 1977,wanaharakati wa dhati wameanza long time kuipigania hii
 
Samahan nauliza kwa sisi wamikoani hakuna Tv au Redio itakayofanya live hii Public hearing ya dar au Dodoma japo tujue kinachoendele na maoni yanayotolnwa.. Tukipata live hhyo ittujenga sana
 
Back
Top Bottom