Rubi
JF-Expert Member
- Oct 5, 2009
- 1,615
- 326
Wimbo Nibebe wa Rose Muhando umechaguliwa na watanzania kuwa Wimbo bora wa Injili kwa mwaka 2009. Wimbo huu umeshika namba 1 baada ya kuzipiku nyimbo 30 zilizotolewa na TBC1 kama zawadi ya x-mass. kwa kushindanishwa kwa siku tatu kuanzia tarehe 25 - 27 Desemba, 2009.
Wimbo wa Nibebe umepigiwa kura zaidi ya 7000 na kushika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na wimbo wa Bwana Yesu ni tegemeo langu na Wimbo wa tatu ni Waraka wa Bahati Bukuku uliopata kura 6000. Washindi wamejipatia vikombe pamoja na pesa taslimu Tshs 50,000 kwa mshindi wa tatu; Tshs 100,000 kwa mshindi wa pili na Tshs 200,000 kwa mshindi wa kwanza.
Hongera TBC1 kwa kipindi kizuri na hongereni waimbaji wote maana nyimbo zenu hakika ni nzuri na mchuano ulikuwa ni mkali sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu kutabiri mshindi.
Wimbo wa Nibebe umepigiwa kura zaidi ya 7000 na kushika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na wimbo wa Bwana Yesu ni tegemeo langu na Wimbo wa tatu ni Waraka wa Bahati Bukuku uliopata kura 6000. Washindi wamejipatia vikombe pamoja na pesa taslimu Tshs 50,000 kwa mshindi wa tatu; Tshs 100,000 kwa mshindi wa pili na Tshs 200,000 kwa mshindi wa kwanza.
Hongera TBC1 kwa kipindi kizuri na hongereni waimbaji wote maana nyimbo zenu hakika ni nzuri na mchuano ulikuwa ni mkali sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu kutabiri mshindi.