Naam sasa hii naikubali kabisa. Mchanganyiko kati ya vijana na wazee na wapya na wazamani kidogo. Kilichobaki kwetu CCM kushirikiana na Rais wetu, katika haya:
1. Tuwe wazi katika majadiliano ya marekebisho ya Katiba bila jaziba wala vizuizi kwa wananchi na tuwe na hoja.
2. Tukae mbali kabisa wote wenye tuhuma za ufisadi na tusifanye kosa kuanza kufikiria Rais wa ajaye ambaye ana tuhuma yeyote ya ufisadi hiyo itakuwa ni kujimaliza kabisa! Na wale wanaothibitika wafikishwe mahakamani moja kwa moja bila kujali walikuwa ni akina nani wako CCM, CHADEMA, CUF n.k
3. Swala la Dowans tuachane nalo kabisa kwa kutolipa hata senti
4. Rais pitia safu ya watendaji wakuu Wizarani, Idarani, Tasisi za umma na ikibidi kama itakavyofaa fanya mabadiliko itakavyostahili kwa kuweka watu wanaokubalika, watu wanaojituma, watu wasio na tuhuma za ubadhilifu watu wasiotishwa na phobia au ushabiki wa udini bali wanaojali zaidi uzalendo wa nchi yetu.
5. Hatuna haja ya kukimbizana na kuzuia maandamano wala speech za watu majukwaani (tunawapa umaarufu wa bure) wacha waseme na sisi tuingie katika kuboresha maisha na tutasema majukwaani pia.
Tuangalie nje ya 'box'; wako wana CCM wenye sifa nzuri kibao huko mikoani. Tusingángánie majina ya watu yanayofahamika katika Chama. Aidha hilo ni sehemu ya mambo yayowakera wengine na kufikiri kuwa Chama kina wenyewe fulani wachache.
Kila la kheri, nimeanza kupangusa vumbi ya kadi yangu na kuchapa mzigo wa kuongeza uzalishaji nchini kwetu.
Maana yake hawajiamini, hatuna chama tawala!
Duh! Kumbe kuna watu bado wana imani na CCM? Kweli mazoea yana tabu!
Koo ya kwanza ndani ya nyumba.Bado zingine sita.Nasubiri.
Duh! Kumbe kuna watu bado wana imani na CCM? Kweli mazoea yana tabu!
Uko sawa kabisa dada Regia hawachezi mbali wanabadilishana kama mashati.Koo ya kwanza ndani ya nyumba.Bado zingine sita.Nasubiri.
hapa wamepatamwigulu mchemba, headboy ilboru sekondari. Mbunge tabora. Worked at bot. The rest his close buddies will provide. But all iborians mid 1990's remember him....at last! True colours. Colours true
Eti wenyewe wanasema Chama Kinajivua Gamba ha ha haaaa
Jamani tuwe objective kidogo, hapa CCM wamepiga bao kiaina. Kumweka Nape na January kwenye Sekretarieti (sp) wamepata hazina ya vijana wa kidotcom ambayo ni upgrade mara 50 ya iliyopita. Kama Nape na January wakiamua kufanya kazi kwa mapenzi ya nchi, na January akawaweka pembeni hao kina RA & EL, itasaidia sana.
Tuwape pongezi vijana wenzetu wanapopata nafasi, then uko mbele tutawajudge namna watakavyoact.
Hongera sana January na Nape.
Inaonekana na Mwigulu Mchemba, naye ni kijana mwenzetu. Hongera Mwigulu na wewe, tunawatakia mafanikio mema.
Msimamo mnaotakiwa kusimamia ni very simple, Maslahi ya walalahoi yawe mbele siku zote na mafisadi wapingwe hata kama waliwasaidia uko nyuma kipesa.
Jamani Nyani Ngabu.Upo?nimefurahi kukuona tena.
Tusingeweza kuelekea uchaguzi 2015 tukiwa na wazee kama mzee Makamba... Ni lazima tubadilike
Yaani licha ya madhambi yote ambayo CCM imeyafanya kuna watu bado wana matumaini na hawa jamaa? Nashindwa kabisa kuelewa!
Haya mamtu ya CCM ili somo liwaingie, yanatakiwa kuwekwa benchi kwa muda wa kutosha. Ni hapo tu ndipo yatakapojifunza.
Lakini hii ya kuyapigia makofi yafanyapo mabadiliko ya viini macho wala haitasaidia kitu. Tayari yashasoma yanadili na mijitu gani na yenyewe yalivyo majanja tayari yashajua namna namna ya kulicheza gemu. Yakiharibu kidogo tu yatakuja na vimisamiati vingine....safari ijayo huenda yakaja na "kujimenya".
Siasa za bongo bana.
Nani aliyesema haya mkuu...Tusingeweza kuelekea uchaguzi 2015 tukiwa na wazee kama mzee Makamba... Ni lazima tubadilike