Wikiendi kwa umakini zaidi...

Mkeshahoi

JF-Expert Member
Jan 4, 2009
2,469
281
NIICHOTA KAMA ILIVO...

Wizi wa kupulizia dawa za kulevya kwenye vipeperushi jijini Dar es Salaam

Kufuatia ugumu wa maisha, kunawizi umeingia Dar es salaam na inawezekana ukasambaa hata kwenye miji mingine mikubwa. Wizi huo uko hivi

1. Unaweza kupewa kipeperushi ambacho kimepuliziwa dawa na baada ya kupokea aliyekupatia ambaye anajifanya anauza bidhaa anazozitangaza kwenye kipeperushi hicho anakufwatilia kwa nyuma na gari nyingine na kukupora kila kitu baada ya wewe kupoteza fahamu.

AU

2. Ukiwa unaendesha gari vijana wanakufuata na kukushitua kuwa gari inawaka moto then utafungua dirisha kutaka kuona na pengine kusimama. Watakwambia hakuna kitu vijana wanakudanganya hao. Ndani ya muda huo mfupi kwa namna ya ajabu ukifungua tu dirisha wanakupulizia madawa yenye radha na harufu kama pipi tamuu na kukufuatilia kwa matumaini kwamba utapoteza fahamu na wao kukunyang’anya mali zako including kupora baadhi ya vitu kwenye gari.

HIVYO KUWENI MAKINI UNAPOENDESHA GARI USIFUNGUE VIOO WALA KUPOKEA KIPEPERUSHI AU KUNUNUA NUNUA HOVYO CHOCHOTE KWENYE HIZO FOLENI ZA DAR. PIA WANAFANYA HUO UCHAKACHUZI WA FAHAMU HASA MAENEO YA PETROL STATION NA MAENEO YA MAEGESHO YA MAGARI KAMA MLIMANI CITY.


TRUE STORY:
Kuna jamaa yangu kama wiki mbili zilizopita, alikuwa anatoka kupata moja mbili kutoka baa moja inayojulikana kama Blackpoint iliyopo mjini kati muda wa saa moja hivi jioni, akaja kijana mmoja alionekana anashida sana ya kutaka kusaidiwa nauli, rafiki yangu akawa msamaria mwema akachomoa noti ya 1,000 na kumpatia kijana, rafiki yangu alipokosea ni kumuuliza kijana kwani unaelekea mitaa ya wapi? Kijana akasema anaelekea kimara, jamaa akasema basi twende nitakuacha manzese maana mimi naelekea Sinza. My friend says the guy dressed very smart and he was looking as a graduate who is for that day alikwama kweli nauli, and you can’t even think if he is a criminal.

They started a journey from Posta via Jangwani, alipofika Jangwani anasema aliaanza kujisikia kizunguzungu na kichefuchefu na kulikuwa na foleni kali sana . Akaamua alipofika Magomeni achepuke kushoto ili apate pumzi kidogo nje, then he did not remember what went on until he found himself hospitali ya muhimbili akiwa hajitambui na wala hajui gari yake ipo wapi (he was driving a Mark X), na yeye mwenyewe akiwa bado na mawenge.

Jamani zikumbukeni namba za wenzi wenu kichwani, usiku huo mnamo saa saba za usiku alipopata fahamu vizuri alikumbuka namba ya mke wake, akampigia na akaja hapo hospitali. Gari yake iliyokuwa na vitu vyake kama Laptop, bank cards, simu, etc havijaonekana mpaka tunavyoongea leo.

Madaktari wanasema, alivuta sumu, sasa swali ni je kwa nini yule kijana hakudhurika na hiyo sumu hiyo kwa kuwa walikuwa naye mpaka Magomeni alipoanza kujisikia vibaya? Au ni wimbi la vijana ambao wanakuwa wanakufuatilia na mmoja wao anajitoa muhanga wa kuvuta sumu hiyo na wengine wanakuwa wanakufuatilia kwa nyuma, na wakishakukamata wanakutupa na kumuokoa mwenzao, which I think it is possible.

WATCH OUT!!!
 
Back
Top Bottom