Wiki hii historia mpya ya Tanzania inaandikwa?

mtu wa mungu huwa haandiki kishetani namna hii...........
 
Naunga mkono hoja japo hujawa muwazi nihistoria ipi, najua nitaifa kurudi mikononi mwa umma! Kwamara yakwanza ktk historia ya nchi hii kikwete na mafisadi wenzake watakumbana na nguvu yaumma na ninawaeleza wana jf watz wanasubiri nani alianzishe tu!! Nimewasiliana na wataalam wa maandamano wa tunisia na misri wameahidi kutusuport wanamageuzi dhidi ya serikali dharimu za kiafrika
 
Aise niandikie kwa kilugha chetu nazan ntaweza kukuelewa maana khaaaa jamaa mweee
 
Nadhani title na maelezo haviendani kabisa, umechanganya mambo mengi yasiyoendana kwenye hiyo title, labda ungetitle habari yako kuwa ni habari mchanganyiko, lakini kwa hiyo title inakuwa ngumu kuelewa unamaanisha nini hasa.
 
Ameandika mambo mengi kiasi kwamba unashindwa uanze na lipi,,,
hoja ni nyingi ungeweza kuzitofautisha watu waweze kuzijadili vizuri.
 
Umesahau moja kuu,
Wiki hii CDM iliendelea kusajili magarasa yaliyoachwa na CUF, safari wamemchukua Prof. Safari.
Kumbuka wameshawahi kuwasajili Shaibu Akwilombe, Wilfred Rwakatare nk. Wote hawa hawakusaidia kitu kwenye timu yao mpya!

Kwanini Prof Safari ni Garasha?
Toa Hoja!
Pia ni vema ukajilinganisha naye au hata wale aliowaacha CUF na Kwanini alitoka CUF?
 
The mind of the post bring, is either outside the caverage area or has the brain switched off.
P/se try me later by spacefying issues.
.
 
Hakuna ulichoongea hapa naona umechanganya mambo, mara ushirikina mara bunge mara majini mara falsafa tushike lipi tuache lipi? weka mada moja moja utafeli mtihani pamoja na kuwa na uelewa.

WanaJF tumsaidie mwenzetu jamani!!!!!!!!!!!!!
 
Fuvu la mtu wa kwanza aligunduliwa bonde la olduvai, bila shaka kama kuna kiama kitaanzia Tanzania.
Naona hii inachangia sana kwa wabongo kubaki kwenye zama za jiwe (stone age!). Wakati wengine wanaendelea kisayansi sisi ndio kwanza tunarudi kwenye imani za giza, dah, kaazi tunayo! Wabongooo tuko ovyoooo!!!!
 
Great Thinkers mimba ambayo kwayo Tz Mpya inakwenda kuzaliwa-Tz ya wengi (siyo ya sisiemu milele) inakwenda kutungwa wiki hii ili malezi ya mimba hiyo yaweze kuanza mpaka hatimaye mtoto NEW TZ anazaliwa!!!!!! Kwangu mimi hii ndiyo historia mpya; ni zaidi ya kikombe cha kishirikina ambacho sisiemu na serikali yake wanataka tuamini kwamba dawa ya HIV/AIDS imegunguliwa Tz!!!!!;
 
Hakuna ulichoongea hapa naona umechanganya mambo, mara ushirikina mara bunge mara majini mara falsafa tushike lipi tuache lipi? weka mada moja moja utafeli mtihani pamoja na kuwa na uelewa.
It is Great Thinkers who see deep ndiyo ambao wameelewa na kujiandaa kupokea hiyo historia mpya!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
dah, ebu mada zenu ziwe zinaendana n heading basi. Maana sijaelewa ki2 hapj zaidi ya siasa 2
 
Historia haitaandikwa kwa kuwa muswada wa katiba unamapungufu mengi mno, naomba usipite. Mapungufu ya mswada huo niliyoyaona ni kama ifuatavyo;

1. Jina la muswada halifai, na limeharibu kila kitu ndani ya muswada, unasomeka constitutinal review act, ikimaanisha kwamba kinachofanyika
ni review ya katiba iliyopo siyo kuandikwa kwa katiba mpya.Hii inathibitishwa na kifungu cha 18(2)(b) cha muswada huo ambapo kinaitaka tume
itakayoundwa kurejea na kuzingatia nyaraka za zamani mno katika kufanya kazi yake, ambazo haziendani kabisa na mahitajio yetu ya sasa na miaka mia moja ijayo.
2. Kifungu cha 8 cha muswada huo pia ni tatizo kubwa, kwa kutumia terms of reference ina maana uwanja wa majadiliano na mapendekezo
umepunguzwa, hasa ukizingatia kuwa terms hizo zinatolewa na mtu mmoja tu.
3. kifungu cha 6 (3)(a)and (b) , hakuna logic kuwaharamisha wanasiasa na wanausalama katika kamati
4. mchakato mzima katika muswada huu umetekwa na serikali, kwa kuwa unaanzia na kuishia kwa rais, hii ni kasoro kubwa sana.
5. Kifungu cha 9 (2)(c) na (d) ambavyo vinalazimisha kuendelea kuwepo kwa mfumo wa rais na kuendelea kuwepo kwa serikali ya zanzibar.
Hili nalo ni kosa kwa maana na hayo watuache wananchi tuamue, kwa kuwa inawezekana wananchi wengine wanataka mfumo wa waziri
mkuu mwenye madaraka, ambaye hatokani na kupigiwa kura moja kwa moja bali chama chenye kushinda wabunge wengi ndio kinatoa
waziri mkuu. Pia suala la rais wa zanzibar watuache wananchi tuamue pia, huenda wananchi sasa tunataka kudumisha kabisa muungano
wetu kwa kutokuwa na serikali ya zanzibar chini ya rais wa zanzibar bali serikali moja tu ya tanzania.
6.Kifungu cha 5 tume iundwe na bunge na kurejesha matokeo bungeni badala ya kuundwa na rais na matokeo kutumwa kwa rais
7. Kifungu 26 tume ya uchaguzi isipewe kazi hii kwa kuwa iliyopo ina matatizo na itashughulikiwa na katiba mpya. kazi hiyo ifanywe na tume
maalum ya bunge yenye mchanganyiko wa watu wasio na kashfa hata kidogo kutoka vyama vyote.
8.Kutaka tume hiyo isipingwe mahakamani , na kuweka kwamba ni kosa kufanya hivyo inaharibu dhana nzima ya kuwa na katiba nzuri
iliyotokana na matakwa ya watu wenyewe.
9. Umuhimu wa idadi ya wajumbe wa tume kutokuwa sawa kati ya bara na visiwani bali itokane na percentage ya idadi ya watu wa pande
zote mbili.
 
Kweli kuishi kwingi ni kuona mengi!

1: Muhimu katika habari kubwa na tamu za leo Jumatatu Aprili 4, 2011 - Kumbe kikombe cha Babu wa Loliondo ni USHIRIKINA!!!!!!
2: Rais na waziri wake wa sheria watofautiana na muswada wa katiba wanaowasilisha bungeni wiki hii - kwa waliofuatilia kongamano la UDASA Jumamosi 2,Aprili 2011 watakumbuka cheche za akina Marando na Mtatiro, na Mbowe kurudi kwa umma; vigogo wa CCM waliingia mitini wakamsukumia masikini wa watu Prince Bagenda, ambaye naye kwa kuhofia cheche akaelekeza kwamba waTz wasidhani katiba nzuri itapatikana kirahisi (alinishangaza kama kweli hapa alikuwa anasemea CCM kweli?); kwa wadadisi linganisha habari za HABARILEO ya leo Jumatatu, Aprili 4, 2011;
3: Mjadala na hatimaye kura ya wabunge wiki hii kuhusu muswada wa katiba mpya kuamua kama ni-sisiemu na serikali yake kusalimu amri na kufuta mtazamo waliopeleka bungeni wa rais kuchukua nafasi ya waTz kutengeneza katiba mpya ama katiba mpya kupatikana kupitia pipoooos pawa-ambayo kwa mtindo uliosemwa kwenye kongamano la Jumamosi kuwa ni ule wa Tunisia na Misri, na sasa Libya!
4: Macho YOTE ya waTz kugeuzwa kutoka kwenye ushirikina Loliondo na kuelekezwa kwenye bunge Dodoma-patawaka moto!
5: Hatimaye Tz kubakia kuwa taifa la viongoizi wanaoongozwa na falsafa ya ushirikina-rais kulindwa na majini ya sheikh na sasa serikali yote imejimwaga katika kikombe cha mashetani Loliondo!
6: Bila shaka wanaJf nao hawatabaki nyuma!!

wewe ni wakala wa makanisa ya Nigeria via Tv?!, Pumba tupu. Kwani Wengine ni watu wa shetani?
 
Back
Top Bottom