Julieth Ms
Senior Member
- Nov 29, 2011
- 102
- 37
Jamani mwenzenu na wifi yangu mke wa kaka angu baada ya kuukwaa Ukurugenzi huko Dodoma ameanza nyodo zilizo pitiliza wakati nilimpokea mwenyewe mjini kaja kujiendeleza kimasomo Chuo kikuu na tulikuwa tunakula dagaa leo hii amepata ukurugenzi anasema hawezi kabisa kufika kwangu anataka alale guest nilipo muuliza mbona pakulala nimekuandalia akasema hadhi yake hawezi kabisa kulala kwangu mitaani pale guest bei gani chumba nikamwambia zipo za Tsh.10000-30000/= akasema hakuna guest yenye hadhi ya kulala yeye akaniambia anaenda Sinza kulala kwenye guest za hadhi yake kwakweli ubinadamu kazi jamani.