Elections 2010 Why Dr. Slaa...?

Pape

JF-Expert Member
Dec 11, 2008
5,488
79
Kwa maana jinsi hii Mungu aliipenda Tanzania, hata akamtuma Dr Slaa (a.k.a Silaha ya maangamizi) ili kila mtanzania atakayemkubali na kumchagua katika uchaguzi wa rais mwaka huu 2010 apate ukombozi wa kweli, kuondokana na dhuluma na ufisadi. Ni zamu ya CCM kuaga, tumeonewa na kukandamizwa kiasi cha kutosha. Kwa miaka mingi sasa patakatifu (ikulu) pamekuwa kituo kikuu cha usanii na siasa za 'matumbo'. Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Dr. Slaa. Chagua Dr.Slaa chagua Chadema!!!
 
Mungu usikie kuomba kwetu, wataruka ruka lakini mwisho wao u karibu, mungu anachukizwa na dhuluma na ufisadi wa jasho la wa tanzania wasio na hatia wanakamuliwa kila kukicha kwa kodi na michango lakini watu wanazitia mifukoni, serikali imekodishwa na chama, askari wanafanya kazi za chama,sasa si heri iitwe tu jeshi la kujenga ccm au jeshi la wanachama wa ccm, au jeshi la usalama wa mafisadi na uwizi wao, na mali zao za uwizi. Lakini iko siku. Daudi alimuua goliati kwa jiwe kutumia kombeo,sasa wao na bunduki zao mungu atawashughulikia kwa maombi na machozi ya watanzania wanao nyonywa kila leo. Takukuru nawaonya msinitumie sms za ajabu kwenye simu yangu mnanipa kazi ya kufuta sms na kunimalia charge ya simu yangu bure, hakuna kitu mnafanya, mnafikiri sisi wajinga hatuelewi mchezo wenu. Kama vipi semeni alichofanya mh marmo mbulu, ok zile simu alizogawa rostam kwenye mkutano wa hadhara na matusi juu. Iko siku kitaeleweka tu. Haki yako ni haki yako tu hatakwakunyakua,
 
Kwa maana jinsi hii Mungu aliipenda Tanzania, hata akamtuma Dr Slaa (a.k.a Silaha ya maangamizi) ili kila mtanzania atakayemkubali na kumchagua katika uchaguzi wa rais mwaka huu 2010 apate ukombozi wa kweli, kuondokana na dhuluma na ufisadi. Ni zamu ya CCM kuaga, tumeonewa na kukandamizwa kiasi cha kutosha. Kwa miaka mingi sasa patakatifu (ikulu) pamekuwa kituo kikuu cha usanii na siasa za 'matumbo'. Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Dr. Slaa. Chagua Dr.Slaa chagua Chadema!!!
Dah nilikua sijaipata hiyo, silaha ya maangamizi :becky:
 
Back
Top Bottom