Who is MZUNGU?

Conclussion:Mzungu ni mtu mwenye asili ya bara la ulaya mwenye tabia ya kuzungukazunguka.kwa hiyo hata kama yupo US,TZ,RSA bado ataitwa mzungu kwani origin yake ni ulaya.
 
Conclussion:Mzungu ni mtu mwenye asili ya bara la ulaya mwenye tabia ya kuzungukazunguka.kwa hiyo hata kama yupo US,TZ,RSA bado ataitwa mzungu kwani origin yake ni ulaya.
Hapa napenda kusumbua kidogo:
a) kwa vizazi vingapi asili ya mtu iko sehemu fulani? Ama Ulaya (mfano makaburu wa Afrika Kusini) au Afrika (mfano akina Michelle Obama). Yaani ngozi na rangi ni milimita 0.3 pekee ya mwili, na damu ni majimaji yenye chumvi tu. Tena kama kizazi ni cha mchanganyiko utasemaje? Kuanzia kiwango gani? Yaani baba mzungu mama Mwafrika ni nani? Mama mzungu na bana mwafrika ni nani? Babu 1 mzungu na wengine waafrika ni nani? Babu 1 mwafrika na wengine wazungu ni nani? Mnajua Malkia Elizabeth wa Uingereza ana kababu mwafrika katika kizazi - cha- ngapi ndani yake? Na wataalamu wa elimukoo (genealojia) wanasema leo hii kila mtu wa namna fulani ni ndugu wa damu na kila mtu mwingine kutokana na mchanganyiko wa watu katika historia.

b) hasa hao wa Ulaya - je si kweli ya kwamba anthropolojia inasema watu wote duniani mababu walitoka Afrika na kuhamia pande nyingine za dunia? Kwa hiyo - si wote Waafrika kuanzia Ulaya hadi China?
 
Kuhusu asili ya neno mimi nimesikia yafuatayo (lakini siwezi kuyathebitisha):
Wazungu wa Kwanza Afrika ya Mashariki walikuwa Wareno lakini hawakuitwa "wazungu".
Neno hili limetokana na hao wapelelezi wa Afrika na tabia yao ya kuzunguka kote bila kukaa mahali pamoja. Yaani watu hao kama Livingstone, Burton, Speke na wengine.
Labda pia wa sababu kutokana na kuzunguka kwao walionekana kama watu wenye hali ya kizunguzungu?

Hata mimi nafahamu hivyo kuwa hawa wazungu walipoingia walikua wanazunguka sana kwa utafiti wao ndio wakaitwa wazungu yaani wazungukaji au wanaotuzunguka. Na mzungu ni mtu mweupe mwenye asili ya ulaya mfano muingereza , mjerumani n.k
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom