utemi
Senior Member
- Mar 27, 2011
- 167
- 23
Ni nani anayemjua vyema huyu ndugu?
Nasikia ni “Nabii”
Je, huduma yake ipo wapi?
=============
============
Nasikia ni “Nabii”
Je, huduma yake ipo wapi?
=============
Huyu ndugu jina lake halisi ni George David Kasambale. Ni mwenyeji wa Singida. Mimi nilianza kumfahamu miaka ya tisini, alikuwa tarishi pale world vision, Arusha. Alikuwa pia mwanamziki wa nyimbo za injili ktk mikutano mbalimbali na alikuwa anasali ktk kanisa la Siloam Gospel Assembly lililokuwa linasali ktk shule ya msingi Uhuru Arusha.
Kwa kipindi hicho, mimi nlikuwa mwanafunzi wa primary. Tulikuwa tunamuita Nyakizanya kwa sababu ya wimbo wake maarufu ''Nyakizanya umeokoka'', ila alikuwa kijana wa kipindi kile na alikuwa ana mambo yake ya ujana kama kuvaa mabegi na kunyoa pushback, kitu kilichomfanya asikubalike na wachungaji wengi wa kiroho hapa Arusha.
Sikumsikia tena hadi miaka ya kuanzia 1996 hivi. Alikuwa na studio ya nyimbo za injili iliyoitwa Supreme na baadae ikawa radio station ila ilikuwa inasikika baadhi ya sehemu za Arusha. Ila kutokana na ujanja ujanja wake na ambitions yake aliweza kukutana na wazungu na kufungua kituo cha watoto wa mitaani ingawa alikuwa anao kama watano hivi wa kuzugia.
Kituo hichi kilikuwa majengo karibia na Sacon, Opposite na kanisa la KKKT Burka, baadaye alihamia Kisongo baada ya kuwa na fedha, aliwaondoa wale watoto kwa namna mbaya sana mmojawapo ni rafiki yangu ni fundi TV, ndio ghafla tukasikia Nabii GeoRDavie, kanisa lake liko Kisongo Mnadani na ofisi zake ziko huko ktk mashamba yake maarufu kama ''mji wa Daudi''. Kwa kweli huduma yake imejaa contrevesial sana, maisha yake pia yana utata.
Means jinsi anavyo-behave, pamoja na family life yake kwa ujumla watu wanaomfahamu tangu kitambo hawamuelewi. Ila hatuwezi kusema sana tusije tukakufuru ila kwa upande wangu mmhh.
Simkubali na hii ni kutokana na matendo yake, yaani tabia, huwezi kuwa na upako kiasi hicho afu matendo ni design kama yake. Ila sijui!
Siwezi sema ni mtume wa Mungu au la ila kuna maswali mengi sana kuliko majibu.
============
Mhe. Nabii GeorDavie ni mtumishi wa Mungu. Anaijua kazi yake, anajiamini, ni shujaa, anajitambua na anaielewa kazi yake. Anamwakilisha Mungu ipasavyo. Anamwelewa boss wake vizuri na hana mashaka naye. Hajali maneno wala haogopi vita kwa kuwa anamwelewa Mungu aliyemwita na kumtuma. Kama tujuavyo shetani ni mpinzani wetu hivyo kurusha makombora ni kitu cha kawaida.
Maelfu ya watu yameshuhudia matendo makuu ya Mungu. Mara nyingi shuhuda zimekuwa zikiwekwa kwenye Radio ya Ngurumo FM Hata hao wakina Channel na watumishi wote waliokengeuka kwa sababu zao wanazojizua walishuhudia, tena walikuwa hawamjui Mungu lakini wamefungua makanisa. Ikiwa wanakufuru matukufu ya Mungu na kusema ni Nguvu za giza, je wao wanatumia nini na wamejifunzia pale?
Tena channel alishuhudia na kusema upako huu ni mtaji kwangu! Wivu ni wa nini watu wa Mungu? Mara ooh kuna mwanamke alifunga macho na alipofungua akaona nyoka mara akafa, inaingia akilini??? Tunaomba kumjua huyo mwanamke ayekufa na ushahidi.... Ni uongo wa Ibilisi jamani, nendeni mkajionee matukufu ya Mungu... Shetani anaharibu kazi ya Mungu lakini ameshindwa.... Kazi ya Mungu inasonga mbele!
Mnashangaa misafara na magari ya kifahari, Mungu ni tajiri atumie hata ndege za angani kumtukuza Mungu! Eti anaitwa mheshimiwa, sasa kama mafisadi wanaitwa waheshimiwa vipi watumishi wa Mungu?!!
Mimi ninasema GeorDavie amemwelewa Yesu na ndiye mtumishi anayemwakalisha Mungu ipasavyo. Hivi mimi kama ninatembea peku na ninakuambia Mungu ni tajiri anaweza kukusaidia kiuchumi utanielewa kweli?!! Unajua mtu ajionavyo ndivyo alivyo.
Ukimwona Mungu unayemwamini hawezi kuponya, kwako kitu kama hicho kitabaki kuwa story, ukiona Mungu unayemwamini anatawala mbinguni na kumiliki duniani na mamlaka alishatupatia ndivyo itakavyokuwa kwako. Wengi hapa wamebaki kumuhukumu na kumkatisha tamaa kwa kazi anayoifanya, na kupakaza mambo ambayo hayana maana. Ila kwa muelewa inaonyesha wazi ni maadui, wivu, chuki kwani sielewi kwanini kinawauma sana.
Kama kweli mnampenda Mungu na mnamjua Mungu, kwanini msimwombee? Mnampiga vita yeye ni mwanadamu kama wanadamu wengine. Wengi walisema anatumia nguvu za giza, wakafunga na kukemea na kuharibu ikaishia GeorDavie kuinuliwa nao wakashushwa! Mwacheni Mungu aitwe Mungu! Mungu akimpenda mtu na kumchagua afanye kazi yake atamtumia mpaka atakapomaliza haijalishi chochote!
Yeye ndiye atakayemhukumu na wala sio mwanadamu! Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote kwani anaangalia utayari wa mtu alionao. Kweli GeorDavie ni shujaa katika mashujaa otherwise angekuwa mtu wa kawaida katika vita zote alizopitia angekimbia na kumwaibisha Mungu. Lakini yeye anasonga mbele akicharaza mapepo. Mungu anawapa watu karama tofauti.
Na maandiko yako wazi, alisema wengine ni Manabii, mitume, wachungaji, waalimu na wainjilist kama yeye amepewa upako wa Kinabii wivu ni wa nini wanadamu??? Hamna jema.
Mtumishi asipotembea na Nguvu za Mungu mnasema hajaitwa, akiwa na nguvu za Mungu mnasema anatumia nguvu za giza, lipi jema kwenu!? Acheni kumnyoshea mtumishi wa Mungu kidole, angekuwa hajatumwa tangu mmeanza kumpiga vita ametikisika??!! Huduma imekufa???
Kitu cha Kimungu hata upambane vipi huwezi kukiharibu! Hamtamweza Nabii huyu mpaka Mungu akamilishe kusudi lake aliloweka ndani yake. Haijalishi punda amechafuka au amelowana lazima safari aimalize na kusudi la Mungu litimie! Lakini ole wake yule ambaye hakumsaidia punda kukamilisha kusudi la Mungu kwa wanadamu! Je, umehusika kufanya nini?? kumchafua, kumwangusha, ulimlisha, ulimtemea mate, ulimpaka marashi?? Ulishiriki vipi kuhakikisha kazi ya Mungu inasonga mbele??
Mungu kumtumia mwanadamu hamaanishi ni malaika! Shida watu hawasomi maandiko na kuelewa neno la Mungu. Nchi yetu hii inanishangaza, kazi kupinga watumishi wa Mungu na kuwaombea mabaya huku wakiwainua watumia mizizi waliojaa udanganyiifu!
Nabii akiwaambia huko siko wanakimbilia hawamtaki Yesu! sasa wanaanza kulalamika ooh tulidanganywa... Tafuteni uso wa Mungu wanadamu na kumwabudu yeye pekee dunia hiini ubatili mtupu.