Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
- Thread starter
- #41
SI KWELI HATA KIDOGO NA KAMA HUMJUI MTU USIMZUNGUMZIE SIO VIZURI NA WALA SIO USTAARABU,MIMI SIO MSHABIKI WA CCM LAKINI NAMJUA BENO MALISA VIZURI SANA NASEMA HE IS MY FRIEND TOKEA ZAMANI NA BADO NI RAFIKI YANGU THOUGH TUNAPINGANA KIMITAZAMO LET ME GIVE A BIT OF HIM;
-BENO ANA AKILI SANA ZA DARASANI NA ZA MAISHA
-NI MTULIVU NA ANA AIBU YA KUONGEA KILA SIKU NAMUULIZA ALIINGIAJE KWENYE SIASA ILHALI SIO MSEMAJI
-NI MTOTO WA MKULIMA NA AMELELEWA KIPADRI SANA,KWA HIYO ANA MAADILI YA KIKATOLIKI
-AMESOMA HIMO PRIMARY SCHOOL NA BAADAE MARANGU SECONDARY THEN DON BOSCO HIGH SCHOOL ,HALAFU LLB UDSM
-ANA MASTERS YA SHERIA LLM
-ALIMSAIDIA SANA RIDHIWAN KIMASOMO UDSM KWANI MTOTO WA RAISI ALIKUWA KILAZA WA KUTUPA
-WALE WANAOKUMBUKA KAMPENI ZA RIDHIWAN PALE UDSM BENO HAKUWA MSEMAJI HATA KIDOGO ALIKUWA THINK TANKER WETU NA MIMI NILIKUWEPO NA NILIKUWA MSEMAJI SOMETIME NOT ALWAYS ,BENO ALIWEZA KUPANGA MIPANGO NA IKAPANGIKA
-AMEALIKWA MARA NYINGI NYUMBANI KWA JK NA ANAIJUA FAMILIA YA JK TOKEA AKIWA UDSM,MARA KADHAA TUMEENDA PAMOJA KULA BIRTHDAYS NA WINE ZA NYUMBANI KWA WAZIRI WA MAMBO YA NJE
-UTULIVU WAKE NA POSITIVE MIND ZIMEMFANYA KUKUBALIKA HATA NA MAFISADI NDANI YA CCM NA HATA SISI WA UPINZANI TUNAMKUBALI KWA KIASI
-KILA MWANACHAMA MWENYE JINA NDANI YA CCM ANAAMINI BENNO NI KICHWA NA KWA SABABU YA UPOLE WAKE ANA WAKUBALI WOTE HAWEZI KUSEMA HAPANA
-HAJANUNULIWA NA MAFISADI ILA HANA MSIMAMO
ANAWEZA KULETA MABADILIKO LAKINI SIO KUONGOZA MABADILIKO
msimlaumu sana amezungukwa na watoto wa mafisadi ila ni MTU SAFI
Mkuu Son of a Peasant, Heshima mbele...
Sitaki kupinga hoja zako, hasa kwa kuzingatia kuwa umesema kuwa ni rafiki yako na unamfahamu kwa karibu sana, pengine kuliko mchangiaji mwingine yeyote. Hata hivyo, kuna hoja ambazo ni controversial kwenye post yako, naomba ufafanuzi...
Kwamba Benno ni mkimya, na ana maadili... nadhani hili ni relative term, kwangu mimi Benno sio mkimya, wala sidhani kama ana maadili kihivyo. Huyu jamaa, nilikuwahi kukaa naye Makuti Hotel, mjini morogoro, kwa kama saa mbili hivi. Alikuwa anasafari ya Dodoma I think, na alipita pale kukutana na rafiki yake ambaye walisoma pamoja huko sekondari, na kwa kuwa huyo rafiki yake ni rafiki yangu pia, nilijikuta nikiwa katika ya mazungumzo yao. By then (2006 au 2007), sikumpa attention sana kwa kuwa hakuwa kiongozi, but nakumbuka sana maongezi yake, stori alizokuwa anapiga, staha na haiba yake... kwa kweli kusema ni mkimya, au ana maadili... kwangu mimi hakukaribia kabisa viwango.
Pili, kuwa Benno hajanunulika... mh, unless unipe strong evidence ndugu yangu, maana hata kwama umeongea naye, usidhani angeweza kukuambia hilo... Lakini ushahidi wa kimazingira, kutokana na kauli ambazo ama anazitoa mwenyewe dhidi ya wapinga mafisadi (ndani na nje ya CCM), kwa kweli itakuwa ngumu sana kusema kuwa ni 'mtazamo' wake, hasa ukizingatia anaoelekea kuwatetea.
Tatu, kusema kuwa Benno ni 'kichwa' napata kigugumizi kidogo. Kama Benno ni kichwa, na kama alilelewa katika mazingira ya utulivu na yasiyo na bughudha za kimaisha, nungetarajia angefaulu darasa la saba pale Himo primary... Kwa nini alifeli??????????? .kufeli hapa namaanisha hakuchaguliwa kuingia sekondari za serikali, kama Old Moshi (ordinary) au akina Ilboru (special) n.k. Kumbuka kipindi kile hakukuwa na shule nyingi za kata, na shule za serikali zilikuwa zinaheshimika sana. Inawezekana kuwa ni kichwa kweli lakini pengine kutokana na umapepe, na kutokutulia kwake (kinyume na ulivyotuambia) akawa hazingatii masomo, akashindwa kupata maksi za kwenda government...
Kweli hana msimamo? Mbona kama anasimamia upande wa mafisadi?
Nasikitika siku ile vilipokuwa vinatoa tamko la kumtukana Slaa, kabisa niliamini Benno hakuhudhuria kikao kile, lakini nilikuja kuishiwa nguvu kuona kuwa alikuwepo, tena ndiye aliyeongoza kikao!!!, ambapo Rz1 hakudhuria...
Son of a peasant... come again my friend.