Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
Wakuu naomba tuangalie issue hii kwa mapana, tusiangalie kwa mtizamo wa mvutano kati ya CCM na CDM, kwani tunaona kuwa nchi yetu imefika hatua ambayo naweza kusema tunaonekana kuchangamka kisiasa.
Nakumbuka by election ya kwanza kabisa ilifanyika hapa Tanzania mwanzoni mwa miaka ya 90 (may be 92), enzi hizo Horace Kolimba akiwa katibu Mkuu wa CCM. Kulikuwa na kina Komba na waiambaji wengi wakiwakejeli wapinzani na wapinzani wenyewe hawakuwa organised hata kidogo. CCM ilishinda kiulaini sana, kama nakumbuka vizuri kulikuwa na by election Mbozi, Igunga na jimbo lingine sikumbuki ni lipi. Uchaguzi wa wagombea ulikuwa very smooth, na ndani ya CCM kulikuwa shwari kiasi.
CCM haikuhitaji kutumia nguvu sana kushinda, haikuwa na haja hata ya kufikiri kuchakachua, hakukuwa na haja ya rais mstaafu, waziri mkuu mstaafu, kamanda mkuu wa polisi, katibu mkuu wa chama, mkuu wa mkoa au hata maofisa wa juu wa usalama wa taifa na mkoa kwenda majimboni kuhakikisha kuwa CCM inashinda. CCM ilikuwa inashinda by default, na wengi kwa wakati huo tulikuwa tunaona kuwa wapinzani wote ni makapi ya CCM na waganga njaa. Imani hii iliongezeka pale mwenyekiti wa TPP Alec Che Mponda, alipotangaza kuwa chama chake kimeshinda by election kwa kupata nafasi ya pili, kwani alisema haitawezekana kamwe kuishinda CCM. Kuna siku pia aliitisha maandamano yasiyo na maana, na kutufanya tuwaone kuwa wapinzani ni waganga njaa. Watanzania wengi tukaona kuwa wapinzani ni kundi la wahuni tu.
Matumizi ya vyombo vya dolam hayakuwa makubwa, idara ya usalama ngazi ya wilaya na polisi ngazi ya mkoa na wilaya waliweza kushughulikia maswala ya uchaguzi na uchaguzi ulikuwa unaisha kwa amani kabisa.
Hakukuwa na lugha za matusi, hasa kutoka kwa CCM, wapinzani ndio walikuwa wanatoa matusi, hadi kuna wakati Horace Kolimba akawa anasema wanakashifu chama.
Ni miaka 20 imepita sasa, hali inaonekana kuwa tofauti sana. Uchaguzi wa Arumeru umeonesha picha tofauti kabisa. Sina haja ya kutaja ni vigogo gani wamekwenda huko, wengi tu wa chama, serikali, polisi na idara ya usalama. Idadi kubwa ya wana usalama kuliko idadi ile ya waliokwenda Zanzibar, sina haja ya kutaja matusi yaliyoporomoshwa kule, sina haja ya kutaja rushwa waziwazi iliyoetembea kule. Walipo Arusha wanaweza kusema mengi zaidi yaliyotokea huko.
Sasa hivi ni wazi kuwa ndani ya CCM kuna makundi mawili, CCM-Asili na CCM-Mtandao, tumeona jinsi walivyotumia mbinu za ajabu kupitisha mgombea. Kundi moja lilitoa rushwa na ikatangazwa wazi, na kundi lingine(lile linalopinga ufisadi) likakaa kimya. Even worse wapinzani nao wamekaa kimya as if ni halali. Tume yetu ya uchaguzi imeendelea kuwa ya kutia mashaka, tumesikia kuwa masanduku ya kura yamekamtwa yakiwa yamejaa kura zilizopigwa na iko kimya tu.
Inaonekana sasa kuwa wapinzani, are not as hopeless as we saw them in 1992, CCM will not win by default as was in 90's, sasa inabidi itumie nguvu zote ilizonazo kushinda uchaguzi. Mtaji wa CCM kushinda uchaguzi kiurahisi kama ilivyokuwa igunga, mbozi na kwingineko ambao Profesa Baregu alisema ni unyonge wa kiuchumi na kielimu walionao wapiga kura katika maeneo husika,a huenda una ukomo. Na matumzi ya vyombo vya dola kwenye uchaguzi inaonekana ni makubwa na makini zaidi kuliko katika kupambana na uhalifu unaotuliza kila siku, hii si dalili nzuri kwa watu tuliozoea kupiga kura tukisimamiwa na mgambo wenye marungu. Tumetoka mbali lakini tunakwenda mbali zaidi.
Hatua iliyofikia CCM sasa ya kutumia nguvu kubwa kushinda by election kwa lolote lile inatia shaka. Hali hii ikisambaa nchi nzima kuna uwezekano kukawa na hali ya ajabu nchini kwetu.
Nakumbuka by election ya kwanza kabisa ilifanyika hapa Tanzania mwanzoni mwa miaka ya 90 (may be 92), enzi hizo Horace Kolimba akiwa katibu Mkuu wa CCM. Kulikuwa na kina Komba na waiambaji wengi wakiwakejeli wapinzani na wapinzani wenyewe hawakuwa organised hata kidogo. CCM ilishinda kiulaini sana, kama nakumbuka vizuri kulikuwa na by election Mbozi, Igunga na jimbo lingine sikumbuki ni lipi. Uchaguzi wa wagombea ulikuwa very smooth, na ndani ya CCM kulikuwa shwari kiasi.
CCM haikuhitaji kutumia nguvu sana kushinda, haikuwa na haja hata ya kufikiri kuchakachua, hakukuwa na haja ya rais mstaafu, waziri mkuu mstaafu, kamanda mkuu wa polisi, katibu mkuu wa chama, mkuu wa mkoa au hata maofisa wa juu wa usalama wa taifa na mkoa kwenda majimboni kuhakikisha kuwa CCM inashinda. CCM ilikuwa inashinda by default, na wengi kwa wakati huo tulikuwa tunaona kuwa wapinzani wote ni makapi ya CCM na waganga njaa. Imani hii iliongezeka pale mwenyekiti wa TPP Alec Che Mponda, alipotangaza kuwa chama chake kimeshinda by election kwa kupata nafasi ya pili, kwani alisema haitawezekana kamwe kuishinda CCM. Kuna siku pia aliitisha maandamano yasiyo na maana, na kutufanya tuwaone kuwa wapinzani ni waganga njaa. Watanzania wengi tukaona kuwa wapinzani ni kundi la wahuni tu.
Matumizi ya vyombo vya dolam hayakuwa makubwa, idara ya usalama ngazi ya wilaya na polisi ngazi ya mkoa na wilaya waliweza kushughulikia maswala ya uchaguzi na uchaguzi ulikuwa unaisha kwa amani kabisa.
Hakukuwa na lugha za matusi, hasa kutoka kwa CCM, wapinzani ndio walikuwa wanatoa matusi, hadi kuna wakati Horace Kolimba akawa anasema wanakashifu chama.
Ni miaka 20 imepita sasa, hali inaonekana kuwa tofauti sana. Uchaguzi wa Arumeru umeonesha picha tofauti kabisa. Sina haja ya kutaja ni vigogo gani wamekwenda huko, wengi tu wa chama, serikali, polisi na idara ya usalama. Idadi kubwa ya wana usalama kuliko idadi ile ya waliokwenda Zanzibar, sina haja ya kutaja matusi yaliyoporomoshwa kule, sina haja ya kutaja rushwa waziwazi iliyoetembea kule. Walipo Arusha wanaweza kusema mengi zaidi yaliyotokea huko.
Sasa hivi ni wazi kuwa ndani ya CCM kuna makundi mawili, CCM-Asili na CCM-Mtandao, tumeona jinsi walivyotumia mbinu za ajabu kupitisha mgombea. Kundi moja lilitoa rushwa na ikatangazwa wazi, na kundi lingine(lile linalopinga ufisadi) likakaa kimya. Even worse wapinzani nao wamekaa kimya as if ni halali. Tume yetu ya uchaguzi imeendelea kuwa ya kutia mashaka, tumesikia kuwa masanduku ya kura yamekamtwa yakiwa yamejaa kura zilizopigwa na iko kimya tu.
Inaonekana sasa kuwa wapinzani, are not as hopeless as we saw them in 1992, CCM will not win by default as was in 90's, sasa inabidi itumie nguvu zote ilizonazo kushinda uchaguzi. Mtaji wa CCM kushinda uchaguzi kiurahisi kama ilivyokuwa igunga, mbozi na kwingineko ambao Profesa Baregu alisema ni unyonge wa kiuchumi na kielimu walionao wapiga kura katika maeneo husika,a huenda una ukomo. Na matumzi ya vyombo vya dola kwenye uchaguzi inaonekana ni makubwa na makini zaidi kuliko katika kupambana na uhalifu unaotuliza kila siku, hii si dalili nzuri kwa watu tuliozoea kupiga kura tukisimamiwa na mgambo wenye marungu. Tumetoka mbali lakini tunakwenda mbali zaidi.
Hatua iliyofikia CCM sasa ya kutumia nguvu kubwa kushinda by election kwa lolote lile inatia shaka. Hali hii ikisambaa nchi nzima kuna uwezekano kukawa na hali ya ajabu nchini kwetu.