What about R&D?..The Case of Foreign Aid Influx & 'A Japanese Expert' Invite

Kwa kifupi, we have other priorities! Sisi bado tunaganga njaa na hivyo hilo unalolizungumzia halina nafasi kwetu. Badala ya kuwapeleka vijana wetu MIT ambako wale walio wakali watabaki huko ( MIT sio wajinga)na wale ambao watarudi tutashindwa kuwapa nyenzo, mishahara na mazingira ya kuwawezesha kufanya hizo R & D tuangalie kwanza basic needs zetu.

Turudi kwenye elimu ya msingi na sekondari, tuiboreshe ili watoto wetu wajifunze udadisi na sio kunukuu. Tupanue wigo la elimu hii nchi nzima ili kila mwenye nia ya kusoma apate nafasi hiyo. hawa ndio watakao'feed' vyuo vyetu vikuu na kuvifanya vitoe watu wenye calibre inayoendana na mahitaji ya dunia ya sasa. Hawa wakiwepo, mashirika binafsi yatawekeza kwenye R&D bila hata ya msaada wa serikali. India wamefanikiwa kutokana kuwa na idadi kubwa ya wasomi waliozalishwa na vyuo vyao vya IIT. Mashirika ya kigeni na yale ya kihindi yenye intenational presence ndiyo sasa yanavuna matunda hayo. Serikali ya kihindi ilishajaribu kubuni gari la gharama ndogo( mradi uliongozwa na mtoto mdogo wa marehemu Indira Gandhi, marehemu Sanjay Gandhi) waliloliita maruti na hawakufanikiwa mpaka waliponunua teknoloji kutoka Suzuki. Leo hii kampuni binafsi ya kihindi, Tata imefanikiwa kubuni gari la gharama ndogo duniani. Tusipoteze wakati kujaribu kuvumbua gurudumu kama tulivyofanya kwa miradi kama ya nyumbu bali tuwekeze kwenye kizazi cha kesho na bila shaka hizi R&D zitakuja. tatizo letu tunapenda sana njia za mkato. Hatuna subira.

Fundi Mchundo:

Naona mambo mengi hapa tulijadili katika mada ya Nuklia. Kwa mijadala ya siasa vitu vyote vinawezekana. Lakini miradi mingi ya kiserikali ni TEMBO MWEUPE (White Elephant).
 
Mzee Masanja!

I can not add more! Huwezi kufikiria ndoto to invest in R & D wakati institutions za kuzingatia haki na sheria are week and no accountability.. hiyo pesa italiwa tu!

Kwanza tuwe sheria zinaheshimiwa kwa wote..awe Waziri au mtu wa kawaida..kama kwa mfano Singapore!

Then ndo R & D... otherwise mbona tuna COSTECH, NIMR, TAFIRI, TPRI.. yet leo as a coutry we have achieved so little?

Tatizo Tz tunatamani sana kila kitu wakati mmoja.. finnaly we achieve so little!

Kwa maoni yangu na kwa hali ilivyo sasa sioni kama investment in R & D should not be a priority now!


Mkuu,

Hata kwenye simple life, bila self discipline huwezi kufanikiwa sembuse taifa?

Unafikria leo Dito angenyimwa mdhamana kama wengine waliofanya makosa kama yake walivyonyimwa..tungekuwa wapi? It would have changed trajectory ya jinsi wananchi tunavyojua na kutizama utawala wa sheria...katika nchi yetu.

Accountability na responsibility mengine yatafuata. We have had alot of studies and research in our country, na the so called donors wametoa millions and millions...zimeishia mifukoni mwa wajanja. kama watuhumiwa wangekuwa keko...aahhhh mbona leo tungekuwa level nyingine? But for now..its business as usual.

Mtu anaiba anahamishwa au anapelekwa kufichwa "ubalozini" na bado tunaongea maendeleo..we must be kidding!
 
Kwanza niwashukuru wachangiaji wote katika mada hii na mambo mengi nimejifunza na ninaamini kama watawala wetu wanapitia hapa kujifunza (siyo kuchunguza nani ni nani) wao pia yawezekana wamejifunza kitu au zaidi.

Maendeleo yana gharama
Mojawapo ya nyaraka muhimu sana ambazo tumewahi kuzipata katika Tanzania ni maandishi ya hotuba mbalimbali za Mwalimu ambayo yaliwekwa kwenye vitabu viwili "Uhuru na Maendeleo" na "Binadamu na Maendeleo". Ndani yake kuna elimu kubwa sana ya kuweza kujenga hoja juu ya dhana nzima ya maendeleo. Katika vitabu hivyo kama vichwa vyake vya habari visemavyo vimejenga hoja nyepesi; kwamba Uhuru wa mwanadamu unahusiana moja kwa moja na maendeleo yake - yaani mwanadamu asiye huru hajaendelea. La pili ambalo ni jambo ambalo naamini bado Mwalimu alikuwa mbali sana ni kuwa lengo la maendeleo yoyote yale ni mtu. Maendeleo yasiyo muendeleza mtu kumudu mazingira yake ni maendeleo ya vitu. Maendeleo ni lazima yalinde utu wa mtu.

Ndio maana utaona kuwa Marekani licha ya kuwa na nguvu kubwa ya kiuchumu haishikilii nafasi ya kwanza katika index ya Maendeleo ya Binadamu (Index of Human Development Report). Hivyo, ni lazima turudi kwenye misingi ya vilivyo muhimu katika maendeleo na hapa namba moja ni WATU.

Ubunifu, uvumbuzi, na ufundi ni kichocheo cha maendeleo
Katika kuleta maendeleo ya watu basi tunajikuta hatuna budi pia kuendeleza vitu; kwa sababu mtu na vitu kuna uhusiano wa moja moja tangu milenia na milenia. Ni pale mwanadamu alipoweza kuboresha kisu chake cha jiwe na kuanza kutumia cha chuma ndipo alivyoweza pia kuboresha maisha yake; ni pale alipoweza kubuni gurudumu (wheel) ndivyo mambo mengi ya mabadiliko ya viwanda yalipoanza kufanyika na zana nyingine nyingi kufuatia. Hivyo, mwanadamu anapoendeleza vitu kwa lengo la kuboresha na kurahisha maisha yake ndivyo anavyojikuta anaendelea.

Hata hivyo mara nyingi huko nyuma mambo mengi yalitokana na vipaji vya mtu na matokeo ya nasibu. Maendeleo ya sayansi hata hivyo yaliongoza kwenye dhana nzima ya kukaa na kufanya utafiti. Lengo la utafiti basi ni kugundua vitu na kuviboresha kwa kufuata kanuni za kisayansi na endapo jambo jingine la kinasibu linatokea basi linatokea kwa sababu ya juhudi hizo mahususi.

Ni kwa sababu hiyo, utaona kuwa nadharia za sumaku, kanuni za mwendo, na kanuni nyingine za sayansi zilibakia kuwa kanuni tu hadi pale zilipoanza kuwa applied katika maendeleo ya teknolojia. Hivyo haitoshi kujua sayansi au elimu ya darasani bila kuweka mkazo katika applied science.

Ni kwa misingi hiyo basi utafiti unahitajika kwa sababu hauwezi kutenganishwa na maendeleo. Tatizo letu naamini ni kuwa tunataka kuendelea lakini tunataka wengine ndiyo wafanye utafiti na kubuni vile vitakavyotuendeleza.

Nurujamii, hapo nyuma katoa mfano rahisi tu, kuhusu kwanini tunawatafuta wajapani kuja kutufanyia utafiti suala la msongamano wa magari Dar? Hivi hatuna wataalamu ambao wanaweza kuangalia data zile zile na kujaribu kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu na hata kubuni visivyokuwapo? Ni lazima tujenge uwezo wa kujiamini.

Wiki kadhaa kuna mtu alibandika hapa picha ya mtasha mmoja akitoa maelezo kwa watendaji wa kata fulani jinsi ya kukabiliana na tatizo la uchafu katika mazingira yetu; nilijihisi kichefu chefu!

Gharama ya kwanza ni watu
Hatuwezi kuendelea bila kulipa gharama ya kuendeleza watu watakaobeba jukumu la kusimamia utafiti na ubunifu nchini. Katika hili ni lazima tudhamirie kuendeleza rasilimali watu (human resources) na hapa nina maana ya kuendeleza the "best brains" in Tanzania.

Huwezi kuwa na mtafiti Chuo Kikuu ambaye anapokuwa maabara baadala ya kufikiria "panya wake wa maabara" anajiuliza kama maji yatapatikana nyumbani au kama piki piki yake inahitaji matengenezo. Ni lazima siyo tu kuwaenzi wanasayansi wetu lakini kuwatendea bora zaidi ili jambo kubwa na la pekee wao kuhangaika nalo kichwani liwe ni utatifi na utafiti tu. Hii ni gharama ambayo hadi hivi sasa hatuko tayari kuilipa.

Tuanze na kizazi kipya cha watafiti
Naamini kuwa miaka kadhaa iliyopita tumeenda kombo na tumechepukia pembeni. Tumetegemea watafiti toka nje na utafiti toka nje. Leo hii kutokana na teknolojia ya mawasiliano vijana wetu wanaweza kujikuta wana"kopy" na kupaste tafiti za watu wengine huku wakibadilisha majina ya mada na kuyafanya zionekane ni za kwao. Sijui kuna utaratibu gani wa kuangalia tatizo la plagiarism katika mambo ya utafiti nchini.

Nakumbuka jinsi tulivyokuwa tunapewa zile "project" na kwenda kuzifanyia utafiti na kuandika report bila ya kuwa na internet wala nini. Tulijifunza then kanuni mbalimbali za kisayansi za kufanya emperical analysis ya data. Leo hii unaingia kwenye google na kupata analysis waliofanya wengine!

Ni kwa sababu hiyo naamini ipo haja ya kurudi nyuma na kuanza kuteka mioyo ya vijana wetu na kuwachochea kwenye sayansi na utafiti. Tusipoteze mawazo ya vijana na kuwaacha wakimbie masomo ya sayanasi na wale walioko kwenye sayansi kujikuta kuwa "sayansi hailipi". Nakumbuka rafiki yangu mmoja alikuwa anapenda hesabu sana na alikuwa anazikokotoa kama mtu anavyo gigida maji; baada ya kwenda Chuo Kikuu badala ya kuendelea na hesabu alizokuwa anazipenda akaamua kuswitch na kwenda BCom kwa ajili ya ajira zaidi ingawa mwenyewe angependa kufanya utafiti wa mambo ya hesabu zaidi. Sijui ni wangapi ambao walijikuta wanaacha michepuo ya sayansi na kuingia sanaa.

Nitawapa mfano binafsi; nilipokuwa kidato cha nne nilikuwa nafundisha Fizikia ya kidato cha pili na nilifundisha (nikisaidiana na mwalimu wangu mkuu aliyekuwa mwalimu pekee wa physics) karibu term nzima. Nilikuwa napenda Physics lakini si kemia. Hata hivyo nilipoendelea na kidato cha tano na sita (licha kufaulu Fizikia na kufeli hesabu - don't ask me how)nilijikuta sina combination yenye akili na kuamua kuishia kufanya HGE na nilipoenda Chuo nikachukua masomo ambayo hayakaribiani na HGE!!

Sasa naamini kama kungekuwa na jinsi ya kuendelea na Physics nadhani ningeenda mbali zaidi; siku hizi nasoma mambo ya physics kama hobby tu nikiishia kutamani.

Je tuwapoteze vijana wetu namna hii? Naamini wakati umefika wa kuanzisha High Schools za sayansi tu na teknolojia ambazo zitakuwa ndiyo vitovu vya wanafunzi wanaoenda Vyuo Vikuu kusomea sayansi. Shule kama Iyunga, Ilboru, Usagara, Bwiru, Mzumbe, n.k zinaweza kugeuzwa na kuwa shule za Sayansi na Teknolojia (siyo za wenye vipaji tu).

Shule hizo siyo tu zibadilishwe kuwa za sayansi lakini ziwezeshwe kufanya sayansi na utafiti na kuchochea wanafunzi wao kuwa wabunifu wakichezea maabara usiku kucha na mchana kutwa. Wakitoka hapo wanaenda kwenye Vyuo Vikuu vya Sayansi na Teknolojia kama MIT, DIT AIT, na Tanga Tech etc. Wale wanaobobea kutoka vyuo hivyo ndiyo wanapewa ofa ya kungia katika National Labs na ofa yenyewe lazima iwafanya wajisikie wanathaminiwa. Hii ni gharama ambayo lazima tuilipe kwa sababu tunaweza.

Hakuna njia ya mkato ya maendeleo endelevu
Tunaweza kutumia njia ya mkato ya kuendeleza vitu tu; lakini kama tunataka maendeleo ya kweli hatuna budi kuendeleza watu wetu. Leo hii hizi milioni 700 tukazotumia kujenga barabaraba na miundo mbinu zinaonekana zina lengo zuri. Lakini endapo tukio la kimungu au la kiasili likitupiga na kuharibu barabara na miundo mbinu hiyo ni nini tulicho nacho cha kushikilia? Itabidi tuombe tena misaada ya kujenga tena barabara hizo.

Leo hii barabara zinazotengenezwa hapo Dar na sehemu nyingine zikiharibika tunatafuta tenda tena za wataalamu toka nje waje watutengenezee. Tusipoweza kuendeleza watu wetu tutaendelea kuwa na maendeleo tegemezi; yaani yale yanayotegemea misaada na utaalamu toka nje.

Naomba niishie hapa kwa sasa..
 
I believe it is research and development that are the catalyst for economic development and prosperity of a modern nation.

How much of our Science and Technology budget annuarly is set aside for R&D in the country?

Mwanakijiji, tuna safari ndefu sana ya kufika tuendako, unless kama kutakuwa na political will ya dhati, then only mambo yatakwenda mbele.

Kwa sasa hivi wala sijui kama tunayo Sera ya R&D na wala sijui ni nani anayeratibu.

Pengine ni wakati muafaka sasa kupitia Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Technolojia kuanza kuleta hoja kama hizi. Tumekuwa na COSTECH ambayo mpaka sasa sina uhakika achievement zake kubwa ni zipi zaidi ya kufanya mambo ya ICT (anayejua anaweza kunifahamisha)
 
Nyie mtalonga weeeee lakini mwisho wa siku itakuwa ni jinsi sisi tulivyo, mwisho wa hadithi!!!! Anayetaka kuamini aamini na asiyetaka afanye hivyo lakini hata iweje ukweli haubadiliki.
 
Kwanza niwashukuru wachangiaji wote katika mada hii na mambo mengi nimejifunza na ninaamini kama watawala wetu wanapitia hapa kujifunza (siyo kuchunguza nani ni nani) wao pia yawezekana wamejifunza kitu au zaidi.

Maendeleo yana gharama
Mojawapo ya nyaraka muhimu sana ambazo tumewahi kuzipata katika Tanzania ni maandishi ya hotuba mbalimbali za Mwalimu ambayo yaliwekwa kwenye vitabu viwili "Uhuru na Maendeleo" na "Binadamu na Maendeleo". Ndani yake kuna elimu kubwa sana ya kuweza kujenga hoja juu ya dhana nzima ya maendeleo. Katika vitabu hivyo kama vichwa vyake vya habari visemavyo vimejenga hoja nyepesi; kwamba Uhuru wa mwanadamu unahusiana moja kwa moja na maendeleo yake - yaani mwanadamu asiye huru hajaendelea. La pili ambalo ni jambo ambalo naamini bado Mwalimu alikuwa mbali sana ni kuwa lengo la maendeleo yoyote yale ni mtu. Maendeleo yasiyo muendeleza mtu kumudu mazingira yake ni maendeleo ya vitu. Maendeleo ni lazima yalinde utu wa mtu.

Ndio maana utaona kuwa Marekani licha ya kuwa na nguvu kubwa ya kiuchumu haishikilii nafasi ya kwanza katika index ya Maendeleo ya Binadamu (Index of Human Development Report). Hivyo, ni lazima turudi kwenye misingi ya vilivyo muhimu katika maendeleo na hapa namba moja ni WATU.

Ubunifu, uvumbuzi, na ufundi ni kichocheo cha maendeleo
Katika kuleta maendeleo ya watu basi tunajikuta hatuna budi pia kuendeleza vitu; kwa sababu mtu na vitu kuna uhusiano wa moja moja tangu milenia na milenia. Ni pale mwanadamu alipoweza kuboresha kisu chake cha jiwe na kuanza kutumia cha chuma ndipo alivyoweza pia kuboresha maisha yake; ni pale alipoweza kubuni gurudumu (wheel) ndivyo mambo mengi ya mabadiliko ya viwanda yalipoanza kufanyika na zana nyingine nyingi kufuatia. Hivyo, mwanadamu anapoendeleza vitu kwa lengo la kuboresha na kurahisha maisha yake ndivyo anavyojikuta anaendelea.

Hata hivyo mara nyingi huko nyuma mambo mengi yalitokana na vipaji vya mtu na matokeo ya nasibu. Maendeleo ya sayansi hata hivyo yaliongoza kwenye dhana nzima ya kukaa na kufanya utafiti. Lengo la utafiti basi ni kugundua vitu na kuviboresha kwa kufuata kanuni za kisayansi na endapo jambo jingine la kinasibu linatokea basi linatokea kwa sababu ya juhudi hizo mahususi.

Ni kwa sababu hiyo, utaona kuwa nadharia za sumaku, kanuni za mwendo, na kanuni nyingine za sayansi zilibakia kuwa kanuni tu hadi pale zilipoanza kuwa applied katika maendeleo ya teknolojia. Hivyo haitoshi kujua sayansi au elimu ya darasani bila kuweka mkazo katika applied science.

Ni kwa misingi hiyo basi utafiti unahitajika kwa sababu hauwezi kutenganishwa na maendeleo. Tatizo letu naamini ni kuwa tunataka kuendelea lakini tunataka wengine ndiyo wafanye utafiti na kubuni vile vitakavyotuendeleza.

Nurujamii, hapo nyuma katoa mfano rahisi tu, kuhusu kwanini tunawatafuta wajapani kuja kutufanyia utafiti suala la msongamano wa magari Dar? Hivi hatuna wataalamu ambao wanaweza kuangalia data zile zile na kujaribu kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu na hata kubuni visivyokuwapo? Ni lazima tujenge uwezo wa kujiamini.

Wiki kadhaa kuna mtu alibandika hapa picha ya mtasha mmoja akitoa maelezo kwa watendaji wa kata fulani jinsi ya kukabiliana na tatizo la uchafu katika mazingira yetu; nilijihisi kichefu chefu!

Gharama ya kwanza ni watu
Hatuwezi kuendelea bila kulipa gharama ya kuendeleza watu watakaobeba jukumu la kusimamia utafiti na ubunifu nchini. Katika hili ni lazima tudhamirie kuendeleza rasilimali watu (human resources) na hapa nina maana ya kuendeleza the "best brains" in Tanzania.

Huwezi kuwa na mtafiti Chuo Kikuu ambaye anapokuwa maabara baadala ya kufikiria "panya wake wa maabara" anajiuliza kama maji yatapatikana nyumbani au kama piki piki yake inahitaji matengenezo. Ni lazima siyo tu kuwaenzi wanasayansi wetu lakini kuwatendea bora zaidi ili jambo kubwa na la pekee wao kuhangaika nalo kichwani liwe ni utatifi na utafiti tu. Hii ni gharama ambayo hadi hivi sasa hatuko tayari kuilipa.

Tuanze na kizazi kipya cha watafiti
Naamini kuwa miaka kadhaa iliyopita tumeenda kombo na tumechepukia pembeni. Tumetegemea watafiti toka nje na utafiti toka nje. Leo hii kutokana na teknolojia ya mawasiliano vijana wetu wanaweza kujikuta wana"kopy" na kupaste tafiti za watu wengine huku wakibadilisha majina ya mada na kuyafanya zionekane ni za kwao. Sijui kuna utaratibu gani wa kuangalia tatizo la plagiarism katika mambo ya utafiti nchini.

Nakumbuka jinsi tulivyokuwa tunapewa zile "project" na kwenda kuzifanyia utafiti na kuandika report bila ya kuwa na internet wala nini. Tulijifunza then kanuni mbalimbali za kisayansi za kufanya emperical analysis ya data. Leo hii unaingia kwenye google na kupata analysis waliofanya wengine!

Ni kwa sababu hiyo naamini ipo haja ya kurudi nyuma na kuanza kuteka mioyo ya vijana wetu na kuwachochea kwenye sayansi na utafiti. Tusipoteze mawazo ya vijana na kuwaacha wakimbie masomo ya sayanasi na wale walioko kwenye sayansi kujikuta kuwa "sayansi hailipi". Nakumbuka rafiki yangu mmoja alikuwa anapenda hesabu sana na alikuwa anazikokotoa kama mtu anavyo gigida maji; baada ya kwenda Chuo Kikuu badala ya kuendelea na hesabu alizokuwa anazipenda akaamua kuswitch na kwenda BCom kwa ajili ya ajira zaidi ingawa mwenyewe angependa kufanya utafiti wa mambo ya hesabu zaidi. Sijui ni wangapi ambao walijikuta wanaacha michepuo ya sayansi na kuingia sanaa.

Nitawapa mfano binafsi; nilipokuwa kidato cha nne nilikuwa nafundisha Fizikia ya kidato cha pili na nilifundisha (nikisaidiana na mwalimu wangu mkuu aliyekuwa mwalimu pekee wa physics) karibu term nzima. Nilikuwa napenda Physics lakini si kemia. Hata hivyo nilipoendelea na kidato cha tano na sita (licha kufaulu Fizikia na kufeli hesabu - don't ask me how)nilijikuta sina combination yenye akili na kuamua kuishia kufanya HGE na nilipoenda Chuo nikachukua masomo ambayo hayakaribiani na HGE!!

Sasa naamini kama kungekuwa na jinsi ya kuendelea na Physics nadhani ningeenda mbali zaidi; siku hizi nasoma mambo ya physics kama hobby tu nikiishia kutamani.

Je tuwapoteze vijana wetu namna hii? Naamini wakati umefika wa kuanzisha High Schools za sayansi tu na teknolojia ambazo zitakuwa ndiyo vitovu vya wanafunzi wanaoenda Vyuo Vikuu kusomea sayansi. Shule kama Iyunga, Ilboru, Usagara, Bwiru, Mzumbe, n.k zinaweza kugeuzwa na kuwa shule za Sayansi na Teknolojia (siyo za wenye vipaji tu).

Shule hizo siyo tu zibadilishwe kuwa za sayansi lakini ziwezeshwe kufanya sayansi na utafiti na kuchochea wanafunzi wao kuwa wabunifu wakichezea maabara usiku kucha na mchana kutwa. Wakitoka hapo wanaenda kwenye Vyuo Vikuu vya Sayansi na Teknolojia kama MIT, DIT AIT, na Tanga Tech etc. Wale wanaobobea kutoka vyuo hivyo ndiyo wanapewa ofa ya kungia katika National Labs na ofa yenyewe lazima iwafanya wajisikie wanathaminiwa. Hii ni gharama ambayo lazima tuilipe kwa sababu tunaweza.

Hakuna njia ya mkato ya maendeleo endelevu
Tunaweza kutumia njia ya mkato ya kuendeleza vitu tu; lakini kama tunataka maendeleo ya kweli hatuna budi kuendeleza watu wetu. Leo hii hizi milioni 700 tukazotumia kujenga barabaraba na miundo mbinu zinaonekana zina lengo zuri. Lakini endapo tukio la kimungu au la kiasili likitupiga na kuharibu barabara na miundo mbinu hiyo ni nini tulicho nacho cha kushikilia? Itabidi tuombe tena misaada ya kujenga tena barabara hizo.

Leo hii barabara zinazotengenezwa hapo Dar na sehemu nyingine zikiharibika tunatafuta tenda tena za wataalamu toka nje waje watutengenezee. Tusipoweza kuendeleza watu wetu tutaendelea kuwa na maendeleo tegemezi; yaani yale yanayotegemea misaada na utaalamu toka nje.

Naomba niishie hapa kwa sasa..

Mwanakijiji hii ni kweli tupu!

Lakini umeshajiuliza kwa nini watu wenye wajibu wa kuyatekeleza haya hawafanyi hivyo? ingawa wanapata mishahara na marupurupu kibao (hapa naongea wakurugenzi na mawaziri nk). Tunarudi kule kule uwajibikaji!

Mfano serikali inatenga pesa kwa ajiri ya kuimarisha ujenzi wa taasisi flani ya utafiti (mfano muhimbili) uliza ni kiasi gani kinaliwa na wajanja na how much goes into the project? and then ask what is done to the culprits? Kifupi hata kama ungepewa billions and billions bila uwezekano kwa waliokabiziwa hizo pesa "kuleta mahesabu jioni" you will achieve nothing!

Hizo taasisi, shule utatenga pesa, lakini afisa elimu atakula 15%, Mkurugenzi 10%, Katibu mkuu na waziri @0% how much is remaining? sijui hesabu.

Hivi umeshawahi kujiuliza what normally happens kwenye ile report ya KILA MWAKA ya Auditor General? Kila mwaka billions zinapotea...umeshawahi kuona mtu anapandishwa kizimbani? halmashauri wanaiba pesa kibao hata Pinda analijua..lakini watu wanahamishwa/wanakuwa promoted...on and on.....

As I said hata binadamu kufanikiwa unahitaji uwe na discipline na miiko on what you can do and not!

Nachoka
 
lakini mbona hamuulizi private sector nayo inachangia ngapi katika hizo research? jibu ni zero,nchi nyingi percentage kubwa ya hizo fund zinatoka private sector,industry nyingi zina namna ya kufanya research zake bila kutegemea serikali kwa sababu is a big business na faida kubwa,angalia pharmaceutical or Energy industry nasikia wanatumia billions bila msaada wa serikali ili kupata kitu safi with maximum profit,kwa TZ naweza kusema hakuna serious industry kwa hiyo kuwa na research bila sector yenyewe naona kama ni ngumu sana
 
Masanja asante sana, na nitajaribu kuingilia hilo la maendeleo ni uwajibikaji.. natumia mawazo yenu hapa ili kuweza kujenga hoja yenye nguvu na kuweza kuchapwa kwenye gazeti..
 
lakini mbona hamuulizi private sector nayo inachangia ngapi katika hizo research? jibu ni zero,nchi nyingi percentage kubwa ya hizo fund zinatoka private sector,industry nyingi zina namna ya kufanya research zake bila kutegemea serikali kwa sababu is a big business na faida kubwa,angalia pharmaceutical or Energy industry nasikia wanatumia billions bila msaada wa serikali ili kupata kitu safi with maximum profit,kwa TZ naweza kusema hakuna serious industry kwa hiyo kuwa na research bila sector yenyewe naona kama ni ngumu sana

Koba umezua point nzito sana; je sekta inaendelezwa kwanza au research ndiyo inasababisha kuendelea kwa sekta fulani. Natumaini hili si swali la yai na kuku kilitangulia kipi..
 
Kuendeleza mada tu. Wakati Kikwete akiwa Washington DC nilitaka kumuuliza swali moja, lakini sikupata nafasi kwa sababu waulizaji walikuwa wengi.

JK akiwa waziri wa mambo ya nje alipendekeza kuanzishwa kwa mpango wa Marshal Plan wa kuzisaidia nchi za Afrika kutokana na madeni. Baada ya vita vya pili vya dunia Marshal Plan ilitumika kusaidia nchi za Ulaya Magharibi kunyanyua uchumi wao.

Nikiwa Sweden kuchuma matunda nilifanya kazi kwa jamaa mmoja ambaye alifaidika na mpango wa Marshal Plan. Katika mpango huo yeye alichukuliwa na kufanya kazi kwenye mashambani nchini Marekani na kujifunza matumizi ya zana, uongozi wa kilimo na mambo mengine. Huyu jamaa hakupelekwa MIT au chuo chochote, alikwenda moja kwa moja shambani na kujifunza na alikuwa ni mkulima mzuri aliporudi kwao.

Swali nililotaka kumuuliza JK, ni kwanini juhudi hazifanyiki kuhamisha teknologia? Tumekazania Marshal Plan ya pesa lakini hatuangalii sehemu nyingine za Marshal plan. Kwa mfano nchi za Scandinavia zinatoa misaada mingi ya kipesa, lakini ingekuwa jambo la maana kuwapeleka watanzania na kufanya kazi mashambani na kujifunza skills za uendeshaji wa mashamba na utumiaji wa technolojia.
 
Bin Maryam.. swali zuri nadhani katika hili la R & D kuna mengi ambayo lazima tuyaangalia mojawapo kama msemaji mwingine alivyosema ni kuhamisha teknolojia (technology transfer). Ni jinsi gani tunaweza kuchota technolojia ya nje na kuileta ndani badala ya wao kuja na kutumia teknolojia yao na kuondoka nayo? Nadhani umejaribu kujibu sehemu ya swali hilo.. thanks
 
Jamani eeeh...mimi kila mara nauliza hapa ni nani alizisaidia nchi za Ulaya na Marekani kuwa na maendeleo kama waliyonayo? Ni nini/ nani alileta mageuzi ya viwanda kule Uingereza na kwingineko ulaya? Nani aliwaletea haya mageuzi?

Mbona yalitokea ulaya tu au ulaya iliumbwa kwanza na Mungu halafu baadae ndio ikaja ikaumbwa Afrika?
 
Koba umezua point nzito sana; je sekta inaendelezwa kwanza au research ndiyo inasababisha kuendelea kwa sekta fulani. Natumaini hili si swali la yai na kuku kilitangulia kipi..

...technically its both,lakini to jump start any sector you need more of feasibility study than research,lakini kwenda mbele zaidi ndio research inaingia na inakuwa muhimu zaidi,to me lazima sekta iwepo kwanza kabla ya research.
 
Bin Maryam.. swali zuri nadhani katika hili la R & D kuna mengi ambayo lazima tuyaangalia mojawapo kama msemaji mwingine alivyosema ni kuhamisha teknolojia (technology transfer). Ni jinsi gani tunaweza kuchota technolojia ya nje na kuileta ndani badala ya wao kuja na kutumia teknolojia yao na kuondoka nayo? Nadhani umejaribu kujibu sehemu ya swali hilo.. thanks

Karibu Mwanakijiji:

Vilevile katika posti moja ulitaja watu kwenda MIT. Naona hiyo ikatustua watu kwa kufikiri kuwa R & D inahusiana na HIGH TECH.

Morogoro kulikuwa na kiwanda cha mbegu. Na tuliokuwa na mashamba ya mahindi tulinunua mbegu kutoka hapo ambazo zilifanyiwa kazi na wataalamu wetu na misaada ya kutoka nje.

Kwa mfano mahindi yalikuwa yanachukua miezi mitano lakini jamaa walikuja na mbegu ya miezi mitatu. Na mbegu hii tulikuwa tunaita STAR iliondoa njaa kwa kiasi fulani.

SUA inasomesha mambo ya nutrition science lakini wataalamu wanakwenda kuwa maafisa mikopo. Tanzania ina tatizo kubwa ya kusindika chakula. Na huwezi kuondoa njaa bila kuwa na chakula cha kusindika. Hivyo kama kuna R & D basi zilenge kwenye midomo kwanza.
 
Bin Maryam umenikumbusha mbali; Pale Uyole walikuwa wanafanya kila aina ya utafiti na mojawapo nakumbuka vizuri ilikuwa ni ya mbegu za maharage na hata zile za mahindi mafupi; Unapokuwa na Chuo Kikuu cha Kilimo, taasisi zisizohesabika za utafiti wa kilimo; kwenye nchi yenye maji mengi, udongo wenye rotuba na mamilioni ya watu wasio na kazi; halatu kila baada ya miaka kumi hivi unapata njaa.. basi kuna tatizo mahali!
 
Bin Maryam umenikumbusha mbali; Pale Uyole walikuwa wanafanya kila aina ya utafiti na mojawapo nakumbuka vizuri ilikuwa ni ya mbegu za maharage na hata zile za mahindi mafupi; Unapokuwa na Chuo Kikuu cha Kilimo, taasisi zisizohesabika za utafiti wa kilimo; kwenye nchi yenye maji mengi, udongo wenye rotuba na mamilioni ya watu wasio na kazi; halatu kila baada ya miaka kumi hivi unapata njaa.. basi kuna tatizo mahali!

Tatizo: Ndivyo Tulivyo!!
 
Tatizo: Ndivyo Tulivyo!!

unajua najaribu kukwepa ukweli huo sana lakini bado unaniandama sehemu fulani kwenye ubongo wangu.. sasa kama ndivyo tulivyo tunaweza kubadilika au ndio tukubali kuingia mikataba na Mataifa makubwa waje kututawala tena... ?
 
unajua najaribu kukwepa ukweli huo sana lakini bado unaniandama sehemu fulani kwenye ubongo wangu.. sasa kama ndivyo tulivyo tunaweza kubadilika au ndio tukubali kuingia mikataba na Mataifa makubwa waje kututawala tena... ?

Mzee unajua ukweli ni kitu kigumu sana kukwepa. Mimi hadi nione mabadiliko ya kweli ndio nitaamini kwamba sivyo tulivyo. Kuhusu kubadilika hilo sijui kama tunaweza kwa sababu ingekuwa rahisi kufanya hivyo tungekuwa tumeshabadilika kwa sababu tunajua kabisa kwamba hali zetu ni mbaya na tunataka mabadiliko/ maendeleo lakini hakuna cha maana tunachokifanya kuleta hayo mabadiliko/ maendeleo....sasa tatizo liko wapi?
 
Bin Maryam umenikumbusha mbali; Pale Uyole walikuwa wanafanya kila aina ya utafiti na mojawapo nakumbuka vizuri ilikuwa ni ya mbegu za maharage na hata zile za mahindi mafupi; Unapokuwa na Chuo Kikuu cha Kilimo, taasisi zisizohesabika za utafiti wa kilimo; kwenye nchi yenye maji mengi, udongo wenye rotuba na mamilioni ya watu wasio na kazi; halatu kila baada ya miaka kumi hivi unapata njaa.. basi kuna tatizo mahali!


Nilipinga mawazo yako pale ulipotaja R &D ya kupeleka watu MIT, re-engineering open source na mambo ya IT. Picha niliyopata ni R & D ya kupata Mobile Phone na high tech gadgets.

Lakini tukirudi katika mambo ya chakula, kuna ulazima wa kuwa na vituo vya utafiti wa nguvu kwa sababu mbili muhimu. Kwanza ni lazima tujitosheleze kwa chakula. Na pili ni lazima tuongeze uzalishaji na kupunguza gharama za uzalishaji huo.

Kwa mfano zile biskuti ngumu wanazotumia Askari wakiwa vitani ni kazi ya R & D. Walifanya utafiti na kuona kwamba Askari anaitaji chakula gani na chenye nutrition ya aina gani na kitakachomfanya asiende choo mara kwa mara.

Kuna vijana wengi wanakwenda shule wakiwa na njaa na shule zisizo na sehemu ya kujisaidia. Pata picha ya kijana wa anayekwenda shuleni na biskuti zake kama askari wa kimarekani aliye vitani. Au mkulima yupo shamba badala ya kusonga ugali anapata biskuti za kijeshi.
 
Jamani eeeh...mimi kila mara nauliza hapa ni nani alizisaidia nchi za Ulaya na Marekani kuwa na maendeleo kama waliyonayo? Ni nini/ nani alileta mageuzi ya viwanda kule Uingereza na kwingineko ulaya? Nani aliwaletea haya mageuzi?

Mbona yalitokea ulaya tu au ulaya iliumbwa kwanza na Mungu halafu baadae ndio ikaja ikaumbwa Afrika?

Aisee, Nyani:
Yaani unataka nasi tukaanzie huko? Unajua iliwachukua miaka mingapi kufikia hapo walipo?

Sisi tuna faida ya ku-'leapfrog,' pamoja na kwamba nasi pia hatuwezi kukwepa 'process' itakayotupeleka katika maendeleo hayo (kwa muda mfupi kuliko waingereza); kwani hatuna haja tena ya kwenda kuvumbua gurudumu.

Pamoja na kwamba njia yetu itakuwa ni fupi, lakini hatuwezi kuyakwepa maandalizi mhimu yanayotakiwa kutupeleka kwenye hayo maendeleo. Ni haya maandalizi ndiyo yanayotusumbua sasa hivi.

Yaani kuwa na shule za kutosha na nzuri ili wataalam wawepo.
Pawe na miundombinu, barabara nzuri kupitisha pembejeo kwa mkulima.
Afya - watoto wasiishie kufa hata kabla ya kufikisha miaka mitano.
Viwanda mhimu - kuyaongezea mazao yetu thamani kabla ya kuyauza nje kwa bei nzuri.

Mifano ya wenzetu tumeiona: Korea ya Kusini, Malaysia, Indonesia, Turkey, Morocco, Tunisia - nchi zote hizi hawakuwa mbali sana na sisi kimaendeleo miaka michache iliyopita?

Mimi ninasema: Tunaweza, tuendelee vizuri na kuchapa kazi; mradi tu mafisadi wasiturudishe nyuma zaidi.
 
Back
Top Bottom