Wezi wa Tanesco ni Sengerema Engineering Goup Ltd

DALA

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
2,212
4,515
Salaam kwa wote,

Mimi ninamiliki biashara ya car wash maeneo ya Mabibo kwenye barabara ya kuelekea Loyola opposite na Jambo Garden.

Nilikamilisha taratobu za kuomba huduma za Za umeme na kufanikiwa kulipa kiasi cha 1,175, 500/= kama gharama za kuunganishiwa umeme 06/02/2012. Mpaka leo, sijaletewa umeme zaidi ya nguzo waliouleta karibia miezi miwili iliyopita.

Leo mida ya saa tano na nusu nilipigiwa simu na kijana wangu akinitaarifu kwamba kuna watu kutoka Tanesco wamekuja kung'oa nguzo ikabidi niongee nao kwenye simu, jamaa wakaniambia kwamba wanalazimika kung'oa nguzo kwasababu watu wanalalamika eti serikali haikuwalipa fidia nilipomuuliza maswali mawili matatu nikaona anashindwa kunipa majibu yakuridhisha ikabidi niende kuongeanao ana kwa ana.

Nilishangaa kukuta gari aina ya Canter yenye namba T845 ASH inayomilikiwa na kampuni ya Sengerema Engeneering Group Ltd.

Tulibishana matokeo yake walishindwa kung'oa nguzo baada ya kuishiwa hoja ikabidi niende Tanesco Magomeni kufuatilia.

Nilichoambiwa ni kwamba hawa ni independent contractors wa Tanesco ila kuna wakati wanaiba vifaa kama hivyo kwa matumizi yao ya kampuni. Mapokeo ya Tanesco kwa kiasi yamenionyesha picha kwamba watumishi wa Tanesco wanalielewa hili ila ninashangaa hawachukui hatua stahiki kuondokana na watu kama hawa katka uchumi wetu.

Tunakokwenda mbali kweli. Ngoja tuone!
 
Pole sana, kwahiyo kama ni kampuni ya ya watu binafsi nani aliaambia waziweke awali hizo nguzo ni Tanesco au waliamua kuziweka wao? Hapo kunatatizo.
 
Hawa kwa kifupi ni wezi hawakuweka nguzo! Wanapita kuiba nguzo kutoka pale ambapo Tanesco wameweka bila kukamilisha kwa kufunga nyaya na mita! Actually walipoona kwamba nimewakalia vibaya ilibidi waondoke!
 
Hii kampuni naijua huwa inafanya kazi za TANESCO. Sijui kama deal hizi huwa hazina mawaa. Hii ikimfikia Prof. Muhongo basi ata deal nao.
 
Sengerema Engeneering Goup Ltd - Sounds like kampuni ya Ngeleja mbunge wa Sengerema
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Dala, hadi leo kwa nini hujapta umeme? Waziri alitoa press release kuwa wale wote waliolipia wanatakiwa wawe wamepata umeme ifikapo 30 Juni. Kama Tanesco wameshindwa kukupa umeme unatakiwa kutoa taarifa Wizarani. Alitoa na namba za simu.
Nenda Wizarani na risiti zako Mkuu na umwone muhisika.
 
Sengerema ni jimbo la aliekuwa waziri wa zamanai wa nishati na madini ndugu Ngeleja aka Megawat, so its sound ni kama kampuni yake ndo maana its untouchable
 
Dala, hadi leo kwa nini hujapta umeme? Waziri alitoa press release kuwa wale wote waliolipia wanatakiwa wawe wamepata umeme ifikapo 30 Juni. Kama Tanesco wameshindwa kukupa umeme unatakiwa kutoa taarifa Wizarani. Alitoa na namba za simu.
Nenda Wizarani na risiti zako Mkuu na umwone muhisika.

Naomba hizo number alizotoa Waziri Muhongo huku kuna watu wengi tu wamelipia lakini hawajafungiwa umeme, TANESCO wanadai hawana nguzo.
 
Una akili sana wewe, inaelekea aliipigia debe ili ishinde zabuni ya mabilioni pale TANESCO.

BAK nimejaribu tu kuunganisha some dots. Maana Ngeleja ambaye ni mbunge wa Sengerema alikuwa waziri wa nishatii na madini na TANESCO ilikuwa chini yake. Na kwa kuwa walishaona rais ni dhaifu basi jamaa wanaunda tu vikampuni na kujipatia tenda za kuiba pesa za walipa kodi kama watakavyo. Too bad.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Salaam kwa wote,
.....
Nilikamilisha taratobu za kuomba huduma za Za umeme na kufanikiwa kulipa kiasi cha 1,175, 500/= kama gharama za kuunganishiwa umeme 06/02/2012. Mpaka leo, sijaletewa umeme zaidi ya nguzo waliouleta karibia miezi miwili iliyopita.................

Hii bei ya 1,175,500 ni malipo ya umeme wa haina gani? Ebu fuatilia, utakuwa umeingizwa mjini.
 
Sidhani kama ni kampuni ya ngeleja,MKurugenzi mkuu wa kampuni hii anaitwa Joseph Masindi yupo pale ubungo NSSF building ndio ofisi yao.Sijui sana kuhusu utendaji wao wa kazi,ila kama ni kweli basi duh sitajaribu kuwatumia nikipata tenda
 
Ibra, nimepiga maktime mpaka nimechoka! Kama nchi inahujumiwa hivi unategemea nini? Tanesco hawaishiwi mistari, suluhisho ni kuweka serikali itakayokuwa na sauti kwa taasisi zake otherwise hapa hakuna kitu! The system is too corrupt to bring us development we want!
 
Salaam kwa wote,

Mimi ninamiliki biashara ya car wash maeneo ya Mabibo kwenye barabara ya kuelekea Loyola opposite na Jambo Garden.

Nilikamilisha taratobu za kuomba huduma za Za umeme na kufanikiwa kulipa kiasi cha 1,175, 500/= kama gharama za kuunganishiwa umeme 06/02/2012. Mpaka leo, sijaletewa umeme zaidi ya nguzo waliouleta karibia miezi miwili iliyopita.

Leo mida ya saa tano na nusu nilipigiwa simu na kijana wangu akinitaarifu kwamba kuna watu kutoka Tanesco wamekuja kung'oa nguzo ikabidi niongee nao kwenye simu, jamaa wakaniambia kwamba wanalazimika kung'oa nguzo kwasababu watu wanalalamika eti serikali haikuwalipa fidia nilipomuuliza maswali mawili matatu nikaona anashindwa kunipa majibu yakuridhisha ikabidi niende kuongeanao ana kwa ana.

Nilishangaa kukuta gari aina ya Canter yenye namba T845 ASH inayomilikiwa na kampuni ya Sengerema Engeneering Group Ltd.

Tulibishana matokeo yake walishindwa kung'oa nguzo baada ya kuishiwa hoja ikabidi niende Tanesco Magomeni kufuatilia.

Nilichoambiwa ni kwamba hawa ni independent contractors wa Tanesco ila kuna wakati wanaiba vifaa kama hivyo kwa matumizi yao ya kampuni. Mapokeo ya Tanesco kwa kiasi yamenionyesha picha kwamba watumishi wa Tanesco wanalielewa hili ila ninashangaa hawachukui hatua stahiki kuondokana na watu kama hawa katka uchumi wetu.

Tunakokwenda mbali kweli. Ngoja tuone!

Hili bandiko lilinipa shida kubwa na nilitishiwa maisha.

Kosa nililofanya ni kuweka wazi taarifa muhimu kwenye bandiko hili hivyo ikawa rahisi kunitambua nje ya jukwaa.

Ni kwamba wakati ninaweka bandiko nilikuwa kwenye mchakato wa kusafiri. Niliporudi toka safarini nilikuta barua pale ofisini kwa vijana wangu. Barua ilikuwa na ujumbe wa kunitaka niombe radhi au nipelekwe mahakamani.

Mimi kwa kuwa nilikuwa na ushahidi wa picha nikaenda Tanesco Kinondoni kwa meneja kuwasilisha taarifa.

Cha ajabu nafika kule nakuta meneja kabadilisha kauli maana kabla ya kusafiri nilimpelekea taarifa. Ilibidi niwajibike kwani wale wajinga walishanijua na wakawa na ushirikiano na Tanesco ambaye meneja wake wa kanda aliniruka. Kumbe wanakula na Tanesco mimi sikuwa na taarifa.

Niliona isiwe shida, nikaomba msamaha ili kuepusha vurugu. Ila bandiko kama nilivyoiweka mwanzo ni tukio la ukweli. Namna walivyokuwa wanahujumu miundombinu za Tanesco
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom