Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
Jambo mojawapo lililotokea kwa mwanadamu dhambi ilipoingia ni kuishi maisha ya umaskini na kupungukiwa. Dhambi pia iliweka matabaka ya matajiri na maskini. Toka mwanzo na hata sasa na siku zote Mungu hapendi watu wake wawe maskini (kwa jinsi ya mwili) Katika 2 Wakorintho 8:9 tunasoma ya kuwa: Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake Kwa hiyo ni mapenzi ya Mungu tuwe matajiri. Njia ambayo Mungu anatumia kutuwezesha tuwe matajiri ni kwa kutupa nguvu zake. Kwa maana imeandikwa katika kitabu cha Kumbukumbu ya Torati 8:18 ya kuwa: Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri, ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo Tunasoma hapa ya kuwa tunaweza kuomba tupate msaada wa nguvu za Mungu ili tupate utajiri halali ndani ya Kristo.