google helper
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 9,629
- 13,691
Ukiweza kulijibu hilo swali maisha yako yatabadilika sana utajifaham ww ni nani, unatakiwa uweje, uvae nn, uishi vipi , hutoiga iga vitu wala kuona mtu mwingine amepewa na ww huna nk
Kwanini unahisi swali ni gumu na si kwamba swali halieleweki?Swali gumu sijapata ona, àsilimia 99.9 ya watu hawajijui wao ni akina nani
Kweli mkuu, nimeipitia jana hii kitu, Apollo alitisha sana katika kuelezea hiliNakumbuka lilishawahi kujadiliwa huku, ila hakuna aliyeleta majawabu yaliyokamilika!
Umeshawahi kujiuliza wewe ni nani?
cc Apollo
Mimi ni mimi duniani kote, mimi mwenye mawazo ya aina yangu, hakuna mwingine kama mimi, mimi ni mimi nilievaa mwili na siku mwili wangu ukichoka nitatoka na kwenda zangu, na siku nikipenda nitarudi mimi ni mimi wa ndani yangu.Wewe ni nani?
Ni swali ambalo ukiulizwa unaweza kuliona rahisi sana na kulijibu haraka haraka kwa kutoa jibu linalotaja jina lako. Mimi ni James, ama nimi ni Janeth. Lakini ni ukweli ulio wazi kua wewe si jina lako. Wewe ni zaidi ya jina lako.
Ama unaweza kujibu kwa kutaja kazi yako, wewe ni nani? Ukajibu, mimi ni Mkurugenzi wa Masoko wa CRDB, mwingine atasema mimi ni Mbunge au mimi ni Waziri, ama mimi ni Mwalimu. Lakini ukweli ni kwamba wewe si kazi yako, wewe si cheo chako. Wewe ni zaidi ya kazi yako. Na kazi yako sio wewe.
MIMI NI NANI?
Naweza kujibu hivi.
Mimi ni mimi duniani kote, nipo mimi mwenye mawazo ya aina yangu, hakuna mwingine kama mimi, Nikifa. Akizaliwa mwingine akapewa jina langu, atakua mwingine mwenye jina langu. Mimi hana mbadala ila kuna mwingine atakayefanya niliyofanya. Mimi hawezi kua ndani ya mwingine popote, kabla yangu na baada yangu.
Je! Wewe ni Nani?