Western Union Tanzania inahujumiwa?

Netanyahu

Senior Member
Oct 2, 2008
147
22
Ukitaka kutuma pesa nchi nyingine kupitia western union Tanzania imekuwa vigumu mno.Wanataka uwe na passport sijui na viza za huyo unayemtumia na vikolokolo vingine kutegemea wanavyojua wenyewe na unapeleka wapi.Hawajali hata unatuma kiasi gani.Hata kama ni dola 10 au 20 utadaiwa vikolokolo kibao.Hivi dola 10 ,20 au 100 hivi nayo inaangukia kwenye kundi la Money laundering au Capital flight? Na hiyo ni kwa Tanzania tu?

Matokeo yake kwa taarifa za mitaani nilizonazo watu wanasafiri na mabasi kwenda Kenya,Zambia au Uganda na kuzituma pesa kupitia Ofisi za Western Union za nchi hizo ambako hakuna ujinga kama huo wa ofisi za western union za Tanzania.Matokeo yake ofisi za western union za nchi hizo zinaneemeka kwa commission nzuri na kuziacha za Tanzania ziko hoi.Je Western Union offices za Tanzania zinahujumiwa au ni kitu gani?
 
Mkuu umeleta point moja nzuri sana. Wetern Union ya Tanzania tayari imeingia uswahili, usanii haupo tu kwenye kutuma upo hata kwnye kupokea jamaa wanakata sana na wanaurasimu wa kijinga, ni kama wakomunisti vile. Labda tu-take trouble na kuwasiliana nao tusikie wanasemaje inawezekanahili hawalijui.
 
Sio Western Union peke yake, mbona hata MoneyGram sevices ambazo zinapatikana Exim wanadai copy ya passport, visa n.k za unayemtumia pesa. Sasa pengine ni standard procedure za TZ??
 
Tatizo sio western union, requirements za BoT ndio zinaifanya western union na other money transfer service providers kuhitaji hizo nyaraka kabla ya kuruhusu kutuma pesa. Hizi requirements ni kero sana. Hata ukitaka kufungua account mtindo ni huohuo. Just imagine inafungua ccount ya kampuni yako, then unaambiwa mojawapo ya mahitaji ni kuwa na makampuni mawili, yenye account kwenye hiyo brancha unayotaka kufungua, yakudhamini!!!
Huu ukiritimba unachelewesha maendeleo...
 
hakuna hujuma jamani,ni utaratibu tu waliopanga BOT
ila vizuri ungesema ni Bank gani iyo inayoleta usumbufu kwa wateja?
 
Si kweli kwamba ni Tanzania tu kwenye "ujinga huo", hii ni world wide hseria hii inatumika! Sasa wewe unamtumia mtu dola 10 au 20........!!! Nje ya nchi????
 
Mkuu umeleta point moja nzuri sana. Wetern Union ya Tanzania tayari imeingia uswahili, usanii haupo tu kwenye kutuma upo hata kwnye kupokea jamaa wanakata sana na wanaurasimu wa kijinga, ni kama wakomunisti vile. Labda tu-take trouble na kuwasiliana nao tusikie wanasemaje inawezekanahili hawalijui.

Hili la kupokea na kukatwa mkuu ni zuri sana,wengi tunapokea kupitia western union isjekuwa tunakatwa,hebu tueleze maana wengine tunapewa kiasi sawa na kilivyo kwenye fomu ya malipo...
 
Si kweli kwamba ni Tanzania tu kwenye "ujinga huo", hii ni world wide hseria hii inatumika! Sasa wewe unamtumia mtu dola 10 au 20........!!! Nje ya nchi????

Unashangaa nini watu wanatuma hizo hela ndogo kama dola 10,20,n.k kwa ajili ya application forms za kujiunga na vyuo mbalimbali duniani.kulipia subscription fees za vitu vidogo kama magazeti,n.k.

Ili watumiwe wanahitaji kulipa hizo hela kwanza.Njia ya western union inakuwa mara ingine ndiyo rahisi zaidi kuliko zingine zote kwa hela ndogo ndogo.
 
Sijui ni kwanini lakini yuko jamaa yangu alihitaji kumtumia mtoto wake pesa za kujikimu anayesoma UK, Western waligoma mpaka wapate copy ya passport na visa ya huyo mtoto huko UK. Na pesa hizo zilihitajika haraka maana alikuwa kaishiwa sasa huu si usumbufu??

Wakati ukiwa ulaya kutuma pesa TZ sio tatizo it is just a matter of seconds hela ziko bongo, kwa nini sie tuwe ving'ang'anizi na kuwekeana masharti lukuki? Mafisadi wametorosha fwedha nyingi sana, nina uhakika hakuna hata mmoja aliyetumia Western Union wote ni kupitia BoT! Hii ni kumnyanyasa mlala hoi ili waendelee kutubana na wao kujineemesha. Ngoja viboko vyao vyaja siku moja!
 
Wakuu, niliwasiliana na utawala wa Western Onion kuhusiana na utaratibu huo.. Kwanza sababu ilonifanya kupiga simu na kuongea nao ilikuwa kuhusu makato ya fedha kwa Mpokeaji huko TZ, wakanambia HAITAKIWI wala sio ruksa kabisa makato ya aina yoyote ikiwa gharama zote zimelipwa na mtumaji.. Na wakasisitiza kuwa utaratibu wao mtumaji ndiye hulipia gharama na sio mpokeaji..wakalifuatilia swala zima na ikaonekana kwamba kuna mchezo huo Bongo.. nadhani niliwahi kuandika hili miaka ya nyuma..
Hivyo walifuatilia swala langu na jamaa yangu alikwenda kuchukua kiasi ambacho alikuwa amekatwa na wafanyakazi wa Bongo..Hilo moja..

Kuhusu utaratibu wa kuonyesha vitambulisho pia walinambia kwamba sio matakwa yao isipokuwa ni matakwa ya serikali ktk kupiga vita Ugaidi..Tanzania ni moja ya nchi zilizoorodheshwa ktk makundi ya nchi zenye kambi za magaidi (Terrorist), na kwamba wafadhili wengi hutumia chombo hicho kutuma fedha ku finance organisation za kigaidi.. ni Orgs zipi hizo wala sijui na ndio maana hata huku majuu ukienda tuma fedha Western Union, mpokeaji akiwa na majina matatu yote ya Kiarabu ni issue kubwa sana..Siku za nyuma ilikuwa unakataliwa kabisa sasa hivi naona wamelegeza kidogo lakini bado kuna watu wanashindwa kabisa kutumia Western Union...
Hivyo chukulieni tu kwamba hivyo vitambulisho ni ktk Usalama zaidi ya ukorofi wa Western Union..
 
Ukitaka kutuma pesa nchi nyingine kupitia western union Tanzania imekuwa vigumu mno.Wanataka uwe na passport sijui na viza za huyo unayemtumia na vikolokolo vingine kutegemea wanavyojua wenyewe na unapeleka wapi.Hawajali hata unatuma kiasi gani.Hata kama ni dola 10 au 20 utadaiwa vikolokolo kibao.Hivi dola 10 ,20 au 100 hivi nayo inaangukia kwenye kundi la Money laundering au Capital flight? Na hiyo ni kwa Tanzania tu?

Matokeo yake kwa taarifa za mitaani nilizonazo watu wanasafiri na mabasi kwenda Kenya,Zambia au Uganda na kuzituma pesa kupitia Ofisi za Western Union za nchi hizo ambako hakuna ujinga kama huo wa ofisi za western union za Tanzania.Matokeo yake ofisi za western union za nchi hizo zinaneemeka kwa commission nzuri na kuziacha za Tanzania ziko hoi.Je Western Union offices za Tanzania zinahujumiwa au ni kitu gani?

sielewi lawama zinatoka wapi. Mimi ni mtumaji na mpokeaji sana wa western Union. hata sasaivi masaa matatu yaliyopita nilikuwa pale ubungo plaza natupa pesa. hakuna kitu kama icho, isipokuwa kwenye branch ya bank moja tu, Bank ya Kenya commercial Bank ya pale Mlimani city, ndio ukienda kutuma au kupokea pesa, wanataka passport au kitambulisho chako na wanakiphotocopy ndo upokee au utume pesa. wale KCB wa pale mlimani city wengi wamekimbia. Ukienda kwenye branch zote za Bank ya posta, hakuna usumbufu kama huo na hawahitaji kitambulisho chako. sijawahi kuombwa kitambulisho mimi na bank ya posta hata siku moja na matawi yote kuanzia posta, ubungo plaza, mlimani, millenium tower na kwingine kote. tuambie ulienda branch gani hiyo? kama ni ile bank ya wakenya pale mlimani city, imenitokea mara tatu nikahama kabisa. mara ya kwanza nilikuwa napokea pesa, wakataka kitambulisho nikawa nimesahau home kwasababu nilikuwa sijazoea kutoa vitambulisho wakati wa kupokea wala kutuma.

Nilisafiri nikamtumia waifu kwa western union, akaenda pale mlimani city bank ya kenya ile ya kijani, akaambiwa alete kitambulisho kama cha kura au passport etc ndio apokee, pamoja na kwamba ametoa swali na jibu lake na MTC number bila matatizo yoyote.

ukienda bank ya posta, ukawa na jina swali na jibu peke yake, ukaonyesha kitambulisho ukawa ni wewe wanakupa bila hata ile namba. au ukiwa na namba ukasahau swali na jibu unapata kama utaonyesha vitambulisho...ila bank ya kenya hawataki kitu kama icho, wanataka utaje kile kitu kuanzia swali, jibu, namba ya siri na uonyeshe passport au kitambulisho kinachoeleweka waphotocopy wabaki na copy yao ndo wanakupa. ni wagoloko sijawahi kuona.
 
sielewi lawama zinatoka wapi. Mimi ni mtumaji na mpokeaji sana wa western Union. hata sasaivi masaa matatu yaliyopita nilikuwa pale ubungo plaza natupa pesa. hakuna kitu kama icho, isipokuwa kwenye branch ya bank moja tu, Bank ya Kenya commercial Bank ya pale Mlimani city, ndio ukienda kutuma au kupokea pesa, wanataka passport au kitambulisho chako na wanakiphotocopy ndo upokee au utume pesa. wale KCB wa pale mlimani city wengi wamekimbia. Ukienda kwenye branch zote za Bank ya posta, hakuna usumbufu kama huo na hawahitaji kitambulisho chako. sijawahi kuombwa kitambulisho mimi na bank ya posta hata siku moja na matawi yote kuanzia posta, ubungo plaza, mlimani, millenium tower na kwingine kote. tuambie ulienda branch gani hiyo? kama ni ile bank ya wakenya pale mlimani city, imenitokea mara tatu nikahama kabisa. mara ya kwanza nilikuwa napokea pesa, wakataka kitambulisho nikawa nimesahau home kwasababu nilikuwa sijazoea kutoa vitambulisho wakati wa kupokea wala kutuma.

Nilisafiri nikamtumia waifu kwa western union, akaenda pale mlimani city bank ya kenya ile ya kijani, akaambiwa alete kitambulisho kama cha kura au passport etc ndio apokee, pamoja na kwamba ametoa swali na jibu lake na MTC number bila matatizo yoyote.

ukienda bank ya posta, ukawa na jina swali na jibu peke yake, ukaonyesha kitambulisho ukawa ni wewe wanakupa bila hata ile namba. au ukiwa na namba ukasahau swali na jibu unapata kama utaonyesha vitambulisho...ila bank ya kenya hawataki kitu kama icho, wanataka utaje kile kitu kuanzia swali, jibu, namba ya siri na uonyeshe passport au kitambulisho kinachoeleweka waphotocopy wabaki na copy yao ndo wanakupa. ni wagoloko sijawahi kuona.

Sasa sijui anayestahili sifa ni yule anayechukua tahadhari ili kuhakikisha fedha haziendi kwa mtu asiyehusika au ni yule mzembe anayechukua shortcut.... it is interesting Ubungoubungo anachekelea uzembe na anadharau uwajibikaji....
 
Back
Top Bottom