Werema kumpinga Pinda ni utovu wa nidhamu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Werema kumpinga Pinda ni utovu wa nidhamu Tuesday, 28 December 2010 20:32

werema.jpg
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema

Mpasuko uliomo katika Serikali ya Rais Kikwete juzi ulidhihirika wazi wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema aliposema kuwa hakuna uwezekano wa kuwa na katiba mpya, isipokuwa katiba iliyopo itafanyiwa marekebisho katika baadhi ya vipengele. Kauli hiyo aliitoa Ikulu, Dar es Salaam juzi, mara baada ya Rais Kikwete kumwapisha Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa suala la kubadilisha ibara zinazoonekana kutokidhi haja na kuingiza mambo mapya kwenye katiba linakubalika, lakini suala la kuandika katiba mpya hapana. Alisema kinachohitajika sasa hivi ni kupata michango mingi ya mawazo ya wananchi kuliko kupoteza muda kwa kile alichokiita kuzungumza kama bata kila kukicha.

Jaji Werema alitaka kujua ‘upya’ wa katiba unaotakiwa ni upi, na kuongeza kuwa sio sahihi kusema Watanzania wanataka katiba mpya wakati kauli za madai hayo zinatoka Dar es Salaam tu. Alisema sio lazima kila mtu anachokisema kifuatwe na akatoa mfano kuwa kule anakotoka, wafugaji watataka mambo ya ng’ombe yaingizwe kwenye katiba na Wahaya nao wanaweza kusema ndizi nazo ziingizwe kwenye katiba.

Huo ndio msimamo na mtazamo wa mtu mwenye dhima na wajibu wa kuishauri Serikali kuhusu masuala ya sheria na katiba ambaye haoni umuhimu wa kuwapo katiba mpya katika wakati na mazingira tuliomo hivi sasa. Ni msimamo wa mtu aliyelewa madaraka na asiyejua mipaka ya madaraka yake wala uzito wa kauli yake pale anaposema waziwazi kwamba “suala la katiba mpya hapana, lakini kuiweka viraka ile iliyopo ni ruksa”. Ni kauli nzito, ya kitemi na kidikteta ambayo hata Rais Kikwete ambaye ni kiongozi wa nchi hawezi kuitoa katika mazingira yaliyopo hivi sasa hata kama naye angekuwa na msimamo kama wa mteule wake huyo.

Ni msimamo hasi unaotolewa baada ya bosi wake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutoa msimamo tofauti Desemba 7, 2010 alipowaambia wahariri wa vyombo vya habari kuwa alikuwa haoni tatizo lolote katika kukaa na kuliangalia suala la kuwapo katiba mpya katika nchi yetu na akaongeza kuwa angemshauri Rais ili uwekwe utaratibu wa kuliangalia suala hilo. Alisema kuwa anadhani njia bora ni kuhusisha watu wengi kadri inavyowezekana, na ikibidi suala hilo lipelekwe kwa wananchi.

Kauli ya Waziri Mkuu Pinda imejaa busara na unyenyekevu anaposema atamshauri Rais. Somo analowapa viongozi wa Serikali, akiwamo Jaji Werema, ni kuwa yeye hana kauli ya mwisho na anatambua kuwa juu yake iko mamlaka kubwa zaidi ambayo ni Rais Kikwete. Hivyo, Jaji Werema anapokurupuka na kutangaza kuwa katiba mpya hapana anakuwa ni mtovu wa nidhamu, kwa sababu ameitoa wakati bosi wake tayari ametoa msimamo tofauti na bahati mbaya Rais Kikwete hajatoa msimamo wowote kuhusu suala hilo.

Ni utovu wa nidhamu uliopindukia, hasa tukitilia maanani kwamba tayari viongozi kadhaa wa nchi, wakiwamo Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Warioba na Frederick Sumaye na Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani nao wameshauri iandaliwe katiba mpya. Kwa vigezo vyovyote vile, Jaji Werema kwa elimu na uzoefu wake wa uongozi ni mithili ya kichuguu mbele ya viongozi hao ambao wako juu kama Mlima Kilimanjaro.

Inatia simanzi kuona pia kuwa hata baada ya viongozi wa kidini, vyama vya siasa, wanaharakati, vyama vya wafanyakazi , Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na wananchi kwa ujumla kutaka katiba mpya, bado anajitokeza mtu na kutoa kauli zenye kuchochea hasira za wananchi ambao wanadai katiba mpya ambayo italinda umoja na mshikamano wetu na kutuepusha na uwezekano wa kutokea machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika siku za usoni. Sisi tunasema Jaji Werema ni mtovu wa nidhamu, awajibishwe.
 
Inatia simanzi kuona pia kuwa hata baada ya viongozi wa kidini, vyama vya siasa, wanaharakati, vyama vya wafanyakazi , Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na wananchi kwa ujumla kutaka katiba mpya, bado anajitokeza mtu na kutoa kauli zenye kuchochea hasira za wananchi ambao wanadai katiba mpya ambayo italinda umoja na mshikamano wetu na kutuepusha na uwezekano wa kutokea machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika siku za usoni. Sisi tunasema Jaji Werema ni mtovu wa nidhamu, awajibishwe.

Kuna wa kumwajibisha huyu?
 
...awachefua Wadau wa Katiba
Tuesday, 28 December 2010 20:50

Waandishi Wetu

MSIMAMO wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kutaka isiandikwe katiba mpya badala yake iliyopo iwekewe viraka, umewakera wasomi, wanasiasa na wanaharakati ambao kwa nyakati tofauti jana walimtaka akae kimya kwa kuwa hana mamlaka ya kuwaamulia Watanzania mambo yao.

Wakati wadau hao wakizungumzia suala hilo kwa uchungu, mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Peter Kisumo, amekitaka chama hicho kutoa tamko linaloonyesha msimamo wake kuhusu mjadala huo.

Kisumo amesema CCM haipaswi kuogopa kuongoza mchakato wa mabadiliko ya Katiba kwa kuwa mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yaliyotokea nchini tangu mwaka 1977, yanalazimisha kuwapo kwa Katiba mpya.

Kisumo, aliitahadharisha CCM na kuitaka iitazame vizuri agenda ya mabadiliko ya Katiba vinginevyo itaonekana ni agenda ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kukipa umaarufu wa bure chama hicho.


"Tusiogope suala la kuleta mabadiliko ya Katiba na mimi naitahadharisha CCM kama haitakuwa msitari wa mbele kuongoza agenda hii basi itaonekana ni agenda ya Chadema kama ilivyotokea katika suala la vita ya ufisadi,"alisema Kisumo.

Mwanasiasa huyo ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa mabadiliko ya Katiba mwaka 1977, alifafanua kuwa mabadiliko ya katiba ya mwaka 1977 yalisukumwa na kuungana kwa vyama vya TANU na Afro Shiraz Party (ASP).

"Sasa tangu wakati huo kumetokea mambo mengi ambayo yanaifanya Katiba yetu ionekane haikidhi haja…mathalani Katiba yetu bado inasema tunajenga nchi ya Kijamaa hivi ni ya kweli haya kwa hali ya sasa?"alihoji Kisumo.

Kisumo alisema hata madaraka makubwa ya kikatiba ya Rais katika kuteua watu kuingia kwenye Utumishi wa Umma ikiwamo Ubunge, ni makubwa mno na kusisitiza kuwa suala la Wabunge wa kuteuliwa na Rais limepitwa na wakati.

Mwanasiasa huyo aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikali ya awamu ya kwanza ya Hayati Jullius Nyerere, alisema ibara hiyo iliingizwa kuhofia uwezekakno wa Rais kukosa Wabunge wenye sifa ya kuunda Baraza la Mawaziri.

Lakini badala yake alisema hivi sasa kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu ambayo ifikapo mwaka 2015, Watanzania watakuwa wamesoma hadi kidato cha nne na wakati huo huo idadi ya wenye shahada itakuwa lukuki.

"Majimbo yatapata Wabunge wasomi tu kwa sababu kiwango cha chini ya Elimu ya lazima itakuwa kidato cha nne ifikapo 2015 kwa hiyo hakuna sababu tena ya Rais kuteua watu maalumu kuwa Wabunge,"alisema Kisumo.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba jana aligoma kujibu hoja hizo za Kisumo na kusema,"Mimi kwanza nipo katika gari, lakini pamoja na hayo mimi siwezi kuongelea suala hilo, hata kama ni kuziba viraka au kuundwa kwa katiba mpya, mimi siwezi kusema lolote bwana," alisema Makamba.

Lakini mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kitengo cha Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma, Bashiru Ally alisema mwanasheria mkuu hana mamlaka ya kusema iundwe au isiundwe katiba mpya.

"Anachofanya Mwanasheria mkuu sasa ni kulinda matakwa ya serikali yake lakini hana haki kuzima mjadala wa Watanzania," alisema Bashiru.

Bashiru alifika mbali zaidi na kueleza kuwa, mwanasheria huyo wa serikali hana mamlaka ya kuzungumzia suala la katiba hasa ikizingatiwa kuwa ofisi yake, imeliingiza taifa katika hasara kubwa kutokana na kuingia mikataba mibovu.

"Nadhani, tunayo mifano mingi halisi inayoonyesha utendaji mbovu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu. Imekuwa ikisaini mikataba mibovu inayolisababishia taifa hasara na pia imekuwa ikipisha miswada mbalibali mibovu. Kwa hiyo, lazima msimamo wake utazamwe kuwa ni wa msingi sana," alisema Bashiru.

Kwa mujibu wa Bashiru siyo sawa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kusema katiba inahitaji viraka badala yake anatakiwa kutekeleza matakwa ya Watanzania ambao ndio waajiri wake.

Mkurugenzi wa Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Agenda Participation 2000 Moses Kulaba, alisema kauli ya Jaji Werema, ni kichekesho.

"Mahitaji ya katiba mpya ni makubwa, kauli zake za kufananisha Tanzania na India kwa kweli zimepitwa na wakati. Sasa Tanzania inahitaji Katiba mpya," alisema Kulaba.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema Erasto Tumbo alisema kitendo cha mwanasheria mkuu wa Serikali Frederick Werema kukataa mabadiliko ya katiba, kimetokana na uroho wa madaraka.

Alisema kisheria katiba ni ya watanzania na yeye ni mshauri wa serikali juu ya mambo yahusuyo sheria na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri asiye na kura hivyo hana sifa za kuzungumiza katiba mpya.

"Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 Ibara ya 54 kifungu kidogo cha 4 yeye ni mshauri wa serikali juu ya mambo yahusuyo sheria na pia ni mjumbe wa baraza la mawaziri asiye na kura, sasa anapopinga mabadiliko ya katiba, anazungumza kama nani?" alihoji Tumbo na kuendelea "yeye anatakiwa akae kimya, awaache watanzania waendelea na madai yao.
Habari hii imeandaliwa na Fidelis Butahe, Hussein Issa, Raymond Kaminyoge, Fredy Azzah na Daniel Mjema
 

"Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 Ibara ya 54 kifungu kidogo cha 4 yeye ni mshauri wa serikali juu ya mambo yahusuyo sheria na pia ni mjumbe wa baraza la mawaziri asiye na kura, sasa anapopinga mabadiliko ya katiba, anazungumza kama nani?" alihoji Tumbo na kuendelea "yeye anatakiwa akae kimya, awaache watanzania waendelea na madai yao.

Kwa kuongezea hapo Katiba Mpya siyo hata ya baraza la Mawaziri ni ya raia wote....................
 
@Rutashubanyuma..... mkuu huyu FW yupo kwenye mihimili yote mitatu... ni Jaji.. (Judiciary), Mwanasheria mkuu..(executive) ...na pia ni mbunge..(parliament) ...... je ndiyo kiburi chake au tunahitaji au ndiyo mapungufu ya katiba hii
 
Ulimi wamponza Mwanasheria Mkuu


Na Waandishi Wetu

KAULI mbili tata za Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema kuhusiana na suala la malipo ya sh. bilioni 185 kwa kampuni ya Dowans na kupinga kuandikwa upya kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zimepokelewa kwa
maoni tofauti na wananchi katika maeneo mbalimbali.

Wakizungumza na Majira kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya wanasheria wakiwemo vigogo serikalini walisema Jaji Werema amejisahau kuwa ni mshauri wa Serikali na si mtoa hukumu.

"Kwanza kauli ya Jaji Werema ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali imewashangaza na kuwashtua sana wanasheria wengi wa ndani na hata wa wale nje tuliozungumza nao asubuhi ya leo (jana).

Nadhani amejisahau kuwa yeye bado ni Jaji wa kutoa hukumu mahakamani, hajui kuwa kazi yake ni kuishauri serikali hasa rais, katika masuala ya kisheria na si kutoa hukumu mapema," alisema mmoja ya kigogo wa serikali na kusisitiza jina lake kutotajwa.

Alisema alichotakiwa kufanya Jaji Werema ni kuishauri Serikali kusitisha hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) baada ya kuandikisha hukumu hiyo katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

"Kwa mujibu wa sheria za migogogoro ya kibiashara za Tanzania hukumu hiyo bado inaweza kubatilishwa na Mahakama Kuu kupitia kitu kinachoitwa Judicial Review baada ya kuandikishwa, huo ndio ushauri ambao Jaji Werema angetakiwa kuutoa kwa serikali badala ya kuwajengea hofu wananchi," alisisitiza.Alisema wana hofu kama Jaji Werema alipitia jalada la hukumu hiyo yeye mwenyewe na kuelewa kilichomo kwa kuwa ushauri wake ni tofauti na hali halisi.

Alisema wao kama wanasheria wanamtaka Jaji Werema kuishauri serikali kuhoji sababu ya wahusika kushindwa kuandikisha hukumu hiyo mahakama Kuu ili kuruhsu hatua zaidi badala ya kuwachanganya wananchi kwa kauli tata.

"Sisi tuna taarifa kuwa mafisadi wanaohusika na Dowans wanaogopa kuandikisha hukumu hiyo Mahakama Kuu kwa kuwa majina yao yatatajwa, wanahofia Watanzania kuwatambua, hili Jaji Werema hajui? alihoji kigogo huyo.

Alishauri Rais Jakaya Kikwete, kuingilia kati suala hilo kama alivyoomba na baadhi ya wananchi kwa kuagiza hukumu hiyo kuandikishwa haraka Mahakama Kuu ya Tanzania au kufunga mjadala huo hadi wahusika watakapotekeleza kipingele hicho.

Mwanasheria mwingine ambaye yuko karibu na Jaji Werema alisema hakuamini kama kiongozi huyo angetoa kauli hiyo kwa kuwa ni mapema mno kufanya hivyo kwa kitu ambcho bado mlolongo wake ni mrefu."Inakuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali aoneshe dalili ya kunyong'onyea mapema kwa kitu ambacho kwanza hakijulikani, hata anayeidai Tanzania hafahamiki ni nani" alisema.

Alisema walitarajia Jaji Werema angeishauri serikali kusubiri kwanza hadi wahusika wa Dowans watakapoandikisha hukumu hiyo Mahakama Kuu ndipo atoe ushauri na si kuongeza mkangaiko."Mimi nadhani Jaji Werema hakusoma hukumu hiyo vizuri, kilichopo mle ni kuwa Dowans wenyewe wanakiri kuvunja mkataba kutokana na kile walichosema ni mazingira ya Tanzania kutoruhusu uwekezaji wao.

Na hata kilichoamuliwa ni Dowans kulipwa madai ya malimbikizo mbalimbali ya huduma, si kwa kuvunjwa kwa mkataba kama inavyodaiwa," alisisitiza.Katika hatua nyingine, baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga walikwenda mbali zaidi na kumtaka Jaji Werema kujiuzulu wadhifa wake, wengine wakidai kuwa huenda anatumika vibaya pasipo yeye mwenyewe kujielewa.Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Majira mjini hapa jana, wakazi hao walisema kitendo cha Jaji Werema kufunga mjadala wa malipo ya Dowans ni sawa na kutumia ‘udikiteta' katika jambo ambalo wananchi walipaswa kufahamishwa undani wake kwa kina
kabla ya malipo.

Walisema madai yaliyotolewa na Jaji Werema kupitia vyombo vya habari kwamba baada ya kuipitia na kuisoma hukumu iliyotolewa na mahakama ya kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC) amekubali kuwa hukumu hiyo iko sahihi ni sawa na kuwauza Watanzania.

Bw. Khalid Kyaruzi alisema "Kwa kweli hapa mwanasheria wetu ameonesha wazi kuwa ameshindwa kutumia wadhifa wake
katika kuitetea nchi, wapo watu wanafikishwa mahakamani kwa makosa halisi kabisa, lakini bado wanakana kutenda makosa hayo kwa nguvu zote, na wakati mwingine wanashinda kesi.

"Leo mwanasheria wetu anakubali kirahisi tu kwamba hukumu hiyo ni sahihi, tunauliza kwa misingi ipi, nani mmiliki wa Dowans…tutajiwe ni nani mwenye hiyo Dowans, Werema (Jaji) si amtaje?" alihoji.Kwa upande mwingine, mmoja wa watumishi wa serikali mkoani Shinyanga ambaye hakupenda kutajwa jina alidai kuwa kitendo cha Jaji Werema kukataa kuwepo kwa katiba mpya hapa nchini kinaonesha jinsi gani mwanasheria huyo asivyoweza kwenda na wakati.

"Watanzania wote pamoja na baadhi ya viongozi wastaafu na walioko madarakani wanakubali kuwa suala la katiba mpya linazungumzika, lakini mwanasheria wetu anakurupuka na kudai kuwa hakuna haja, bali kinachowezekana ni ‘kuiwekea viraka zaidi hii ya sasa', nafikiri huyu bwana anatumika vibaya," alieleza mtumishi huyo wa umma.

Mtumishi huyo alishangazwa na kauli ya Jaji Werema kwamba katiba iliyopo inastahili kuendelea kuwepo na kwamba kama suala la masahihisho ni bora katika baadhi ya vipengere badala ya kuandikwa mpya na kutoa mfano wa katiba ya India ambayo alidai imefanyiwa marekebisho zaidi ya mara 50.

Naye mmoja wa wajumbe wa Baraza la wa wazee wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mjini Shinyanga ambaye hakupenda pia kutajwa gazetini amemuomba Rais Kikwete akubali kulizungumzia suala la malipo ya sh. bilioni 185 kwa kampuni ya Dowans kwa kumtaja mmiliki wake.Suleiman Abeid, Shinyanga na John Daniel, Dar

 
@Rutashubanyuma..... mkuu huyu FW yupo kwenye mihimili yote mitatu... ni Jaji.. (Judiciary), Mwanasheria mkuu..(executive) ...na pia ni mbunge..(parliament) ...... je ndiyo kiburi chake au tunahitaji au ndiyo mapungufu ya katiba hii

ndio mapungufu hayo.
Inabidi kuwe na separation of power. Sasa kama mtu mmoja anacover sehemu zote tunaelekea wapi!
Mavyeo mengi ndio maana wanashindwa kutumikia jamii effectively. Shame on him.
 
CUF yawasha moto wa Katiba Dar
• Risasi zalindima, 20 wajeruhiwa kwa kupigwa virungu

na Asha Bani


amka2.gif
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimewasha moto wa madai ya Katiba Mpya kwa kufanya maandamano, lakini wafuasi wake waliambulia kipigo kutoka Jeshi la Polisi ili kuwatawanya waandamanaji hao.
Maandamano hayo ambayo ni ya kwanza kufanyika kwa lengo la kutaka kushinikiza mabadiliko ya Katiba, yalifanyika jana kuanzia ofisi ya Makao Makuu ya chama hicho yaliyoko Buguruni kwenda katika ofisi ya Waziri wa Katika na Sheria, Celina Kombani.
Hata hivyo Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, lilizidiwa ujanja na wafuasi wa CUF kwani licha ya kupigwa na kutawanywa, kundi lingine lilifanikiwa kupita njia za vichochoroni na kuwasilisha rasimu ya Katiba yao Mpya ofisini kwa Waziri Kombani.
Jeshi hilo kupitia Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, juzi lilipiga marufuku kufanyika kwa maandamo hayo na kuahidi kuimarisha ulinzi kwa madai kuwa hayakuwa halali kisheria.
Hata hivyo, wafuasi wa chama hicho kutoka maeneo ya Buguruni walijitokeza kwa wingi majira ya saa 4:30 asubuhi kwenye ofisi za CUF na kuanza maandamano.
Maandamano hayo yalianza majira ya saa 4:30 asubuhi katika ofisi kuu za chama hicho Buguruni jijini Dar es Salaam ambapo kabla ya kuanza, gari nne za polisi (Defenders) zilifika kwa ajili ya kuzuia maandamano hayo.
Tanzania Daima Jumatano ilishuhudia magari hayo yaliyokuwa na namba za usajili za PT 0890, PT 1144, PT 1858, T778 AFG na gari la maji ya kuwasha namba PT 0837.
Magari hayo yaliyosheheni askari waliokuwa na silaha, yaliweka ulinzi mkali katika barabara ya uhuru hadi eneo la Karume ambapo maduka, usafiri wa daladala na biashara nyingine, zilifungwa kwa saa kadhaa.
Wafuasi hao waligawanyika katika makundi mawili ambapo moja lilipita barabara ya Uhuru na kusambaratishwa na polisi na lingine lilipita njia za vichochoroni na kuibukia katika mitaa ya Arusha Ilala na kufanikiwa kufika wizarani.
Hata hivyo majira ya saa 4:50 askari waliokuwa katika Defender namba T 778 AFG, PT 1858 na T 547 AVG walipita na kuimarisha doria katika mitaa hiyo na kukumbana na baadhi ya wafuasi wengine wakiwa wanaelekea wizarani kwa maandamano na hapo ndipo walipoanza kurusha risasi za moto kila kona ya mtaa ili kuwatawanya.
Zaidi ya saa moja hadi kufikia majira ya saa sita mchana, risasi zilikuwa zikilindima hewani na hofu kutanda kwa wananchi wanaoisha maeneo hayo huku wafanyabiashara wakiwa wamefunga maduka yao kuhofia vurugu hizo.
Risasi ziliendelea kupigwa na askari polisi waliokuwa katika Defender PT 1858 na T 778 AFG na hatimaye kuwakamata wafuasi kadhaa na kuwapeleka katika kituo kidogo cha polisi Karume huku wakiwa wamefungwa pingu mikononi.
Maandamo hayo yaliongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Julius Mtatiro, aliyekuwa katika gari lenye namba T 438 AGZ majira ya saa 6:5 mchana, na kufanikiwa kuwasilisha rasimu ya Katiba kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Oliver Mhaiki ambaye aliipokea kwa niaba ya Waziri Kombani ambaye hakuwepo ofisini kwake kwa muda huo.
Huku Naibu Katibu Mkuu huyo wa CUF akiwa ndani ya jengo la Wizara ya Sheria na Katiba, kundi kubwa la wanachama wa CUF lilitanda katika mitaa ya Mani Fild Posta na kushindwa kufika makao makuu ya wizara kutokana na ulinzi wa askari polisi waliokuwa wamezingira jengo hilo.
Habari zaidi zilisema zaidi ya watu 20 wamejeruhiwa katika sakata hilo huku watu kadhaa ambao idadi yao haikuweza kujulikana mara moja, wakishikiliwa na polisi kwa kuhusika na maandamano hayo ambayo yanadaiwa kutishia amani na usalama.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha rasimu ya Katiba hiyo Mtatiro, alisema azma waliyokuwa wameikusudia imefanikiwa.
'Tulitaka kuwasilisha rasimu ya Katiba Mpya na lengo hilo limetimia hata kama wenzetu wengine wamepigwa na kukamatwa na polisi,'� alisema Mtatiro.
Alisema rasimu hiyo ina kurasa 88 sura 36 ibara zaidi ya 130 ambayo itatawanywa nchi nzima kwa wananchi ili waweze kuongezea mabadiliko yenye manufaa kwao na kwa wananchi wote.
 
Werema anataka machafuko - Wananchi


na Samwel Mwanga, Maswa


amka2.gif
SIKU moja baada ya Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Fredrick Werema, kupinga madai ya kuandikwa kwa Katiba mpya, akidai iliyopo inafaa na kama kuna matatizo ifanyiwe marekebisho, kauli hiyo imeonekana kuwakasirisha sana wananchi. Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Maswa baadhi ya wananchi katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu wamesema kuwa kauli yake hiyo huenda ikaleta machafuko hapa nchini.
Kwa mujibu wa maelezo yao, suala la kuandikwa kwa katiba mpya si la hiari kwa sasa bali ni la lazima kwani iliyoko imepitwa na wakati.
Wananchi hao walionekana kumshangaa Mwanasheria Mkuu huyo kwa kutumia maneno ya kejeli katika kuzungumzia suala nyeti kama hilo ambalo linaungwa kwa kiasi kikubwa.
Kadhalika hasa wakati huu ambapo mjadala huo umeendelea kupamba moto kwa kuungwa mkono na makundi mbalimbali wakiwemo wanasiasa, wasomi na wanaharakati.
'Kwa kweli ni jambo la kushangaza mtu kama Jaji Werema kutumia maneno ya kejeli katika kuzungumzia suala la uanzishwaji wa katiba mpya huku Watanzania wa kawaida, wanasiasa, wasomi na wanaharakati wakieleza bayana wanahitaji katiba mpya huku ni kutaka kusababisha machafuko hapa nchini,'� alisema Donald Julius.
Kadhalika akizungumza kwa niaba ya wenzake mmoja wa wananchi hao, alisema licha ya nafasi aliyonayo serikalini hawezi kuzuia wananchi kujadili kuandikwa kwa Katiba mpya kwani si ya kikundi cha watu.
Wananchi hao wamemuonya, Mwanasheria Mkuu huyo kuwa aache kutumia majibu ya zamani kwa maswali mapya na kumtaka asome nyakati vinginevyo hawezi kuishinda nguvu ya umma.
Pia walisema kauli ya Mwanasheria Mkuu kwamba 'Marekebisho ya Katiba ni ruksa'� na 'kuandikwa kwa Katiba mpya si ruksa'� ni kauli za kulewa madaraka tena zilizojaaa ubinafsi na udikteta ambazo hazikupaswa kutolewa na kiongozi huyo wa ngazi za juu hapa nchini.
Aidha walilalamikia kauli ya Jaji Werema kuwafananisha wananchi wanaojadili kuwepo kwa katiba mpya na bata jambo ambalo walisema ni vizuri awaombe radhi Watanzania vinginevyo watamwomba Rais Jakaya Kikwete kumwondoa katika nafasi hiyo.
Mjadala wa kutaka katiba mpya iandikwe uliibuka, mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ambako wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walipotoka nje ya Bunge wakati Rais Jakaya Kikwete akilihutubia Bunge wakidai hawaitambui katiba iliyomuingiza madarakani.
Pia wakidai kuwa Katiba ya sasa ina upungufu mkubwa ambao hauwezi kumalizwa kwa marekebisho bali kwa kuandikwa Katiba upya.
 
Mwanasheria Mkuu anapokuwa na matege ya kifikra


Josephat Isango

amka2.gif
UZEMBE wa kufikiri sio ugonjwa mzuri sana. Uzembe wa kufikiri huwakumba watu wa jinsia zote. Uzembe huo huo huwakumba watu wa rika zote, bahati mbaya sana uzembe wa kufikiri umeingia katika idara mbali mbali za serikali, na hivyo kupenda kufanya kazi kwa mazoea, na uzembe huo bila aibu umetinga mpaka kwa Mwanasheria Mkuu. Mwanasheria Mkuu amekurupuka, bila kutafakari anachokisema. Anasema kuwa hoja ya kuandika katiba mpya haina mashiko, isipokuwa kubandika viraka.
Akifafanua kuhusu Katiba hiyo ya mwaka 1977, Jaji Werema alisema, 'Tunapaswa kujiuliza Watanzania wanahitaji nini? Mimi binafsi ukiweka wadhifa wangu kando, bado sioni haja ya Katiba Mpya.'�
Alisema serikali iko tayari kufanya kile Watanzania wanachokitaka bila wasiwasi kwa kuwa ipo kwa ajili yao, lakini si kufanya matakwa ya mtu fulani na kuongeza kuwa hoja zinapaswa kuletwa mezani na kuzungumzwa kwa pamoja.
Sijajua vema huyu mwanasheria mkuu anapotaja watanzania, anawataja akina nani, na anawaondoa akina nani? Ina maana waliojitokeza hadharani kuzungumzia katiba mpya sio Watanzania? Waliojitokeza mapema katika suala hili walianza wabunge wa CHADEMA kwa kususia hotuba ya Rais mjini Dodoma, wakisema kuwa Kikwete ni Rais kwa sababu ya katiba mbovu, wapo viongozi wakubwa waliojitokeza kuunga mkono suala hilo, wapo walioona umuhimu wa katiba mpya wakiwemo, Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba, Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, Mwanazuoni maarufu nchini, profesa Issah Shivji, Prof. Mwesiga Baregu, Mwandishi wa Habari maarufu nchini Jenerali Ulimwengu na wengine ambao wameandika au wamesema kuhusu Katiba mpya.
Hata CUF waliolazimika kuandamana jana na kupigwa virungu, wanataka Katiba Mpya na katika hili pengine hawana sababu ya kuangalia ndoa yao na CCM.
Wapo pia wasomi mbalimbali wa vyuo vikuu, wapo viongozi na wafuasi wa vyama vya siasa, wapo wanaharakati mbalimbali, je wote hawa kwa mtazamo wa mwanasheria mkuu huyu sio watanzania?
Mwanasheria huyu anawanyang`anyaje uraia wananchi hawa? . je matakwa ya mtu anayoyataja anataja matakwa ya nani? Je huyo mwenye matakwa hayo sio mtanzania? Imekuwaje mwanasheria mkuu akawa mbaguzi kiasi kikubwa hivi?
Mwanasheria huyu anapotaja Watanzania, anataka wote tutoke majumbani tukusanyike katika ukumbi upi ili aelewe kuwa sisi tunaodai katiba mpya ni Watanzania? Je kuna ukumbi maalumu wa watanzania kukutana kwa ajili ya maamuzi kuhusu nchi yao? Je ni chini za uenyekiti wa nani?
Mwanasheria Mkuu anapinga serikali. Anampinga waziwazi Waziri Mkuu ambaye yeye ameona umuhimu wa katiba mpya na kuahidi kumshauri Kikwete ili achukue maamuzi magumu tuweze kurekebisha mfumo uliopo kwa kuingia mkataba mpya unaofaa kati ya watawala na watawaliwa.
Inakuwaje Mwanasheria Mkuu anapokuwa dikteta? Nani amemteua Mwanasheria Mkuu kuwa msemaji wa watanzania kuhusu mambo ya katiba?. Mwanasheria huyu hana nia njema na Tanzania, anapenda katiba iliyopo inayotumikia mafisadi kuendelea kukandamiza taifa letu. Hatutaki kumwaga damu, ila hatuna haja na mwanasheria wa aina hii.
Watawala akiwemo Mwanasheria Mkuu hawafikiri zaidi ya hapo. Kauli za 'wanaotaka kuleta vita na kuondoa amani, au kusema ni kauli ya mtu binafsi'� ni silaha kuu za watawala katika kunyamazisha umma na hata kuufanya usifikiri tofauti. Hata kama ni wazo la mtu binafsi lenye manufaa kwa watanzania wote tunaliunga mkono. Kama mawazo za mtu binafsi ni mabaya, Werema alishirikiana na nani kusema kuwa Katiba mpya haihitajiki?
Kwa miaka 18 sasa tangu 1992 ulipoanzishwa mfumo wa vyama vingi, kumekuwa na madai ya wazi kwenye majukwaa ya siasa kuwa nchi inahitaji katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.
Watawala ama wametoa majibu ya kejeli au wamekaa kimya. Walichoona kwenye marekebisho ya katiba ni kutamka tu kwamba nchi ni ya mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Vizuizi, minyororo, pingu na magereza, vilivyomo ndani ya Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi, vimebaki vilevile. Siyo kwamba watawala hawavioni. Wanaviona kuwa ni vya ubabe, vya kihuni na katili,vilivyojaa ujanja ujanja lakini wanaviacha viendelee kuwemo kwa kuwa vinawasaidia kubaki madarakani.
Watanzania wamechoka, wapo wengi, na wapo ambao wanaweka maisha yao rehani kuhakikisha Katiba mpya inapatikana, wanajua kuwa katika kudai katiba watauawa, watatishwa na kuacha familia zao yatima, lakini hawakati tamaa, hawasemi kwa siri, wala hawataki kunong'oneza baadhi ya watu.
Wanasema hadharani tunataka katiba mpya, suala hili wala sio tajamala sio upendeleo wa viongozi, ni haki ya watanzania. Tunatuma jina hili kwa mzee wetu Ndimara, aendelee kuorodhesha idadi ya majina ya kupelekwa The Hegue, jina la Kombani lifuatiwe na la Fredrick Werema.
Mtu aweza kujiuliza: Kwa nini kuwe na katiba inayoruhusu mwanya wa kutenda uhalifu? Katiba yenye njama za uovu, iliyojaa ujeruri na kejeli kwa watu wake, Kwa nini kuwe na katiba inayotilia mashaka nguzo muhimu ya dola mahakama katika usimamizi wa haki?
Inawezekana watawala wanajua kuwa siyo wasafi? Kwamba hawana sifa isipokuwa ghiliba? Kwamba hawakubaliki isipokuwa kwa shinikizo? Kwamba hawawezi kumudu kushindanishwa na wengine mpaka kuwepo mwanya wa kukiuka taratibu, kanuni na sheria? Werema anataka tuendelee kuwa na viraka kama India na Marekani. Hivi mahitaji ya India na Marekani ndio mahitaji ya watanzania?
Tumezoea kudhulumiwa katika nchi yetu na watu hao, walioingiza nchi yetu katika ufisadi wa EPA na rada, tunawaita watanzania wenye asili ya kiasia, ambao muda sio mrefu tutaendelea kuangamia kulipa Dowans, bado Werema unataka tuige kwao. Tuige nini? Sisi hatuwezi kufikiri tukajitegemea?
Mwanasheria anayeleta ukoloni katika nchi yetu wa nini? Najua Kikwete hatamchukulia hatua, kwa kuwa Kikwete naye anafurahia kauli hizi. Lakini kitu kimoja tu tukubaliane, au tusikubaliane, watanzania wanataka mabadiliko hata katika vitisho na kauli dhaifu za kutiliwa mashaka kama hii ya Mwanasheria Mkuu.
Uamuzi wa ama Katiba iandikwe upya au irekebishwe ni wa wananchi walio wengi na kamwe hauwezi na wala haupaswi kuwa uamuzi wa viongozi wa serikali.
Sisi hatutaacha kufuatilia na kuchunguza kwa makini yale yanayojiri katika nchi hii, tunaweka wazi kwamba mpaka sasa wananchi waliojitokeza kutoa maoni yao kuhusu Katiba, wanataka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iandikwe upya.
Moja ya sababu kuu ya hitaji hilo kama lilivyobainishwa na wengi ni ukweli kuwa Katiba ya sasa ina mapungufu makubwa mno ambayo hayawezi kumalizwa kwa marekebisho bali kwa kuandikwa kwa Katiba upya.
 
CHADEMA: Werema amelewa madaraka


na Janet Josiah


amka2.gif
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemshangazwa na kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ya kupinga madai ya kuandikwa Katiba mpya na kusema kuwa mwanasheria huyo amelewa madaraka. Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, Erasto Tumbo, alisema Jaji Werema hakupaswa kutoa kauli kama hiyo kwa kuwa yeye si msemaji wa serikali wala Watanzania bali ni miongoni mwa washauri wa serikali.
Tumbo alimtaka Jaji Werema kufanya kazi yake aliyopewa na si kuingilia kilio cha Watanzania wengi ambao alidai ndiyo wenye uchungu nayo. Alisisitiza kuwa wakati anaonekana wazi kazi yake aliyopewa imemshinda anakimbilia kazi isiyomhusu!
Jana Jaji Werema alikaririwa akisema marekebisho ya Katiba ni ruksa kwa kuondoa baadhi ya mambo ya zamani na kuweka mambo mapya na kukataa kuandikwa kwa Katiba mpya.
Katika hatua nyingine, CHADEMA imemtaka Jaji Mkuu mpya wa Tanzania, Mohamed Chande Othman, kuendeleza mapambano ya kudai na kuandikwa Katiba mpya ambayo katika kipindi hiki imezua mjadala mkali.
Tumbo alisema CHADEMA inaamini Jaji Othman atauendeleza mjadala huo kama alivyouanza Jaji Mkuu Mstaafu, Augustine Ramadhan, ambaye alinukuliwa akisema umefika wakati kwa Watanzania kutoa maoni kuhusu uwepo wa Katiba mpya.
'Kutokana na wadhifa mkubwa alioteuliwa na Rais kama Jaji Mkuu anayo kila sababu kukabiliana na changamoto alizozikuta ukiwamo mjadala huo wa kuandikwa kwa Katiba mpya,'� alisema.
 
"UZEMBE wa kufikiri sio ugonjwa mzuri sana. Uzembe wa kufikiri huwakumba watu wa jinsia zote. Uzembe huo huo huwakumba watu wa rika zote, bahati mbaya sana uzembe wa kufikiri umeingia katika idara mbali mbali za serikali, na hivyo kupenda kufanya kazi kwa mazoea, na uzembe huo bila aibu umetinga mpaka kwa Mwanasheria Mkuu. Mwanasheria Mkuu amekurupuka, bila kutafakari anachokisema."

Kweli mwandishi kachana live!
 
Jamii imepata kichaa cha Katiba Mpya
ban.blank.jpg

Robert Nyanda

amka2.gif
'Katiba ni sheria mama'�; hii ni moja ya maana nyingi zinazoelezea maana ya neno 'katiba' ambazo zimependekezwa na wasomi na wachambuzi wa mambo ya kisiasa na kijamii. Maana hii hupendwa sana na wanafunzi wengi kuitumia wakati wa kujibu swali "katiba ni nini?" hasa katika masomo ya Civics na General Studies.
Huchagua maana hii kwa sababu kuu mbili: Mosi ni ufupi wa sentensi yenyewe. Hapa inamaanisha uchache wa maneno yaliyotumiwa kukamilisha maana yenyewe ambayo humfanya mwanafunzi kukariri kiurahisi. Pili ni matumizi ya neno 'mama'.
Kwa maneno mepesi 'mama' ni mzazi wakike kwa viumbe vyote ambavyo vinaongezeka kwa kutumia ufumo wa uzazi. Kati ya wazazi wawili wa watoto ni mzazi huyu ambaye huthaminiwa sana na watoto, kwa sababu ndiye mwenye jukumu zito la kulea mimba na kumtunza mtoto.
Hili haliko kwa binadamu tu, bali kwa kila kiumbe; mfano angalia ng'ombe, mbuzi, mbwa na viumbe wengine utaona mtoto kumtambua zaidi mama yake kuliko babaye. Kutokana na hulka hiyo wapowaliofikia kusema kuwa 'mzazi halali ni mama na baba ni mlezi tu'�.
Kuliamini hilo, hebu msikilize mtu anapopatwa na tatizo lolote lile. Neno la kwanza kutamka ni 'mamaaa!' hii inadhihirisha uwepo wa mama katika maisha ya mtu, hata kama hayupo kimwili, yupo kiroho.
Maelezo haya yote yanaonyesha umuhimu wa kuwa na mama. Kwa mantiki hiyo basi 'katiba' kuifananisha na 'mama', inaonyesha umuhimu wa pekee katika jamii yeyote ile.
Kwa kawaida mtoto huwafanana wazazi wake na kujifunza zaidi kutoka kwao, hasa mama ambaye anakuwa naye kwa muda mrefu zaidi. Kama mama atakuwa na tabia nzuri, haidhulu hata mtoto atakuwa vivyo hivyo, lakini pia kama atakuwa na tabia mbaya na hata mtoto haitaepuka kuwa hivyo.
Kwa mtazamo huo basi, jamii yeyote ile ikitaka kuwa na sheria nzuri zenye kukidhi matakwa ya watu wake, haina budi kuwa na katiba nzuri. Hii itatoa mwelekeo mzuri wa sheria dada na kaka ambazo hutokana na sheria hiyo mama.
Na sifa ya katiba ya namna hiyo ni ile tu, iliyoridhiwa na wananchi wenyewe na sio viongozi wachache wanaojali maslahi yao. Katiba ya namna hii, kama ikifuatwa ipasavyo na walinzi (viongozi) wake, huwa ni nadra sana kutokea kwa migongano ya kikatiba na sheria zake.
Kwa katiba ya Tanzania, hali ni tofauti kabisa na maana hiyo ya katiba niliyoitoa hapo juu. Hapa "katiba si sheria mama bali ni sheria baba". Maana yake ni kwamba haipendwi na watoto wake, hivyo huamua kufuata njia zao wenyewe bila kujali misingi ya baba yao.
Kutoka na hali hiyo, hapa inaonyesha kuwa watoto wote wa katiba ya Tanzania ni wakiume ambao kila mmoja huhitaji utwala na himaya yake, kutoka kwa babaye. Hapo ndipo unapotokea mgongano wa kikatiba, kwa sababu kila sheria inasimama yenyewe bila sheria ya msingi ya kuziongoza.
Kwa mfano tuitazame ibara ya 18 (1) na (2) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotoa uhuru wa mawazo na habari kwa watoto (wananchi) wake. Ibara hii imejieleza wazi kabisa kuhusu umuhimu wa mtu kutoa na kupokea ujumbe bila kubughudhiwa na mtu yeyote ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu.
Lakini sheria zinazoongoza vyombo vya habari, si dhani kama vilitokana na ibara hii au ibara gani ndani ya katiba hiyo. Mathalani, sheria ya magazeti (Newspapers Act) ya 1976, Penel Code ya 1945 na sheria ya Magereza (Prisons Act) ya 1970 kwa kutaja chache tu dhidi ya nyingi.
Sheria hizi zilitokana na katiba ipi? Wakati katiba iliyopo ni ya mwaka 1977? Ziliongezwa katika kifungu gani cha katiba? Je, nani mama yake? Au sheria hizi nazo ni katiba? Kama hazijatamkwa kwenye katiba, sasa zilitoka wapi?
Pamoja na uozo wa sheria hizi, bado katiba yetu haitambui vyombo vya habari! Ni ibara gani inayotamka kuwepo kwa vyombo vya habari na wanahabari? Hakika wataalam wa sheria mtanisaidia kujibu swali hili.
Ibara ya 18 inayodaiwa kulinda vyombo vya habari, si kweli. Ibara hii imejikita katika kutoa uhuru wa mawazo (Freedom of Expression) tu.
Ibara ya 18 (1) inasema, 'Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.'�
Na ibara ya 18 (2) inasema, 'Kila raia ana haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia juu ya masuala muhimu ya jamii.'�
Kwa vigezo hivi hapa hakuna ubishi kwamba vyombo vya habari na wanahabari wanafanya kazi zao nje ya katiba ya nchi. Na kutokana na ukweli huo, ndio maana matumizi ya sheria kandamizi (dragonian laws) nilizozitaja hapo juu, zinatumiwa na watawala bila wasiwasi.
Kwa manti hiyo, kilio cha kutaka katiba ambayo itakuwa sheria mama ndio sasa imepanda kichaa vichwani mwa wanahabari, viongozi wastaafu, baadhi ya viongozi waliopo madarakani ambao hawanufaiki na katiba iliyopo pamoja na wasomi na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani.
Joto hilo lakutaka katiba mpya limetiwa nguvu sana na uchaguzi wanne wa udiwani, ubunge na urais ndani ya mfumo wa vyama vingi. Ambapo baadhi ya wagombea wa kiti cha urais, ubunge na udiwani walionyesha kuwa katiba hiyo inakipendelea sana chama tawala.
Kwa upande wa chama tawala chenyewe hakiamini hivyo kwa sababu inalinda maslahi yake. Viongozi wake waandamizi wanazidi kuutangazia umma "katiba yetu ni nzuri na hatuhitaji katiba nyingine kwa sasa".
Ni kweli kauli hizi ni za kweli? Kwa watanzania wengi ambao wao uumini wao ni kwa viongozi wanaowapenda ni za kweli hata kama ni hatarishi. Huwezi kuwashawishi kwa sababu kiongozi wao kasema.
Lakini mimi pamaoja na watanzani wachache, siungi mkono hoja hizo na ninahitaji katiba mpya. Hii inatokana na ukweli kwamba katiba iliyopo ni ile ya "Westminister".
Maana yake ili tengenezwa nchini Wingereza katika kitongoji cha "Lancaster" na Waingereza kwa manufaa yao. Ndiyo maana inaibeba Penel Code Act ya 1945 sheria ambayo ilitungwa kabla ya taifa huru la Tanganyika na baadaye Tanzania.
Sisi watanzania tumekuwa tukiifanyia mabadiliko madogo madogo ili ifanane na mazingira ya kwetu, lakini imeshindikana na kwa sasa imetosha. Yawezekana hapo awali tulishindwa kutengeneza katiba yetu wenyewe ya Dodoma ama Dar es Salaam ama Mwanza, kwa sababu za kutokuwa na wasomi wengi wa mambo ya sheria za kitaifa na kimataifa.
Lakini kwa sasa tunahazina kubwa ya wasomi hao, wakianzia kwenye ngazi ya cheti hadi Maprofesa. Hawaishii hapo tu bali wamevuka hadi kwenye hadhi za uprofesa. Hivyo naamini kabisa tunaweza kutengeneza katiba yetu wenyewe yenye kuzingatia mazingira halisi ya Tanzania.
Viongozi wetu wamekuwa waoga katika hili kutokana na ukweli kwamba, nafuu nyingi wanazozipata zitaondolewa. Ni kweli lazima ziondolewe kwa sababu hazina maslahi kwa taifa.
Majaribio ya kutaka shaeria mama mpya yalianza tangu enzi za serikali ya awamu ya kwanza. Mjadala mkubwa wa kikatiba ulioibuka mwanzoni mwa maika ya 80, ulisababisha katiba hiyo kuwekewa kiraka kwa kuongezwa kwa ibara iliyotambua haki za binadamu 1984 na vingine vingi vilivyosababisha sera mpya za uchumi.
Pamoja na kuwepo kwa matakwa ya katiba mpya miongoni mwa walioitwa wapinzani wa katiba hii, bado hayati mwalimu Julius Nyerere na viongozi wenzake hawakuwa tayari kutunga katiba mpya. Kutokana na mfumo wa kisiasa wa wakati huo wa chama kushika hatamu, watu hao walinyamazishwa na mjadala huo ukakoma.
Mwanzoni mwa miaka ya 90, mjadala huu ukaibuka tena kwa kutaka mageuzi makubwa ya kisiasa na kiuchumi. Katika kutekeleza hilo, rais wa awamu ya pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi akalazimika kuunda tume iliyoongozwa na Hayati Jaji mkuu mstaafu Francis Nyarali.
Tume hiyo ili kuja na mapendekezo lukiki likiwemo la katiba, lakini cha kushangaza baadhi ya mapendekezo hayo yalitupiliwa kapuni na badala yake, katiba ikatiwa viraka tena kuruhusu mfumo wa vyama vingi kwa matakwa ya watawala wakipewa msukumo na uchumi wa dunia.
Pamoja na aslimia 80 ya watanzania kuukataa mfumo huu wavyama vingi na kupendekeza kuendelea na mfumo wa cha kimoja, viongozi walitumia rungu kuamua. Hatimaye mwaka 1992 vyama vingi vikaruhusiwa rasmi na soko huria likaanzishwa.
Baada ya kuruhusiwa kwa mfumo huu pamoja na uhuru wa kutoa mawazo, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa vyombo vya habari binafsi kulileta msukumo mpya tena katika kudai katiba mpya. Fukuto kubwa ambalo linaweza kukumbukwa katika miaka hiyo ni lile la kundi la G 55 mwaka 1994.
Kundi hili liliibukia bungeni likiwa na wapambanaji kama Njelu Kasaka mbunge wa Chunya na wenzake. Kimsingi kundi hili lilikuwa nadai moja la muhimu la serikali ya Tanganyika ambayo imepotezwa na katiba ya sasa bila kujua mstakabali wake.
Madai hayo yalimchukiza sana muasisi wa taifa hili na kufikia hatua ya kuwaapia baadhi ya waasisi wa kundi hilo kutoruhusiwa kushika nyadhifa kubwa za nchi.
Sakata la uchaguzi la 1995 wakati wa kinyang'anyiro cha nafasi ya urais kupitia tiketi ya CCM ni kielelezo tosha cha hasira ya muasisi huyo na viongozi wa chama chake kukumbatia katiba mbovu.
Joto la kudai katiba mpya bado ni changamoto kwa uongozi wa serikali ya awamu ya nne na serikali nyingine zijazo. Hakuna suruhisho jingine la matatizo yetu bali ni kuundwa kwa katiba mpya itakayozingatia vipaumbele vya watanzinia na sio waingereza ama wamarekani ama wachina kwa lugha ya uwekezaji.
 
Katiba mpya: Deni lililoibuliwa kwa kasi 2010 Wednesday, 29 December 2010 11:06

katibamazungumzo.jpg
John Tendwa(kulia), Ibrahim Lipumba (Katikati) na John Chipaka

Fidelis Butahe
DEMOKRASIA na utawala wa kidemokrasia ni moja ya dhana muhimu zinazoleta mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi yoyote duniani, sio tu ni vichochezi vya maendeleo bali ni mihimili mikubwa ya kupambana na umasikini.

Nchi ikikosa demokrasia na kanuni ambatanishi kama utawala wa sheria, heshima kwa haki za binadamu na utawala bora uwezekano wa kupambana na umasikini ni ndoto.

Nchini Tanzania kumekuwa na madai ya muda mrefu ya kubadilishwa kwa katiba kwa madai kuwa haikidhi matakwa ya watanzania na kwamba ina kilinda chama tawala (CCM).

Kukosekana kwa katiba yenye ridhaa halisi ndio chanzo kikubwa cha kugawanyika kwa jamii na kudumaa kwa maendeleo hasa katika nchi za dunia ya tatu na hasa zilizopo barani Afrika.

Hivi karibuni Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kiliandaa mkutano uliohudhuliwa na viongozi na wawakilishi wa vyama vyote vya siasa nchini kwa ajili ya kujadili umuhimu wa kuwa na katiba mpya.

Mkutano huo ulifanyika huku mawaziri wawili wakuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba na Frederick Sumaye, pamoja na Jaji Mkuu Agustino Ramadhan, Jaji Robert Kisanga,

Jaji Amir Manento, Jaji Mark Bomani, na mhadhiri wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Issa Shivji wakiwa wameshatoa maoni yao kuhusu kuundwa kwa katiba mpya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye pia ni mwenyekiti wa CUF, anasema kuwa katiba mpya inatakiwa itokane na mapendekezo ya wananchi, iwe ni misingi ya demokrasia, wananchi wawe na haki ya kuchagua na kuchaguliwa.

"Mbali na hilo rasilimali za nchi zinatakiwa kutumika kwa manufaa ya wananchi. Mpaka sasa katiba yetu tayari ina vikara 15 hivyo ni vyema ukaandaliwa mchakato mzito kwa ajili ya kulipatia ufumbuzi suala hili la katiba," anasema Lipumba
Lipumba ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa TCD, anasema, "Katiba mpya ni dira ya maendeleo na uchumi, mwaka 2001 tulifanya maandamano kudai Tume huru ya Uchaguzi na katiba mpya jambo ambalo lilisababisha watu kupoteza maisha,".
Anasema kuwa nchi ya Kenya imepata Katiba mpya kwa njia ambazo hazikuwa nzuri na kutoa angalizo kuwa nchini Tanzania mchakato wa katiba mpya unatakiwa kufanyika haraka ili isije kutokea kama yaliyotokea nchini Kenya.

Mkurugenzi wa utetezi na maboresho ya sheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia anasema kuwa katiba ya mwaka 1977 na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 zinakinzana kwa kuwa makamu wa kwanza na wa pili wa rais wa Zanzibar hawatambuliki katika katiba ya mwaka 1977.

"Mwaka 1964 kulikuwa na muungano wa Tanganyika na Zanzibar lakini watu hawakuulizwa kama walikuwa tayari kwa ajili ya muungano huo,"anasema na kuongeza,

"Uundwaji wa sheria unatakiwa ujumuishe watu wa rika zote, Katiba ya sasa haiweki bayana mahusiano ya mwananchi na dola,".

Anabainisha kuwa zipo changamoto nyingi kuhusu katiba inayotumika sasa na kuhoji kuwa mmiliki wa katiba hiyo ni nani?, je ni serikali au wananchi?,

Anasema kuwa vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi inaonyesha wazi kuwa wananchi hao hawana imani na dola.

Mwenyekiti wa Chama cha (UDP), John Cheyo ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki anasema kuwa nchi ya Kenya, Malawi na Afrika Kusini zimefanikiwa kubadili katiba zao na kuhoji iweje suala hilo lisifanikiwe nchini Tanzania.

"Suala la Katiba wananchi nao wanapaswa kushirikishwa, hapa tusijali gharama bali tutizame hii katiba,hivi ikiendelea kuwa hivi mwisho wake itakuwa ni nini?,"

Anaongeza, "Ndio…,kuna mambo ya msingi sana ambayo tunayakosa, mfano ni wagombea urais kuwa na viti maalum ‘special seat' ndani ya bunge, umefikiwa wakati wa mabadiliko, tudai katiba, huu si muda wa kuogopa, katiba mpya ni kwa ajili ya watanzania,".

Mwenyekiti wa Chama cha Tadea, John Chipaka anasema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinatakiwa kutambua kuwa Katiba mpya ni kwa maslahi ya watanzania na kusisitiza kuwa Tanzania sio nchi ya kifalme.

"Katiba hata haieleweki ipo kwa maslahi ya nani, hiki ni kilio cha muda mrefu sasa umefikia wakati wa kukaa na kuona jinsi ya kuwa na katiba mpya yenye misingi ya kidemokrasia," anasema Chipaka.

Mwenyekiti wa Chama cha APPT-Maendeleo, Peter Mziray ambaye pia aligombea urais katika uchaguzi mkuu 2010, anasema mchakato wa kudai katiba uanze mara moja kwa kukusanya majina ya watanzania wote wanaohitaji katiba mpya.

"Sheria tulizonazo hazikidhi, iweje rais achaguliwe na watu milioni 5 wakati nchi ina watu milioni 43 huku wapiga kura wakiwa milioni 19,",

Anaongeza, "Iweje rais achaguliwe na watu wachache harafu uongozi wote wa serikali yake aupeleke kwa watu wa chama chake,".

Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Emmanuel Makaidi anasema kuwa suala la Katiba mpya sio ombi na kuhoji iweje wazanzibar waamue kujitenga lakini hawakamatwi kwa uhaini?.

"Umefikia wakati wa kukaa na kuamua hili suala la katiba, Hawa Zanzibar waachwe waende zao kwa kuwa katiba yao na yetu zinakinzana, sasa huo ni muungano gani, ndio maana wameamua kwenda zao,"anasema Makaidi.

Makaidi anatoa angalizo kuwa CCM ina vibaraka ndani ya vyama vingine vya siasa ndio maana ukifika wakati wa mchakato wa kudai katiba mpya suala hilo huzimika taratibu.

"Nawaelezeni……, tena hili liko wazi, matokeo ya uchaguzi yatazidi kuchakachuliwa kama CCM ikiendelea kuwa madarakani na pia kama tutaendelea kutumia sheria, kanuni na taratibu hizi hizi tunazozitumia sasa,"anasema Makaidi.

Mwenyekiti wa Chama cha UPDP, Fahm Dovutwa ambaye alijiengua kugombea urais dakika za mwisho na kutangaza kumuunga mkono mgombea urais wa CCM,alikuwa na mawazo tofauti kuhusu suala la Katiba mpya, anasema tatizo sio serikali bali ni vyama vya siasa hususan kambi ya upinzani.

"Sio kama CCM haiko tayari kwa mchakato wa katiba mpya bali hakuna wadaiji wa katiba, hii ni ajabu………, kama kweli tulikuwa tunataka katiba mpya basi tangu 1995 tungesusia kushiriki uchaguzi,"anasema Dovutwa, hoja ambayo ilipingwa na washiriki wengi wanaosema kuwa kudai katiba mpya na kutoshiriki uchaguzi ni vitu viwili tofauti.

Dovutwa ambaye katika kamepeni zake aliahidi kujenga kiwanda cha silaha anasema Katiba inatakiwa kudaiwa katika misingi ya amani huku akiwashutumu baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kuwa si wakweli.


Mwakilishi wa CCM katika mkutano huo, Glorious Luoga ambaye kitaaluma ni mwanasheria anasema, "Naona hapa CCM kama ndio inabebeshwa lawama, na inaonekana hivyo kwa kuwa ipo madarakani,"


‘Si kweli hata kidogo……, CCM inaona umuhimu wa kuwa na katiba mpya sema wadaiji wa katiba wanaweka chumvi sana katika hoja zao wanazozitoa juu ya katiba ya sasa,".

Anasema kuwa si ajabu katiba kuwa na viraka kwa kuwa hata katiba ya nchini Marekani kwa muda wa zaidi ya miaka 200 imefanyiwa marekebisho mara 14.

"CCM haina hati miliki ya Tanzania, wenye hati miliki ya Tanzania ni wananchi, tatizo letu ni sisi wanasiasa hatutaki kufauata njia za msingi kudai katiba, Waziri wa Katiba na sheria suala hili la kudai katiba mpya halijafika mezani kwake sasa tunalalamika nini, je kafikishiwa kashindwa kulitatua?,"anahoji,

Anaongeza, "Ndio maana katika mkutano huu wanachama wa CCM tuko sita, lengo ni kupata maoni ya kuyapeleka makao makuu, iweje tugombee fito wakati tunajenga nyumba moja, tuweke mapendekezo yetu tuyapeleke Wizara husika huko wakishindwa ndio tuanze kuzungumza kuanzia hapo,".


Katika mkutano huo Msajili wa vyama vya siasa, John Tendwa aliungana na waliounga mkono uundwa wa katiba mpya ambapo anasema katiba mpya inatakiwa kabla mambo hayajaharibika na kupendekeza kuwepo kwa mkutano wa kitaifa wa kikatiba utakaojumuisha watu wa kada mbalimbali.


"Hata kama tuko katika taasisi za serikali, lazima tueleze ukweli. Mnaona wenyewe jinsi Bunge lilivyo na kigugumizi cha kuundwa kwa katiba mpya," anasema Tendwa.

Anaongeza, "Katiba ni kama moyo; hata sisi binadamu moyo ukiwa na tatizo ni lazima uende hospitali kwa ajili ya kupata tiba. Kwa hiyo hii katiba inayotumika sasa nayo ni lazima itazamwe upya,".

Anasema kuwa katika nchi nyingine katiba zimeshutumiwa kwa kuwa na viraka vingi vinavyowekwa kila mwaka na ambavyo mara nyingi huungwa mkono na kupitishwa na chama chenye wabunge wengi ndani ya Bunge.

"Jambo kubwa linalolalamikiwa na wadau wengi ni mamlaka ya rais. "Niruhusu... niseme nukuu ya mwanafalsafa mmoja Sir William Blackstone ambaye kwa kuangalia mamlaka ya mfalme wa Uingereza mwaka 1765 alisema 'The King can do no wrong is a necessary and fundamental principle of the English Constitution(mfalme hawezi kufanya makosa ndio msingi mkuu wa katiba ya Uingereza)'. Ukibadili neno King na Rais... basi kwa hali hiyo utaona mantiki ya kilio cha wapinzani," anasema.

Washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa utatolewa muongozo utakaoeleza mapungufu ya katiba inayotumika sasa na aina ya katiba mpya inayotakiwa na Watanzania.

Pia walikubaliana kuitisha mkutano mkubwa utakaojumuisha asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama vya wafanyakazi na wakulima pamoja na wananchi kwa ajili ya kujadili muongozo huo pamoja na kupeleka maazimio ya yaliyojadiliwa katika mkutano huo serikalini.
 
Werema ametoa mtazamo wake binafsi,no under his capacity,tueshimu mawazo ya watu wengine!!
 
Hivi Mwansheria huyu anatoka wapi? Inawezekana huko anakotoka mambo ya ugomvi ni ya kawaida. Huenda nafasi hiyo ilihitaji mtu tofauti.
 
Werema kumpinga Pinda ni utovu wa nidhamu Tuesday, 28 December 2010 20:32

werema.jpg
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema

Mpasuko uliomo katika Serikali ya Rais Kikwete juzi ulidhihirika wazi wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema aliposema kuwa hakuna uwezekano wa kuwa na katiba mpya, isipokuwa katiba iliyopo itafanyiwa marekebisho katika baadhi ya vipengele. Kauli hiyo aliitoa Ikulu, Dar es Salaam juzi, mara baada ya Rais Kikwete kumwapisha Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa suala la kubadilisha ibara zinazoonekana kutokidhi haja na kuingiza mambo mapya kwenye katiba linakubalika, lakini suala la kuandika katiba mpya hapana. Alisema kinachohitajika sasa hivi ni kupata michango mingi ya mawazo ya wananchi kuliko kupoteza muda kwa kile alichokiita kuzungumza kama bata kila kukicha.

Jaji Werema alitaka kujua ‘upya' wa katiba unaotakiwa ni upi, na kuongeza kuwa sio sahihi kusema Watanzania wanataka katiba mpya wakati kauli za madai hayo zinatoka Dar es Salaam tu. Alisema sio lazima kila mtu anachokisema kifuatwe na akatoa mfano kuwa kule anakotoka, wafugaji watataka mambo ya ng'ombe yaingizwe kwenye katiba na Wahaya nao wanaweza kusema ndizi nazo ziingizwe kwenye katiba.

Huo ndio msimamo na mtazamo wa mtu mwenye dhima na wajibu wa kuishauri Serikali kuhusu masuala ya sheria na katiba ambaye haoni umuhimu wa kuwapo katiba mpya katika wakati na mazingira tuliomo hivi sasa. Ni msimamo wa mtu aliyelewa madaraka na asiyejua mipaka ya madaraka yake wala uzito wa kauli yake pale anaposema waziwazi kwamba "suala la katiba mpya hapana, lakini kuiweka viraka ile iliyopo ni ruksa". Ni kauli nzito, ya kitemi na kidikteta ambayo hata Rais Kikwete ambaye ni kiongozi wa nchi hawezi kuitoa katika mazingira yaliyopo hivi sasa hata kama naye angekuwa na msimamo kama wa mteule wake huyo.

Ni msimamo hasi unaotolewa baada ya bosi wake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutoa msimamo tofauti Desemba 7, 2010 alipowaambia wahariri wa vyombo vya habari kuwa alikuwa haoni tatizo lolote katika kukaa na kuliangalia suala la kuwapo katiba mpya katika nchi yetu na akaongeza kuwa angemshauri Rais ili uwekwe utaratibu wa kuliangalia suala hilo. Alisema kuwa anadhani njia bora ni kuhusisha watu wengi kadri inavyowezekana, na ikibidi suala hilo lipelekwe kwa wananchi.

Kauli ya Waziri Mkuu Pinda imejaa busara na unyenyekevu anaposema atamshauri Rais. Somo analowapa viongozi wa Serikali, akiwamo Jaji Werema, ni kuwa yeye hana kauli ya mwisho na anatambua kuwa juu yake iko mamlaka kubwa zaidi ambayo ni Rais Kikwete. Hivyo, Jaji Werema anapokurupuka na kutangaza kuwa katiba mpya hapana anakuwa ni mtovu wa nidhamu, kwa sababu ameitoa wakati bosi wake tayari ametoa msimamo tofauti na bahati mbaya Rais Kikwete hajatoa msimamo wowote kuhusu suala hilo.

Ni utovu wa nidhamu uliopindukia, hasa tukitilia maanani kwamba tayari viongozi kadhaa wa nchi, wakiwamo Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Warioba na Frederick Sumaye na Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani nao wameshauri iandaliwe katiba mpya. Kwa vigezo vyovyote vile, Jaji Werema kwa elimu na uzoefu wake wa uongozi ni mithili ya kichuguu mbele ya viongozi hao ambao wako juu kama Mlima Kilimanjaro.

Inatia simanzi kuona pia kuwa hata baada ya viongozi wa kidini, vyama vya siasa, wanaharakati, vyama vya wafanyakazi , Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na wananchi kwa ujumla kutaka katiba mpya, bado anajitokeza mtu na kutoa kauli zenye kuchochea hasira za wananchi ambao wanadai katiba mpya ambayo italinda umoja na mshikamano wetu na kutuepusha na uwezekano wa kutokea machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika siku za usoni. Sisi tunasema Jaji Werema ni mtovu wa nidhamu, awajibishwe.

I thought we have always been crying for CHECK AND BALANCE in our system...........
 
Werema ametoa mtazamo wake binafsi,no under his capacity,tueshimu mawazo ya watu wengine!!

Akiwa pale kwenye viwanja vya Ikulu, aliingia kama Mwanasheria mkuu wa serikali, hawezi kutoa maoni binafsi akiwa kwenye shughuli za serikali. Waandishi wangeenda kumuuliza hayo nyumbani kwake, akiwa likizo au kama wangemkuta baa anapata kinywaji kidogo tungefikiria ni maoni yake binafsi.
Leo hii Rais Kikwete hawezi kutoa maoni kwa wanahabari alafu kesho yake akasema yale yalikuwa maoni yake binafsi, siyo ya Rais
 
hivi jamani watanzania wenzangu suala la katiba mpya hadi wao waamue? sisi si ndo tumewaajiri sasa cha kushangaza sisi wananchi ndio tunawatetemekea na kusubiri wao wakubali suala la katiba mpya,mr naona waazi kabisa huyu anaejiita mtoto wa mkulima hawezi amua lolote hadi amsikilize mkulu wa nchi anasema nini.
 
Back
Top Bottom