Wenyeji wa Kagera muone uyu Babu.

Gsana

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
4,383
1,321
Kutokana na babu wa Loliondo kuwa mashuhuri katika dawa aliyoiota,nimeanza kuamini kuwa miti shamba hutibu. Ktk mkoa wa kagera,wilaya ya Muleba karibu na Rubya kuna mzee mmoja ambaye baada ya kupata habari za Babu wa Loliondo,nimeanza kuona ukweli uliopo ktk maono. Pia Babu anatibu kwa vikombe viwili vya dawa,ila kilichonifanya nimuamini zaidi ni kuona yeye hatozi hata senti na hataki umshukuru kwa kupona kwa kuwa anafanya kazi kufuatana na ndoto. Cha ajabu watu wamefurika siku zote na wanapona. Mwaka jana mwezi wa 9 mdogo wangu ambaye ni mwanafunzi wa SAUT aliumwa sana baadae akaelekezwa huko,baba mzazi alimpeleka na mdogo wangu akapata glass ya kwanza,mganga akamwambia arudi baada ya wiki ili apatiwe tiba ya figo,bahati mbaya alikuwa anawahi mtihani chuo hakuweza kurudi pia alishapata nafuu ya tatizo lake, mdogo wangu baada ya kurudi chuo kaenda Bugando kupima kuhakiki ukweli na ajabu kafanyiwa vipimo na kugundua figo la kushoto lina matatizo. Mi nashindwa kuelewa mtu ambaye hatumii mashine yoyote,hatumii dawa yoyote ila akimuona mgonjwa anamueleza matatizo yake yote! Nlikuwa ktk mpango wa kutega kazini ili nkapate tiba ya ulcers ila sasa napata ugumu nielekee kagera au Lolindo!niko njia panda. Imani yangu ni kuwa kama mtu ahitaji hata shilingi au hata 500,kwa nini nishindwe kwenda? Najiandaa niende,na kama mtu yupo kagera namshauri aende muleba kijiji cha Nshambya ukitokea kishanda,buganguzi au Rubya seminary unafika kirahisi. Kwa kuwa niko Dar,naona Loliondo ndo karibu,plz foleni ikipungua tuambizane niweze kuunga foleni nyingne. All the best.
 
Back
Top Bottom