Wenje na Highness wabunge CHADEMA MWANZA, msiidhalilishe CHADEMA

Kabla hujaandika umejiuliza vizuri kwamba kwa nini barabara hizo ni za vumbi toka tupate Uhuru? Kwa miaka mingapi barabara hizo hazikuangaliwa na haikuwa hoja isipokuwa walipoingia Chadema ndio zinatazamwa na kuwa sababu ya uwakilishi mbaya wa Wabunge hawa?.

Barabara zote hutegenezwa kutokana na mipango ya miji ama toka mfuko wa serikali za mitaa ama serikali kuu hatuna mfumo wa madaraka mikoanikusema kwamba mbunge anawajibika moja kwa moja. Kama barabara hizo zipo chini ya manispaa ya jiji nadhani hoja hii ungeipeleka kwa wahusika yawezekana kuwa uzembe uko huko ama serikali kuu.. Labda ungefuatilia hansard za bunge na kutazama uwakilishi wa wabunge hawa kuhusiana na barabara hizo kama wamewakilisha..

Jiji la Mwanza, ni mali ya CDM. Kwa swali lako la barabara hizo toka uhuru, ndo maana wananchi wamechagua vyama mbadala ili kuwapima usimamizi wao wa miradi ya maendeleo. Kama CCM walilala, hatutaki CDM walale. Tunahitaji kuwathibitishia wananchi uthubutu wa wadau wa CDM na kuwathibitishia kuwa CDM haifanyi kazi kwa mazoea, wana namna mpya ya kuhakikisha rasilimali zinatumika kwa manufaa ya wananchi
 
Ni vigumu kuwalaumu wabunge, lakini si busara pia kuwatetea. Kitu cha msingi hapa ni kujua pesa zinazokusanywa kutoka vyanzo vya ndani na zile zinazo top -up toka kwa wafadhili au serikali kuu ni kiasi gani na zinatumikaje. Ninavyojua mimi nchi hii yote si MZA pekee inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo haziwezi kutatuliwa kwa bageti ya mwaka mmoja. Yamkini jiji linavipaumbele vingine nje ya barabara vilivyoelekezewa rasilimali chache zilizopo.
 
siyo rahisi kwa kila mwananchi kwenda council kusikiliza vikao vya madiwani, lakini ni wajibu wa mbunge kurudi kwa wananchi na kutoa ufafanuzi wa masuala yaliyozungumziwa council. Barabara ni mbovu, yeye katulia, si wananchi watajitafutia majibu?

Juzi maeneo ya Kiloreli kwa msuka, wananchi walikerwa na hali ya barabara, waendesha pikipiki wakaamua kuziba eneo lililokuwa korofi, walipofanikiwa, wakataka kila gari linalopita pale wachangie japo 500/=. Watu waovu wakapiga simu polisi-Ilemela, Polisi walikuja na kuwatimua wale wananzengo.

Mbunge yeye katulia tu. Ataikost CDM huyu, nasema haya kwa uchungu na kwa kuwa sina njia nyingine ya kumfikia

sasa wewe unataka aje afanye mkutano na wananchi bila kibali? Wakiomba kibali wananyimwa kisingizio al shabaab.ongea na polisiccm watoe vibali vwa political gatherings.
 
Mtamaholo,

Nakubaliananawe kuwa kuna haja ya wabunge wa CDM kuwa tofauti na vilea vitambi vya CCM. Barabara unazoongelea ziko hasa jimbo la Ilemela kwa mh. Hyness.
Kwa kifupi barabara ya Kilimahewa Nyasaka imeshapata fedha za ujenzi wa lami probably itaanza mwakani. Kuhusu kuharibika kwa barabara hizo na kutorekebishwa ni kwa sababu mvua zinanyesha kwa wingi sana Mza na barabara za vumbi ukizitengeza kwenye mvua ni kama unatwanga maji kwenye kinu. Utaparua mvua itakuja kiharibu fasta. Hicho ni kizuizi kinachokwamisha uparuaji wa hizo barabara.
 
Ulikwishawahi kuhudhuria vikao vya halmashauri na hukuona wabunge hawa wakikemea?Au unadhani ni mpakawaende kwenye vyombo vya habari au bungeni!Fanya utafiti kwanza ndipo uje na kauli kama hizo,pia suala la mtu kuhama ni la mtu binafsi ili mradi anaishi jimboni kwake,au ulitaka akae unapopataka wewe?

Kuna watu huwaza kwa kutumia macameroon,yaani kila akiona kitu kibovu basi mbunge aseme hovyo tu ni kweli huwa wanapiga sana kelele hao jamaa kwenye vikao!!BINADAMU BWANA HAWA WABUNGE WAKIITA WANANCHI WAONGEE NAO OOOOOH WAMEANDAMANA SASA WAFANYEJE JAMANI MBONA MKO KAMA M*****KILA UPANDE INALALA!!!
 
wenze alishahama mwanza,amemwamisha mke wake anasimamia duka la madawa dar ni kama masha tu,mi nashauri mkuu wa mkoa dar wafukuze dar wabunge wetu mkosamali,kafulila na wale wa ccn karibu wote wapo dar
 
Nadhani mtoa hoja ana pointi ingawa ameitoa kwa kulalamika na si kushauri moja kwa moja, Wenje na Highness pokeeni huu ushauri positively.
 
mtamaholo,

nakubaliananawe kuwa kuna haja ya wabunge wa cdm kuwa tofauti na vilea vitambi vya ccm. Barabara unazoongelea ziko hasa jimbo la ilemela kwa mh. Hyness.
Kwa kifupi barabara ya kilimahewa nyasaka imeshapata fedha za ujenzi wa lami probably itaanza mwakani. Kuhusu kuharibika kwa barabara hizo na kutorekebishwa ni kwa sababu mvua zinanyesha kwa wingi sana mza na barabara za vumbi ukizitengeza kwenye mvua ni kama unatwanga maji kwenye kinu. Utaparua mvua itakuja kiharibu fasta. Hicho ni kizuizi kinachokwamisha uparuaji wa hizo barabara.

nimkuelewa mkuu, pamoja sana. Kupeana taarifa siyo mie nayefika mtandaano, hata wananzengo, ni jambo la faraja siyo kuuchuna tu
 
sasa wewe unataka aje afanye mkutano na wananchi bila kibali? Wakiomba kibali wananyimwa kisingizio al shabaab.ongea na polisiccm watoe vibali vwa political gatherings.

kuna njia kibao za kufikisha ujumbe kwa wananchi, tunahitaji wabunge cdm wawe wabunufu. Mfano, hapa mwanza kuna redio kibao ambazo akienda kuwaomba kipindi/kununua kipindi hawatokataa, kitakachofanyika ni kupita na gari la matangazo kila kona ya jiji kuwatangazia kuwa kuna kipindi m,aalumu, wafungue redio zao station fulani, na wataruhusiwa kuuliza maswali.

Anaweza Kuwafikia wananchi wengi na klisingizio cha alshaababu kitaep[ukwa. Ni ubunifu tu
 
wenze alishahama mwanza,amemwamisha mke wake anasimamia duka la madawa dar ni kama masha tu,mi nashauri mkuu wa mkoa dar wafukuze dar wabunge wetu mkosamali,kafulila na wale wa ccn karibu wote wapo dar

nalo neno. Ukiwauliza watakwambia ili washiriki mbio za kitaifa kujenga chama. Kwani midege siku hizi hakuna mpaka un'gang'ania mbali na wapiga kura wako? Waache kuwaiga ccm
 
ni vigumu kuwalaumu wabunge, lakini si busara pia kuwatetea. Kitu cha msingi hapa ni kujua pesa zinazokusanywa kutoka vyanzo vya ndani na zile zinazo top -up toka kwa wafadhili au serikali kuu ni kiasi gani na zinatumikaje. Ninavyojua mimi nchi hii yote si mza pekee inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo haziwezi kutatuliwa kwa bageti ya mwaka mmoja. Yamkini jiji linavipaumbele vingine nje ya barabara vilivyoelekezewa rasilimali chache zilizopo.

ni sahihi rose, ndo kuna umhimu wa wananchi kueleezwa, na kupewa mikakati siyo kuuchuna tu bwana
 
Back
Top Bottom