nyangasese
Senior Member
- Aug 21, 2011
- 129
- 22
Inapofika hapo ndipo ninapojua umakini wa viongozi wa juu wa chadema.kitendo cha kumuengua matata mapema ktk kinyang'anyiro cha umeya mara baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 mlitumia busara ya hali ya juu, jambo ambalo limemfanya aichukie cdm mpaka leo.kwa nini nasema kilikuwa ni kitendo cha busara kumuengua ktk kuwania umeya;kwanza,ni muda mfupi sana aliokua nao tangu aamie kutoka ccm baada ya kushindwa ktk kura za maoni ndani ya ccm.haikua rahisi kwa mtu ambaye hajakitumikia chama kupewa wadhifa mkubwa wa umeya.Hii inadhihilisha kuwa alikuwa na uchu wa madaraka.pili ni kuhusu mwenendo na tabia yake.kwa ujumla huyu mtu ana sifa mbaya na ya kutisha ktk mji huu wa mwanza.we fika mwanza taja jina matata utaambiwa historia yake utaziba kinywa kwa mshangao.mimi mwanzoni nilishtuka kusikia huyu bwana ni miongoni mwa madiwani ktk jiji.kwa hili uongozi wa cdm mwanza mlionesha udhaifu mkubwa sana kumpitisha huyu,mnatakiwa muachie ngazi.Tatu, matata na chagulani walianza mapema kampeni za umeya mara baada ya uchaguzi kabla hata majina yao kupendekezwa kugombea hali iliopelekea majina yao kuenguliwa matokeo yake wameamua kuendekeza chuki binafsi kwa makamanda wetu kama wanavyofanya wahanga wa uchaguzi wa BAVICHA.