Wengi hutendwa na , si hiyari yao

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Oct 28, 2012
18,620
20,955
Najua unaweza kushtuka baada yakusoma kichwa cha habari,lakini huo ndiyo ukweli wa mambo yanayoendelea kwenye ulimwenguwa giza,kuna mengi ya kutisha na kusikitisha yanafanyika ungana nami nikuelezee tukio nililolishuhudia katika kijiji cha Njungwa mkoani Morogoro.

Ilikuwa ni siku ya pili tangu nifike hapo kijijini kumuona babu yangu Mzee Kilunda,ni Jumapili jioni baada ya kutoka msituni kuelekezwa miti na dawa mbalimbali mzee aliamua kupitia kilabuni kupiga story na wazee wenzie,nami nikajumuika nao kwenye kikao hicho kuweza kupata faida yoyote kutoka kwa wazee hao wa kijiji.

Tukiwa hapo kilabuni huku wazee wale wakiendelea kunywa pombe inayotengenezwa kwa mahindi mara akapita kijana wa kiume ambaye kwa makadirio yangu ni kati ya miaka20-25 lakini kijana huyu muonekano wake alionekana ni shoga(anafanywa kinyume na maumbile).

Cha ajabu ambacho kilinishangaza kuna mzee mmoja ambaye anaonekana pombe zishaanza kumkolea alipomuona yule kijana alitamka kuwaambia wenzie''Mimi ndiyo kiboko yenu mmemuona nilivyomfanya rogat! yeye si alikuwa anajifanya kidume nilishamkataza sana kutembea na binti yangu akaleta dharau sasa analalwa yeye,ngoja nimtie adabu kama mwaka1 halafu ntamfungilia mshenzi yule''

Nikajikuta nimeuliza kwa sauti kubwa ya mshangao''ina maana huyu kijana zamani alikuwa mzima na wewe ndiyo umemgeuza hivi?? mzee yule akajibu kwa sauti ya kilevi huku akicheka kwa furaha inayoonekana wazwaz usoni mwake''ndiyo huyu kijana alikuwa ananifanyia ushenz sana kila
nikimkataza asitembee na binti yangu hataki bado miezi 7 atamaliza adhabu yake na vijana wengine kijijini watajifunza''.

Nikajikuta nimekaa kimya huku nikimtazama yule kijana kwa huruma maana nikaogopa hata kumuhojihoji sana mzee yule asije akachukia bure akanifanya kitu mbaya,nikawa naomba mungu Mzee wangu ainuke tuondoke kwenye kile kikao kwani jasho la kwapa lishaanza kunimwagika kwa uoga.Baada ya babu kumaliza kinywaji chake tukarejea nyumbani ambapo nilikuwa na kazi ya ziada kumsaidia kupanda milima mpaka tukafika nyumbani hoi bin taaban.

Bila kuchelewa nikamuuliza babu mimi;''hebu mzee niambie vizuri yale maneno ya yule mzee ni kweli au ndiyo story zenu tuu za kilabuni
babu;aliyosema ni kweli mjukuu wangu huku kuna mambo mazito sana'' mimi;mmmh sasa wanafanya vipi mpaka mwanaume rijali akabadilika kuwa vile mbn mm naona ajabu babu???.

babu;ni mambo tuu ya kichawi mjukuu wangu anatumika jogoo,chupi ya mtakiwa,na baadhi ya miti basi ndani ya muda mfupi yule mwanaume anabadilika na kuhitaji kuingiliwa na akiingiliwa tuu mara ya kwanza basi ndiyo dawa inakubali lkn kama atatokea mtu akamuwahi kabla ya kuingiliwa akaletwa kwangu anapona''(Yeye ni mwenyekiti wa waganga wa jadi hapo kijijini)

Baada ya kunigusia hayo machache nilikuwa na hamu ya kutaka kujua kwa undani kabisa wanavyofanya hatua kwa hatua.Nikamuomba anieleze kwa kina ndipo aliposema babu;
kwanza ni lazima ipatikane nguo ya ndani ya mwanaume anayetakiwa kufanyiwa uchawi huu,na uchawi huu mara nyingi hufanyiwa watu wanaotembea na wake za watu au mabinti za watu lakini sharti kwanza apewe onyo la kuachana nae kama atakataa ndyo uchawi huu hufanya kazi lkn kama hutompa onyo basi mizimu haikubali kisha anachukuliwa jogoo mkubwa mwekundu anayependa kupanda makuku jike na unaandaliwa mchanganyiko wa mafuta ya nyemba,unga wa miti ya faijar na hanjar na unga wa maganda ya mtomoko pamoja na unga wa uume wa mnyama punda mweusi
vyote hivi vinawekwa kwenye ungo mpya ambao haujawahikutumika.

Inachukuliwa ile nguo ya ndani inaunguzwa mpaka iwe jivu na jivu lile linachanganywa kwenye ule mchanganyiko wa kwenye ungo sasa kinachofuata mchanganyiko huu wa vitu hivi huwekwa nje ya nyumba sehemu yenye umande (Unyevunyevu unaopatikana kwenye majani nyakati za asubuhi)kuanzia jioni mpaka asubuhi ikifika asubuhi huchukuliwa unga ule na anapakwa jogoo yule kwenye njia yake ya haja kubwa na mwingine anakorogewa kwenye maji kama uji anakunywa,baada ya hapo kuna maneno yanaanza kusemwa kwa muda wa dk15(ni maneno ya lugha ya kikaguru) na akimaliza maneno hayo anasema kwa sauti kubwa ''NENDAAA'' kisha jogoo anamrusha juu akitua chini jogoo yule atakimbia mbio nyingi na majogoo wengine wakimuona tuu wataanza kumfukuzia na kumpanda kama vile ni kuku jike,wakati huohuo kule kwa kidume kinachofanyiwa uchawi ataanza kujiskia anatamani kwa nguvu zote aingiliwe na akitokea mshenzi akamuingilia kinyume na maumbile ndyo basi tena dawa inaanza kufanya kazi atakuwa anaingiliwa mpaka zitimie siku zilizotiliwa nia kwenye uchawi,au kama ndugu zakewatamuwahi kabla ya kuingiliwa anatibiwa kirahisi anapona,ukifika muda aliotiliwa nia uchawi ule humtoka na anaacha kabisa anarudi kama zamani ingawa kama mchezo umeshamuathiri anaweza akawa anaendelea kufanya uchafu huo hata baada ya uchawi kumtoka.
 
Back
Top Bottom