Tuliwacheka wahenga kwa kuwauza ndugu zetu utumwani. Mpaka sasa tunajiuliza kama kweli walikuwa na akili timamu. Sisi tumekwenda zaidi! Vizazi vijavyo, vitatushangaa sana, si kama vile tunavyowashangaa wahenga, hapana - sisi hata mifupa yetu itafukuliwa na kuchomwa moto.
Ujinga huu wa kukitanguliza chama badala ya Taifa, kutanguliza tumbo badala ya taifa, kuuza rasilimali zote, kutoa fedha ndani ya nchi na kuzichimbia ulaya, kununua shahada za wapiga kura, kupindisha ukweli, ukabila na udini, ni mambo ambayo yataonekana kinyaa na kichekesho mbele ya vizazi vijavyo.
Ni kweli wema hawajazaliwa. Viongozi wetu wanataka kuendelea kutawala, hata wale walioondolewa kwa kashfa kubwa ,bado wanataka kusafishwa ili wawe Zuma wa Tanzania. Ni mambo ya kusikitisha kabisa. Wanayaangalia matumbo yao, badala ya kuliangalia taifa letu. Tukianza kupigana, wao na familia zao watakimbilia walikoficha vijisenti vyao.
Tafakari.
Ujinga huu wa kukitanguliza chama badala ya Taifa, kutanguliza tumbo badala ya taifa, kuuza rasilimali zote, kutoa fedha ndani ya nchi na kuzichimbia ulaya, kununua shahada za wapiga kura, kupindisha ukweli, ukabila na udini, ni mambo ambayo yataonekana kinyaa na kichekesho mbele ya vizazi vijavyo.
Ni kweli wema hawajazaliwa. Viongozi wetu wanataka kuendelea kutawala, hata wale walioondolewa kwa kashfa kubwa ,bado wanataka kusafishwa ili wawe Zuma wa Tanzania. Ni mambo ya kusikitisha kabisa. Wanayaangalia matumbo yao, badala ya kuliangalia taifa letu. Tukianza kupigana, wao na familia zao watakimbilia walikoficha vijisenti vyao.
Tafakari.