Website ya IKULU na miradi ya COMPUTER ya Serikali

Sawa tuseme basi alishindwa kutengeneza hiyo website kwa sababu moja au nyingine. Wewe kama Mtanzania, huoni kuna sababu ukajitolea kutengeneza Website ya Ikulu, na itakufanya pia ujulikane zaidi ya Utanzania wako! Jitolee bwana usiwe kama hao walioshindwa kama unavyosema.
 
Sawa tuseme basi alishindwa kutengeneza hiyo website kwa sababu moja au nyingine. Wewe kama Mtanzania, huoni kuna sababu ukajitolea kutengeneza Website ya Ikulu, na itakufanya pia ujulikane zaidi ya Utanzania wako! Jitolee bwana usiwe kama hao walioshindwa kama unavyosema.


LWAMA PAPA


http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=2469&highlight=Communications+team

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=989

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=1147&highlight=Communications+team
 
Papa,

Karibu sana! Well; umejileta mwenyewe nasi twashukuru kwani nnavyoona wewe ni mjumbe mzuri wa serikali na kuna uwezekano ukasaidia katika hoja nyingi tulizokuwa tunaitupia serikali bila majibu.

Aidha nashukuru kwa namna ya kipekee ambayo umeonyesha kusema ULIZA UJIBIWE ukimaanisha wewe ni mjumbe wa kweli!

Naam; naomba unambie mimi binafsi nikiifungua tovuti ambayo ni Dynamic na kutaka kuipa serikali ikiwa ni zawadi kwa Ikulu (na sitaki kutangazwa kwa zawadi yangu) nani naweza kumpa bila kuwekewa mizengwe?

I assure you; within 14days naweza kukutengenezeeni tovuti ambayo ina quality ya kueleweka na nikawa nimelipia hosting ya mwaka mmoja.

Nasubiri jibu lako mheshimiwa
 
Halafu kwa nini mtu ajitolee wakati kuna pesa zilishatengwa kwa ajili ya kazi hiiii?

sasa budget ya hiyo communications department imefanya nini? na najua baadhi yenu manona suala hili ni dogo sana lakini kusema ukweli ni kuwa mtu kama ni head wa hii department anashindwa kuwa na uwezo wa kuwaambia watumishi wake kuwa website iwe up and running within 2 weeks sasa sielewi wanafanya nini zaidi ya kuangalia TALK SHOWS kule ofisini kwao

Rais ilitakiwa tupate podcasts zake...maana hakuna mwenye muda wa kukaandani the whole day akasikiliza hotuba za rais ..kwani mambo ya sikuhizi ni kudownload na kumove on...

Sasa kama KALLAGHE alishindwa jukumu dogo kama hili je, ataweza majukumu makubwa zaidi?
 
Na kweli Dr.WHO,

Hakuna haja ya kuwapa bure! Kwanza wameajiri watu wa fani husika; KWANINI HAWAWATUMII IPASAVYO?
 
DrWho, wamekuambia wako "Under Construction, Visit Us Soon"... kwanini wewe unaharaka? Roma haikujengwa kwa siku moja. Halafu inawezekana hawakupangiwa bajeti ya vitu kama hivyo. Unajua wakiwa na tovuti itabidi wawe na mtu anayeisimamia n.k... Serikali haina hela za kufanya hivyo kwa sasa (at least that is what I think). Hivi katika vitu muhimu vya serikali kufanya tovuti ni mojawapo? Wao watasema wanahangaikia barabara, maji, hospitali, shule n.k... wanasema "tupate vitu vya lazima kwanza, halafu ndio tutafute hivyo vya anasa"! Sasa usiniulize imekuwaje tovuti iwe ni anasa..
 
Huyo mhe. Kijazi ndo kwakeli alistahili hiyo nafasi baada ya kufanya kazi nzuri kule wizara ya Ujenzi enzi hizo! Kwamba alipokuja Mramba na Miundo mbinu yake, ya kupanga na kuongea bila kufikiri ndo akamboa, ndipo Kijazi ambaye ni Engineer akaona hapo naharibiwa unga na huyu mzee. Akamwomba Jk kuachia ngazi ndiposa Jk akampeleka Mambo ya nje kusubiri huo Ubalozi!

Kwakweli pale India palishaharibika, hasa kutokana na kauli chafu za huyo mama balozi alitukuwepo, kumbe lugha chafunile ni kwakuwa alishajua atarudi hm kustaafu!
 
YES Mwanakijiji,

Wanaodhani internet ni anasa wana-lag behind. Na ulivyojibu almost ndiyo majibu ya Mheshimiwa Lwama Papa! Lakini wajue kuitangaza nchi worldwide na hasa leo tukiwa tunaadhimisha uhuru wa vyombo vya habari ni pamoja na kutumia njia za mitandao na kuitangaza nchi kwa mazuri iliyo nayo.

Haya bana, mie nshakata tamaa!
 
Dr.WHO, hizo website hapo hata moja sio ya Serikali.Muwe munaelewa mada inayoongelewa. Nilizungumzia kama Balozi XX mteule alishindwa kuanzisha Website, na kwa kuwa unaona kuwa na Website ni kitu muhimu sana kwa maisha ya Watanzania, basi ujitolee kuanzisha moja. Wewe ukapost a series of Jambo Forums.
Afadhali mwenzio WORM aliyejitolea kujenga Website ya Serikali bure na hataki ajulikane na anataka ajue amuone nani ili afanikishe. Kwa kuwa bado thread inaendelea, na kuna wajuzi wanaotoa hoja ya kusema bwana WORM asifanye kazi ya bure ya kujitolea, basi malizeni kwanza majadiliano, mtapofikia muafaka, kama kuna haja ya kujitolea, basi nitawashauri nani wa kumouna.
 
Lwama, karibu na tunatumaini you can deliver... wOrM anaweza kuishauri serikali kuhusu hiyo tovuti lakini wakiamua kutaka atengeneze ni lazima alipwe... tumeamua kuishi kibepari, basi tuzinagatie kanuni ya kwanza ya mfumo huo...
 
Duh, Mwanakijiji!

Well, mimi nakusikiliza tu Lwama Papa. Ninachoomba ujue hapa utakumbana na mawazo tofauti. Hilo liko wazi. Unatakiwa kuwa na hekima kuchambua cha kufanyia kazi na kipi cha kuacha. Dhamira ya kuisaidia serikali ipo nadhani ndani ya kila roho ya Mtanzania MZALENDO na wengine kujitolea tuko tayari. Hata ushauri tu juu ya namna ya kuendesha masuala flani muhimu ili taifa lisonge mbele.

Hata mawazo yanayoandikwa hapa si kuiponda serikali bali kukuamsheni ili mjue wajibu wenu na wapi mmelega. Ni kweli kuwa si kila kitakachoandikwa utakipenda. Isiwe sababu ya kuingia mitini mkuu.

Back to the topic, kuwa na tovuti ni jambo la busara sana na lenye kutupandisha na kuwapa moyo watanzania walio wengi. Si kila mmoja atakupa ushauri wa kujenga pia (ukianzisha tovuti hiyo). Lakini tambua kuwa ukiona watanzania wanafikia hatua ya kuona haja ya kufanya kazi hata bure elewa kuwa wanajua umuhimu wa suala wanalolikomalia.

Ni kweli; wengi husema hakuna kazi ya bure, na kazi ya bure huchosha lakini ikithibitika kuwa serikali inakiri haina hela ya kufanya jambo hili wengine tuko tayari kukusaidieni BURE ili mradi taifa letu lipige hatua hiyo.

Ushauri BURE; Mengine ni maelewano tu lakini hata bure we can after proving kuwa kulipia ni ngumu. Tatizo la hapo Ikulu ni usumbufu wa NJOO AFTER 3 MONTHS! Hii kitu inaboa mkuu; just imagine naunguza hela zangu kuchukua taxi mimi nisiye na gari ama naunguza mafuta yangu na kuja kwa ajili ya kujitolea kazi hii lakini naambiwa SUBIRI MIEZI MITATU IJAYO NDIPO APPOINTMENT YAKO ITAFIKIA. Angalieni masuala mengine muhimu na muda kwetu wengine ni mali!

Kama ni kukuona wewe right; nadhani umeshajua kuwa kuna nini kinasababisha watu waone ugumu wa kusaidia na you can work on it!

By the way, karibu JamboForums.com... We dare to talk Openly mzee
 
Mzee Mwanakijiji, he umekuwa msemaji wa wOrM? Malizeni mjadala halafu mseme bayana msimamo kama kulipwa au bure? Ni lini mtatoa mchango nchini kwenu kama mmeamua kuishi kibepari kwa maana chochote kinachofanywa, kiwe na consideration? Hebu kumbukeni "Kijana aliyepewa chakula na Kijiji kilichokuwa na njaa, ili apate nguvu ya kwenda kutafuta chakula mbali arudi nacho kuwasaidia aliowaacha Kijijini kwake maana, wangekigawa pale Kijijini kisingewatosha na wasingefika huko kupata chakula kingine- Kijana akala akashiba akaenda na akapata hicho chakula alichikifuata, badala ya kukirudisha Kijijini kwa wengi aliowaacha na njaa akaamua kubaki huku huko". Sasa na nyie msiwe kama huyo kijana kwa kusingizia eti mmeamua kuishi Kibepari. Lazima mkumbuke mlikotoka!
 
Dr.WHO, hizo website hapo hata moja sio ya Serikali.Muwe munaelewa mada inayoongelewa. Nilizungumzia kama Balozi XX mteule alishindwa kuanzisha Website, na kwa kuwa unaona kuwa na Website ni kitu muhimu sana kwa maisha ya Watanzania, basi ujitolee kuanzisha moja. Wewe ukapost a series of Jambo Forums.
Afadhali mwenzio WORM aliyejitolea kujenga Website ya Serikali bure na hataki ajulikane na anataka ajue amuone nani ili afanikishe. Kwa kuwa bado thread inaendelea, na kuna wajuzi wanaotoa hoja ya kusema bwana WORM asifanye kazi ya bure ya kujitolea, basi malizeni kwanza majadiliano, mtapofikia muafaka, kama kuna haja ya kujitolea, basi nitawashauri nani wa kumouna.

Acha uwakala wako wa serikali.Kuna mtu analipwa fedha kwa jukumu hilo la kuhakikisha website ya Ikulu iko hai,kuna kitengo kinategengewa fedha kwa jukumu hilo,sasa unapoleta zako za kuleta kuwa "wazalendo wajitokeze kushughulikia ujenzi wa website kwa kujitolea" hayo mafungu ya fedha yalotengwa maalum kwa suala hilo yanakwenda wapi?Usitetee wazembe.
 
Hapa ndipo Watanzania mtatia akili na mjue JK alikuwa msanii na anendeleza na juweni kwa 100% kwamba Urais wake una UBIA .
 
YES Mwanakijiji,

Wanaodhani internet ni anasa wana-lag behind. Na ulivyojibu almost ndiyo majibu ya Mheshimiwa Lwama Papa! Lakini wajue kuitangaza nchi worldwide na hasa leo tukiwa tunaadhimisha uhuru wa vyombo vya habari ni pamoja na kutumia njia za mitandao na kuitangaza nchi kwa mazuri iliyo nayo.

Haya bana, mie nshakata tamaa!
Kama sababu zenyewe zakuwa na website nikujitangaza bila shaka haihitajiki. Rais wetu anakwenda mwenyewe huko huko waliko hao watumiaji wa website na kuwaaambia ana kwa ana hayo mambo ambayo yangewekwa kwenye mtandao.
 
Mzee Mwanakijiji, he umekuwa msemaji wa wOrM? Malizeni mjadala halafu mseme bayana msimamo kama kulipwa au bure? Ni lini mtatoa mchango nchini kwenu kama mmeamua kuishi kibepari kwa maana chochote kinachofanywa, kiwe na consideration? Hebu kumbukeni "Kijana aliyepewa chakula na Kijiji kilichokuwa na njaa, ili apate nguvu ya kwenda kutafuta chakula mbali arudi nacho kuwasaidia aliowaacha Kijijini kwake maana, wangekigawa pale Kijijini kisingewatosha na wasingefika huko kupata chakula kingine- Kijana akala akashiba akaenda na akapata hicho chakula alichikifuata, badala ya kukirudisha Kijijini kwa wengi aliowaacha na njaa akaamua kubaki huku huko". Sasa na nyie msiwe kama huyo kijana kwa kusingizia eti mmeamua kuishi Kibepari. Lazima mkumbuke mlikotoka!

Lwama tatizo ni kuwa.. huyo kijana kwenda kutafuta chakula zaidi huko kwingine hakutumwa na kijiji!! Hata hivyo ana hamu ya kurudi na "mikungu ya ndizi" ili kukisaidia kijiji chake. Tatizo ni kuwa, viongozi wa kijiji wameshauza mali zote za kijiji hata maghala ya kuhifadhia chakula! Na mashamba yaliyokuwa ya kijiji wamegawiana wenyewe halafu wamepangisha wageni walime!!
 
Back
Top Bottom