Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,949
- 4,444
Jana niliwahi kurudi home nikawa na angalia kipindi cha Bunge kupitia TBC kuna mbunge mmoja wa Ludewa nafikiri Mh. Mwalyosi alitaka apewe Ambulance katika jimbo lako kwani ipo moja kwa jimbo zima.
Kuna waziri mmoja wa TAMISEMI alinichefua wakati anajibu swali hilo la mbunge Mwalyosi eti serikali imetenga fedha kwa ajili ya AMBULANCE 50 nchi nzima. Duh jamani hii inaonyesha jinsi gani serikali isivyo jali afya zetu yaani nchi nzima serikali imetenga ambulance 50 tu? Huu ni utani tena na dharau kwa wananchi na walipa kodi wao wanatembelea magari ya kifahari wanashindwa hata kuwathamini wananchi kwa angalau kuwapa AMbulance za kutosha kwenye mahospital akina mama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma za haraka.
Jamani kutokana na hasira niliipasua TV yangu pale pale huu ni upuuzi sasa kodi tunalipa za nini? Kama huduma ndo kama hivyo tunapewa kwa kusua sua kuna hospital kubwa hata Ambulance hakuna wao wanabadilisha magari kila baada ya miaka 2 na wanajiuzia wenyewe kwa bei za kutupwa kwani mnafikiri hatujui haya! Si hata nyumba za serikali mmejiuzia wenyewe kwa bei za kutupwa sasa serikali inazidi kuingia hasara kwa kuwapangia nyumba.
Kuna watu hawana uchungu na nchi hii yaani machungu mpaka yananipitiliza.
Kuna waziri mmoja wa TAMISEMI alinichefua wakati anajibu swali hilo la mbunge Mwalyosi eti serikali imetenga fedha kwa ajili ya AMBULANCE 50 nchi nzima. Duh jamani hii inaonyesha jinsi gani serikali isivyo jali afya zetu yaani nchi nzima serikali imetenga ambulance 50 tu? Huu ni utani tena na dharau kwa wananchi na walipa kodi wao wanatembelea magari ya kifahari wanashindwa hata kuwathamini wananchi kwa angalau kuwapa AMbulance za kutosha kwenye mahospital akina mama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma za haraka.
Jamani kutokana na hasira niliipasua TV yangu pale pale huu ni upuuzi sasa kodi tunalipa za nini? Kama huduma ndo kama hivyo tunapewa kwa kusua sua kuna hospital kubwa hata Ambulance hakuna wao wanabadilisha magari kila baada ya miaka 2 na wanajiuzia wenyewe kwa bei za kutupwa kwani mnafikiri hatujui haya! Si hata nyumba za serikali mmejiuzia wenyewe kwa bei za kutupwa sasa serikali inazidi kuingia hasara kwa kuwapangia nyumba.
Kuna watu hawana uchungu na nchi hii yaani machungu mpaka yananipitiliza.