Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Mimi mwenyewe niliwahi kuchangia mada fulani kuna mtu akanivaa maungoni kama vile ile ishu ilikuwa ni "personal" na yeye ananijua kinagaubaga wakati hanijui hata chembe. Hadi nikamuuliza "tunaishi chumba kimoja na wewe?" kwa kweli ilinitumbukia nyongo wiki nzima sikugusa JF!! Mtu hakujui lakini anavyokushadadia kama vile ni mkeo/mumeo.Inasikitisha ehhh!!!?
Sasa fikiria hata mdada tu ambae hajiamini amini alafu apate na watu wakumchamba na kumchambua hivyo kama hatofikia kutamani mauti. Yani watu wanawanyima wenzao raha kwa madhaifu yao wenyewe.
Huyo mzee ni mzee haswa. . . ndo kama hawa wanautimia maneno, wengine wanatumia mikono yani alimradi ajisahaulishe kuhusu udhaifu wake kwa kumuonea mtu mwingine.
Kwenye hii mitandao usipokuwa mvumilivu mwisho wa siku unageuka na kuwa mtu wa ajabu ajabu!!