Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Nimekisoma Lizzy kisa cha Natasha nakuishia kushangaa hii mitandao itatupeleka wapi. Watu wazima kama mimi huwa tunajua kudili na hisia zetu, lakini huwezi kujua nyuma hizi avatar ni mtu wa aina gani.Kigarama nilikua naifikiria hii ishu mapema kweli kwasababu nilishaona kipindi kile cha msiba Regia. . .
Ila hii ya YM kwakweli imezidi. Kuna wengine hata kama sio hapa hua wanasababisha wenzao wanapoteza kabisa kujiamini, na wale wadogo wadogo wanafikia hata kujiua.
Suicide teen Natasha MacBryde was bullied online even after her death | Metro.co.uk
Mwingine anaanzisha mada ili ajifunze kutoka kwa wengine lakini mwisho wa siku anaishia kugeuzwa kituko. Natasha binti mdogo kabisa alikuwa, lakini alisongwa songwa hadi akajiu. "unajifanya wewe ni bomba na wanaume wote wanakuzimikia..." haya ni maneno ya watu dhaifu.
Mzee mmoja alinifunza kwamba watu dhaifu ni pamoja na Hittler kwani wanatumia sana mabavu kuwasilisha ujumbe wao kwa sababu hawajiamini!