Wazushi mtandaoni. . .

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,770
59,109
Ni rahisi kweli watu kuwa nyuma ya computer na kumuattack /bash a.k.a kumponda mtu mwingine kwa muonekano wake hata kama mpondaji hamjui mhusika kwa sura kwasababu tu yeye haonekani. Yani anapata confidence ya bandia ambayo uraiani hana na kushambulia wale wasiomuona/wasiomfahamu.

Je. . .hawa watu wao sura na maumbo yao binafsi yanalipa kweli hata wawezeze kuwakashifu wengine? Wakijiangalia kwenye vioo wanajifurahia?Wanajipenda?Mitaani wanaangalika mara mbili au ndio hasira za kutokua na hayo yote wanashushia kwa wenzao?
 
Lizzy Luu..

kwa maoni yangu ni kwamba kuna watu wanadhani wao ni wazuri kuliko wengine..
na wameshajiwekea picha fulani kichwani mwao kuwa mtu mzuri yuko hivi.. na hivyo
ndivyo ilivyo hiyo picha ikija vingine basi..

haya sasa
kuna wale ambao watafanya wawezalo kumuweka mtu mwingine chini ili wao wajisikie
vizuri.. Hawana ile "Self esteem" mpaka wamponde au waongee maneno fulani mabaya
kuhusu mwingine...

either way
Dunia ni jalala la maonyesho..
 
Kiukweli kabisa Lizzy sio mtandaoni tu ingawa kwenye mtandao ndio inaweza kuwa asilimia kubwa ila hata huku mtaani unasikia mtu anasema yule dada ana miguu kama spoku za baiskeli wakati yeye hajajiangalia au hajui kuwa kuna watu na yeye wanamuongelea vile vile. Ila hii ya mtandaoni imekithiri sana mfano mzuri tu ni juzi pale BC kuna jamaa alikuwa kwenye Skype akasema mbona fulani (sitaki kutaja jina lake) sura yake nzito tofauti na avatar yake kwa kweli nilijisikia vibaya ila nikaamua kupotozea tu na huyo member aliyemsema hivyo mwenzake namkumbuka vizuri...
 
Lizzy Luu..

kwa maoni yangu ni kwamba kuna watu wanadhani wao ni wazuri kuliko wengine..
na wameshajiwekea picha fulani kichwani mwao kuwa mtu mzuri yuko hivi.. na hivyo
ndivyo ilivyo hiyo picha ikija vingine basi..

haya sasa
kuna wale ambao watafanya wawezalo kumuweka mtu mwingine chini ili wao wajisikie
vizuri.. Hawana ile "Self esteem" mpaka wamponde au waongee maneno fulani mabaya
kuhusu mwingine...

either way
Dunia ni jalala la maonyesho..

Weee Kurwa unaweza ukawa unajiona ni mzuri ukahangaika kuponda wengine kweli?
 
Lizzy pole bibie najua mashambulizi dhidi ya Young Master kwenye ile siredi yamekukwaza lakini ndiyo dunia ilivyo. Nafikiri siyo kwenye sura tu hata kwenye "core issues" za kitaifa watu wanawashambulia wenzao kwa sababu tu wao hawaonekani kiuhalisia wao. Kuna watu hapa ikiwekwa sheria ya kujitambulisha kiuhalisia wote watafutika ghafla!
 
Kiukweli kabisa Lizzy sio mtandaoni tu ingawa kwenye mtandao ndio inaweza kuwa asilimia kubwa ila hata huku mtaani unasikia mtu anasema yule dada ana miguu kama spoku za baiskeli wakati yeye hajajiangalia au hajui kuwa kuna watu na yeye wanamuongelea vile vile. Ila hii ya mtandaoni imekithiri sana mfano mzuri tu ni juzi pale BC kuna jamaa alikuwa kwenye Skype akasema mbona fulani (sitaki kutaja jina lake) sura yake nzito tofauti na avatar yake kwa kweli nilijisikia vibaya ila nikaamua kupotozea tu na huyo member aliyemsema hivyo mwenzake namkumbuka vizuri...

Loh. . watu bana!!
Hapo angeambiwa aonyeshe yake tuone kama ni laini tofauti na anaemponda basi, kama tusingeshangaa basi tungekimbia!!
 
Kiukweli kabisa Lizzy sio mtandaoni tu ingawa kwenye mtandao ndio inaweza kuwa asilimia kubwa ila hata huku mtaani unasikia mtu anasema yule dada ana miguu kama spoku za baiskeli wakati yeye hajajiangalia au hajui kuwa kuna watu na yeye wanamuongelea vile vile. Ila hii ya mtandaoni imekithiri sana mfano mzuri tu ni juzi pale BC kuna jamaa alikuwa kwenye Skype akasema mbona fulani (sitaki kutaja jina lake) sura yake nzito tofauti na avatar yake kwa kweli nilijisikia vibaya ila nikaamua kupotozea tu na huyo member aliyemsema hivyo mwenzake namkumbuka vizuri...

duhhhhhhh TF nimejaribu kucheka lakini imeniwia vigumu...
 
Sio mtandaoni, hata hadharani wapo wanaowaona wengine si chochote wakijilinganisha nao. Ila wanapopata nafasi ya kujitafakari wanajijua si lolote, hivyo kuneutralize ya moyoni kwa kinachotaka nafsi wanaishia kujikweza na kuwananga wengine
 
Lizzy pole bibie najua mashambulizi dhidi ya Young Master kwenye ile siredi yamekukwaza lakini ndiyo dunia ilivyo. Nafikiri siyo kwenye sura tu hata kwenye "core issues" za kitaifa watu wanawashambulia wenzao kwa sababu tu wao hawaonekani kiuhalisia wao. Kuna watu hapa ikiwekwa sheria ya kujitambulisha kiuhalisia wote watafutika ghafla!

Kigarama nilikua naifikiria hii ishu mapema kweli kwasababu nilishaona kipindi kile cha msiba Regia. . .
Ila hii ya YM kwakweli imezidi. Kuna wengine hata kama sio hapa hua wanasababisha wenzao wanapoteza kabisa kujiamini, na wale wadogo wadogo wanafikia hata kujiua.

http://www.metro.co.uk/news/870057-suicide-teen-natasha-macbryde-was-bullied-online-even-after-her-death
 
Loh. . watu bana!!
Hapo angeambiwa aonyeshe yake tuone kama ni laini tofauti na anaemponda basi, kama tusingeshangaa basi tungekimbia!!
Ukimwambia aweke ya kwake sasa...kuna msemo unaosema wale wanaoponda sura za wenzao mara nyingi huwa wanakuwa na inferiority complex
duhhhhhhh TF nimejaribu kucheka lakini imeniwia vigumu...
Lol...acha tu ndio mambo yalivyo mtaani mixer mtandaoni..
 
Weee Kurwa unaweza ukawa unajiona ni mzuri ukahangaika kuponda wengine kweli?

Doto ,
Kumbuka kuna watu ambao hawaridhiki na walicho nacho ..
waweza kuwa wazuri wa kila kitu nje "mwili" lakini bado something is missing
kwa hiyo kwa wao kujisikia vizuri ni kupoteza muda wao kuponda au kutosifia
wengine ili nafsi zao ziridhike... Shame on them ...
 
Kigarama nilikua naifikiria hii ishu mapema kweli kwasababu nilishaona kipindi kile cha msiba Regia. . .
Ila hii ya YM kwakweli imezidi. Kuna wengine hata kama sio hapa hua wanasababisha wenzao wanapoteza kabisa kujiamini, na wale wadogo wadogo wanafikia hata kujiua.

http://www.metro.co.uk/news/870057-suicide-teen-natasha-macbryde-was-bullied-online-even-after-her-death
Lizzy huku duniani kuna watu kazi yao ni moja tu, kujikweza wao na kuwashusha wenzao! Yaani mtu anahakikisha kila unachofanya/sema anakikosoa tena sio kwa lengo la kukusaidia ila kwa lengo la kukufanya uache kujiamini... Kwenye uzi wa YM hilo pia limejitokeza na asipoangalia anaweza akajishusha thamani na kuanza kujichukia, sijajua wametumia vigezo gani kukosoa ile picha yake manake kiukweli vile ndivo ambavyo Mungu amemuumba!... Kabla hatujamua kuwashambulia wenzetu mara sijui ana sura mbaya, miguu mibaya, anaenda kama anarudi hebu na tujitizame je unayeshambulia mwenzako wewe u mkamilifu kiasi hicho?
 
Sio mtandaoni, hata hadharani wapo wanaowaona wengine si chochote wakijilinganisha nao. Ila wanapopata nafasi ya kujitafakari wanajijua si lolote, hivyo kuneutralize ya moyoni kwa kinachotaka nafsi wanaishia kujikweza na kuwananga wengine
Mbaya sana, badala ya kuangalia mapungufu yao watafute namna ya kuyarekebisha ama kujipendezesha kama inawezekana wanakomaa na watu wengine.


Uzuri na urembo upo ndani kwa nje mnajiongopea-FidQ
Uzuri upo ndani na nje. . . wanaochagua mmoja ndio wanaojiongopea.

Ukimwambia aweke ya kwake sasa...kuna msemo unaosema wale wanaoponda sura za wenzao mara nyingi huwa wanakuwa na inferiority complex

Lol...acha tu ndio mambo yalivyo mtaani mixer mtandaoni..

Kaaaazi kweli kweli!!!
 
Lizzy huku duniani kuna watu kazi yao ni moja tu, kujikweza wao na kuwashusha wenzao! Yaani mtu anahakikisha kila unachofanya/sema anakikosoa tena sio kwa lengo la kukusaidia ila kwa lengo la kukufanya uache kujiamini... Kwenye uzi wa YM hilo pia limejitokeza na asipoangalia anaweza akajishusha thamani na kuanza kujichukia, sijajua wametumia vigezo gani kukosoa ile picha yake manake kiukweli vile ndivo ambavyo Mungu amemuumba!... Kabla hatujamua kuwashambulia wenzetu mara sijui ana sura mbaya, miguu mibaya, anaenda kama anarudi hebu na tujitizame je unayeshambulia mwenzako wewe u mkamilifu kiasi hicho?

Yaani wamenishambulia hadi nimekosa raha! Hii dunia tabu tupu
 
Doto ,
Kumbuka kuna watu ambao hawaridhiki na walicho nacho ..
waweza kuwa wazuri wa kila kitu nje "mwili" lakini bado something is missing
kwa hiyo kwa wao kujisikia vizuri ni kupoteza muda wao kuponda au kutosifia
wengine ili nafsi zao ziridhike... Shame on them ...
Shame on them indeed. . .
Wanahitaji somo la kujiamini!!
 
prrrrrrrr!!hawana lolote hao lizzy,...sura zao kama avatar za watu fulani humu...nitonye, mphamvu na wengine wafananao na hao....
wangekua km preta cjui ingekuwaje!?!loh!!
 
Lizzy huku duniani kuna watu kazi yao ni moja tu, kujikweza wao na kuwashusha wenzao! Yaani mtu anahakikisha kila unachofanya/sema anakikosoa tena sio kwa lengo la kukusaidia ila kwa lengo la kukufanya uache kujiamini... Kwenye uzi wa YM hilo pia limejitokeza na asipoangalia anaweza akajishusha thamani na kuanza kujichukia, sijajua wametumia vigezo gani kukosoa ile picha yake manake kiukweli vile ndivo ambavyo Mungu amemuumba!... Kabla hatujamua kuwashambulia wenzetu mara sijui ana sura mbaya, miguu mibaya, anaenda kama anarudi hebu na tujitizame je unayeshambulia mwenzako wewe u mkamilifu kiasi hicho?

Kweli ubinadamu kazi!!
 
Back
Top Bottom