Not_Yet_Uhuru
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 1,304
- 431
Wadau na wapenda mabadiliko ya kifikra, kisiasa na kijamii!
Ni Wazo muafaka sana kwa sasa CHADEMA kuanzisha vyombo vyake rasmi vya Habari ikiwa ni pamoja na TV, Radio na Magazeti. Wazo hili limekuwa hamasa sana na linaungwa mkono na kila watu 8 kati ya 10 unaokutana nao na kuwauliza umuhimu wa CDM kuwa na chombo chake rasmi cha habari kinachoweza kuwafikia wananchi kwa asilimia kubwa popote Tanzania. Wengi wanasema CDM inasubiri nini? Au hadi Mafisadi wapeleke muswada kuondoa uhuru wa Vyama vya Siasa kumiliki vyombo vyao vya habari? Chama cha Mafisadi kimejiwekea mbinu zao za propaganda ikiwapo Radio-feki, magazeti-ya kufungia vitumbua nk....lakini wameishia kuchakachua haki za umma na kufisadi hata kujichakachua kwa siasa na kura za wao kwa wao! Sasa wanaelekea kule Baba wa Taifa alipokwishawatabiria!
Wadau, katika kulikomboa taifa, lazima tukubaliane kuwa gharama, kutoka jasho na kujitolea ni sehemu ya ukombozi, hasa kwa nchi ambayo imedhoofishwa na mafisadi kama taifa la Tanzania. CDM inayo nguvu ya umma na hakuna woga hata chembe ktk kuijengea umma ukurasa na jukwaa jipya la habari sahihi na siasa sahihi kwa ukombozi wa umma!!
Ili ukombozi uwafikie wananchi wote na waelewe kwa nini wao ni masikini kwa Miaka zaidi ya 50 toka wapate uhuru, na kwanini wamebaki dhaifu na kwa nini wanahitaji haraka kujenga fikra sahihi, na ni kwanini wachague siasa sahihi (waachane na maji-taka) na wapate maendeleo ya kijamii, suala la HABARI NI NGUVU KAMILIFU. "Information is Power" na hakuna wa kuibadili kauli na ukweli huo.
Maisha ya taifa hili kwa jinsi yaliyotokomea mifukoni mwa wajanja na mafisadi wachache, ni muhimu sana wapate habari, kwa haraka, mapema na zisizokuwa na ukandamizaji, na kujengewa woga. Tukumbuke kuwa, Mifumo ya mitandao kama Internet, e-mails nk kwa sasa inawafikia wachache sana na hasa waliojikusanya mijini. Ni wananchi wachache mno wanaoweza kupata habari za kweli kupitia Radio, TV na magazeti ya binafsi yasio na mlengo wowote wa kiitikadi, na hasa masikini waliojaa vijijini, ambao ndio wamebaki kuwa chambo na kuvikwa minyororo ya mateso na kitanzi na Chama cha Mafisadi ili kujichukulia na kujinufaisha kwa hali zao na kuwaangamiza watanzania kwa kuwaibia kura na kuwajengea woga wasiweze kujitetea, wazidi kutokujiamini ili kuwaibia rasilimali zao. Mwisho ndio sasa!!
HAKIKA, Sasa ni wakati muafaka kwa CDM kutangaza mkakati rasmi wa kuanzisha Vyombo vyake rasmi vya mawasiliano ikiwapo TV, Radio na Magazeti ili kukamilisha harakati za ukombozi wa Taifa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uraia, Katiba, na siasa safi kwa ajili ya kulinusuru taifa hili linaloangamia kwa kasi. CDM itakapotoa Tamko Rasmi kuhusu Mkakati huu, nchi itatikisika kwa jinsi Wananchi kwa mamilioni toka katika Mikoa yote, Wilaya, Majimbo, Kata, Tarafa, Vijiji hadi vitongoji watakavyojitolea kwa hali na mali tayari kwa Michango, kuchangia ufanisi wa ukombozi huu kwa njia zozote zile kama wafanyavyo bila kuchoka ktk masuala ya dini, sherehe nk. Tunaomba CDM itangaze rasmi mkakati huu mapema iwezekanavyo! Wananchi wamejaa HAMASA sana, ili ndani ya 2012 hadi mwishoni mwa 2013, tuwe katika ramani halisi ya kuwapa watanzania walichokikosa miaka yote. Muda ni sasa! MUDA ULIOBAKI KUFIKA 2015 NI MFUPI SANA NA UNAENDA KWA KASI SANA!. Watanzania wanahitaji kwa haraka Habari sahihi na Siasa sahihi na uongozi sahihi kuelekea 2014, MUDA NI MFUPI SANA! Mara ifikapo 2015 kuelekea kupiga kura, Taifa linatakiwa liwe limekomaa hasa! Taifa jipya linaundwa kutokana na Wapiga Kura waliojaa elimu, fikra na Hamasa za ukombozi na maendeleo ya jamii na nchi yao!
NAOMBA KUWASILISHA, tuchanganue na tujadili, TUTOE DIRA...TUSONGE MBELE! Wakati ni sasa!
TUPO PAMOJA....Mungu ibariki Tanzania....!
Ni Wazo muafaka sana kwa sasa CHADEMA kuanzisha vyombo vyake rasmi vya Habari ikiwa ni pamoja na TV, Radio na Magazeti. Wazo hili limekuwa hamasa sana na linaungwa mkono na kila watu 8 kati ya 10 unaokutana nao na kuwauliza umuhimu wa CDM kuwa na chombo chake rasmi cha habari kinachoweza kuwafikia wananchi kwa asilimia kubwa popote Tanzania. Wengi wanasema CDM inasubiri nini? Au hadi Mafisadi wapeleke muswada kuondoa uhuru wa Vyama vya Siasa kumiliki vyombo vyao vya habari? Chama cha Mafisadi kimejiwekea mbinu zao za propaganda ikiwapo Radio-feki, magazeti-ya kufungia vitumbua nk....lakini wameishia kuchakachua haki za umma na kufisadi hata kujichakachua kwa siasa na kura za wao kwa wao! Sasa wanaelekea kule Baba wa Taifa alipokwishawatabiria!
Wadau, katika kulikomboa taifa, lazima tukubaliane kuwa gharama, kutoka jasho na kujitolea ni sehemu ya ukombozi, hasa kwa nchi ambayo imedhoofishwa na mafisadi kama taifa la Tanzania. CDM inayo nguvu ya umma na hakuna woga hata chembe ktk kuijengea umma ukurasa na jukwaa jipya la habari sahihi na siasa sahihi kwa ukombozi wa umma!!
Ili ukombozi uwafikie wananchi wote na waelewe kwa nini wao ni masikini kwa Miaka zaidi ya 50 toka wapate uhuru, na kwanini wamebaki dhaifu na kwa nini wanahitaji haraka kujenga fikra sahihi, na ni kwanini wachague siasa sahihi (waachane na maji-taka) na wapate maendeleo ya kijamii, suala la HABARI NI NGUVU KAMILIFU. "Information is Power" na hakuna wa kuibadili kauli na ukweli huo.
Maisha ya taifa hili kwa jinsi yaliyotokomea mifukoni mwa wajanja na mafisadi wachache, ni muhimu sana wapate habari, kwa haraka, mapema na zisizokuwa na ukandamizaji, na kujengewa woga. Tukumbuke kuwa, Mifumo ya mitandao kama Internet, e-mails nk kwa sasa inawafikia wachache sana na hasa waliojikusanya mijini. Ni wananchi wachache mno wanaoweza kupata habari za kweli kupitia Radio, TV na magazeti ya binafsi yasio na mlengo wowote wa kiitikadi, na hasa masikini waliojaa vijijini, ambao ndio wamebaki kuwa chambo na kuvikwa minyororo ya mateso na kitanzi na Chama cha Mafisadi ili kujichukulia na kujinufaisha kwa hali zao na kuwaangamiza watanzania kwa kuwaibia kura na kuwajengea woga wasiweze kujitetea, wazidi kutokujiamini ili kuwaibia rasilimali zao. Mwisho ndio sasa!!
HAKIKA, Sasa ni wakati muafaka kwa CDM kutangaza mkakati rasmi wa kuanzisha Vyombo vyake rasmi vya mawasiliano ikiwapo TV, Radio na Magazeti ili kukamilisha harakati za ukombozi wa Taifa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uraia, Katiba, na siasa safi kwa ajili ya kulinusuru taifa hili linaloangamia kwa kasi. CDM itakapotoa Tamko Rasmi kuhusu Mkakati huu, nchi itatikisika kwa jinsi Wananchi kwa mamilioni toka katika Mikoa yote, Wilaya, Majimbo, Kata, Tarafa, Vijiji hadi vitongoji watakavyojitolea kwa hali na mali tayari kwa Michango, kuchangia ufanisi wa ukombozi huu kwa njia zozote zile kama wafanyavyo bila kuchoka ktk masuala ya dini, sherehe nk. Tunaomba CDM itangaze rasmi mkakati huu mapema iwezekanavyo! Wananchi wamejaa HAMASA sana, ili ndani ya 2012 hadi mwishoni mwa 2013, tuwe katika ramani halisi ya kuwapa watanzania walichokikosa miaka yote. Muda ni sasa! MUDA ULIOBAKI KUFIKA 2015 NI MFUPI SANA NA UNAENDA KWA KASI SANA!. Watanzania wanahitaji kwa haraka Habari sahihi na Siasa sahihi na uongozi sahihi kuelekea 2014, MUDA NI MFUPI SANA! Mara ifikapo 2015 kuelekea kupiga kura, Taifa linatakiwa liwe limekomaa hasa! Taifa jipya linaundwa kutokana na Wapiga Kura waliojaa elimu, fikra na Hamasa za ukombozi na maendeleo ya jamii na nchi yao!
NAOMBA KUWASILISHA, tuchanganue na tujadili, TUTOE DIRA...TUSONGE MBELE! Wakati ni sasa!
TUPO PAMOJA....Mungu ibariki Tanzania....!