Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,961
- 2,138
PPF ni moja ya mifuko ya mafao ya uzeeni ambayo imelalamikiwa sana juu ya malipo duni kwa wanachama wao ikilinganishwa na mifuko mingine.
Habari tuliyonyaka inaonyesha kwamba wajumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake kipindi kilichopita ilipitisha na kujilipa milioni 200 kwa kila mjumbe. Hiyo ikiwa eti ni shukrani kwa kazi nzuri waliyofanya.
Nimepiga mahesabu yangu kwa idadi ya wajumbe wa bodi ambao walikuwepo, ambao ni wanane mbali na staff wengine wa pembeni:
1. Gray Mgonja
2. Prof Bertha Koda
3. Monica Mbega
4. Elvis Musiba
5. Ramadhan Khijah
6. Dr Kassim Kapalata
7. William Erio
8. Samwel Lwakatare
inaonyesha zaidi ya bilioni iliondoka.
Je, hii ni halali? Wanacahama wa PPF wengine huishia milioni 20 baada ya kuchangia hata kwa miaka 25. hawa wajumbe wanajilipa milioni 200 kila mtu kwa kukaa ktk vikao vya bodi kipindi kisichofikia hata miaka 5!! Na tena nasikia hao hao tena wamependekezwa kurudi ndani ya Bodi.
Heb
Ndugu MchunguZI, naomba ulete vithibitisho kama vile signed minutes, cheque number nk kuonyesha uchotaji huu wa fedha za walalahoi. Na kama taarifa yako ni ya kweli, kazi tunayo kwani huyo Gray Mgonja bado ana soo ya EPA na richmond na tayari kajichomekea ufisadi mwingine!! Na huyo dada Mbga naye,mmmmmmm hhhhhh!!!!