Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Waziri wa Uchukuzi , Mh. Omar, mimi ninamwelewa na nimemkubali.
Kupitia ITV amesema tuimarishe PPP na sio kutegemea bajeti ikiwa ni pamoja na kukaribisha wawekezaji kwa kuwapa vivutio, kuingia Ubia na pia ubinafsishaji ; tuondoe ukiritimba katika huduma zetu za usafiri na tuongeze ushindani katika usafirisaji ili kuboresha huduma na kupunguza gharama kwa wateja.
Ni kwa kiwango gani Wanasiasa na Vyama vya Wafanyakazi wanamwelewa na watampa ushirikiano juu ya anachoeleza hususani suala ka kukaribisha Wawekezaji toka nje na kuingia nao mikataba jambo ambalo sasa inabidi ulitetee huku unatokwa jasho baada ya yaliyoonekana mfano katika Mamlaka ya Reli yetu na katika eneo la Nishati & Madini.
Mwisho nimeuona ukweli wake wake alipogusa kwa lugha laini tatizo la uzabuni wa Car tracking system ambao tayari umepigiwa kelele na baadhi ya wamiliki wa mabasi.
Nilichokikosa kwake ni kutoongea kwa ushupavu na nguvu zote kukemea wanaochelewesha wateja na mizigo yao bandarini na wadokozi na pia kama Waziri, tone yake juu ya hiyo tracking system isingekuwa kama ya kulalamika bali ya kuagiza utaratibu mpya ulio wazi na unaozingatia kupunguza ajali katika mazingira mbalimbali na wenye wazabuni wengi utumike.
Vinginevyo nimejisikia vizuri sana kuona wasomi kama hawa wanapata nasafi kutumia ujuzi na uzoefu wao walioupata nje na ndani ya nchi katika maendeleo ya nchi yao!
Kupitia ITV amesema tuimarishe PPP na sio kutegemea bajeti ikiwa ni pamoja na kukaribisha wawekezaji kwa kuwapa vivutio, kuingia Ubia na pia ubinafsishaji ; tuondoe ukiritimba katika huduma zetu za usafiri na tuongeze ushindani katika usafirisaji ili kuboresha huduma na kupunguza gharama kwa wateja.
Ni kwa kiwango gani Wanasiasa na Vyama vya Wafanyakazi wanamwelewa na watampa ushirikiano juu ya anachoeleza hususani suala ka kukaribisha Wawekezaji toka nje na kuingia nao mikataba jambo ambalo sasa inabidi ulitetee huku unatokwa jasho baada ya yaliyoonekana mfano katika Mamlaka ya Reli yetu na katika eneo la Nishati & Madini.
Mwisho nimeuona ukweli wake wake alipogusa kwa lugha laini tatizo la uzabuni wa Car tracking system ambao tayari umepigiwa kelele na baadhi ya wamiliki wa mabasi.
Nilichokikosa kwake ni kutoongea kwa ushupavu na nguvu zote kukemea wanaochelewesha wateja na mizigo yao bandarini na wadokozi na pia kama Waziri, tone yake juu ya hiyo tracking system isingekuwa kama ya kulalamika bali ya kuagiza utaratibu mpya ulio wazi na unaozingatia kupunguza ajali katika mazingira mbalimbali na wenye wazabuni wengi utumike.
Vinginevyo nimejisikia vizuri sana kuona wasomi kama hawa wanapata nasafi kutumia ujuzi na uzoefu wao walioupata nje na ndani ya nchi katika maendeleo ya nchi yao!