Waziri wa Nishati na Madini awawashia moto Wakorea kwa kumdharau

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Date::7/31/2008
Waziri wa Nishati na Madini awawashia moto Wakorea kwa kumdharau
Na Habel Chidawali, Mpwapwa
Mwananchi

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, juzi aliwajia juu wanunuzi wa madini wakiwamo raia wa Korea akisema wamemdharau kwa kutoka nje katika semina ya madini wilayani hapa.

Ngeleja aliyasema hayo baada ya kutoa hotuba ya ufunguzi wa semina iliyokuwa imeandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mpwapwa kwa lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kujua thamani za madini na namna ya kuondokana na umasikini kwa kutumia rasilimali hiyo.

Waziri huyo alipomaliza kutoa hotuba yake ya ufunguzi juzi katika Ukumbi wa Sinema mjini Mpwapwa, wanunuzi hao walisimama na kutoka ukumbini wakati mada kuhusu madini ikitolewa na Afisa Madini Mkazi na kujikuta akiwa na wanachama wa CCM na wananchi.

Baada ya kuona hivyo, Ngeleja alimtuma Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Deogratius Rutta, kutoka nje kwenda kuwafuata wanunuzi hao ambao wengi wao ni raia wa Korea na kuwaambia warudi ukumbi.

Walipoingia ukumbini, aliwashambulia kwa maneno na kubadilika ghafla sura yake na kuwa mkali mithili ya mbogo.

Ngeleja aliomba kipaza sauti na kuanza kusema kwa ukali kuwa Wakorea hao, wameshindwa kumheshimu kwa kuonyesha kumdharau hizo mbele yake na kusisitiza kuwa anaamini wageni hao wanawadharau zaidi raia wa kawaida wanaowauzia madini.

Aliendelea kusisitiza kuwa, dharau zao hizo zinaonyesha kuwa huenda zinatokana na kuwanyonya Watanzania wanaowapelekea madini hayo kwa kununua kwa bei ndogo.

Ngeleja alisema anakielewa Kiingereza huenda kuliko wao na kusisitiza kwamba hawezi kukitumia kama wao wanavyotaka kwa sababu katika mkutano huo wengi wao wanazungumza Kiswahili ambacho ni lugha mama ya Tanzania.

''Nimechukizwa sana na kitendo cha ninyi kuondoka katika mjadala huu wakati mkijua kabisa kuwa hili linawahusu na ninyi nawaheshimu na kuwajali, lakini katika hili mmeniudhi sana siwezi kuvumilia ni lazima niseme,'' Ngeleje alisema na kuendelea kutoa dukuduku lake kwa akaongeza kuwa:

''Hamjui kuwa mimi ndie mwenye dhamana ya madini hapa Tanzania kwa niaba ya Watanzania wote, ninaweza kusema hapana au ndio kwani kutokujua sheria isiwe chanzo cha kuvunja sheria, hata katika nchi zenu kuna taratibu na sheria kwani muda wote mliokaa hapa hakuna mtu anayeweza kuwatafsiria Kiswahili ndio maana mkaamua kuondoka, naomba tuheshimiane.''

Aliwaambia wanunuzi hao kuwa ni lazima watafute wakalimani ili wanapokutana na umati katika hafla kama hizo, waweze kutafsiriwa kila kinachozungumzwa kuliko kutaka kulazimisha kiongozi kuzungumza Kiingereza katika nchi yake wakati kuna Kiswahili ambacho kinaeleweka na wananchi wengi wa vijijini.

Mmoja wa wanunuzi hao alisimama na kutuliza mzuka wa Waziri kwa kuomba radhi kwa niaba ya wenzake.

Mnunuzi huyo aliyejulikana kwa jina moja la Omary alimwomba Waziri Ngeleja kuwasamehe na kuahidi kuwa hawatarudia kitendo kama hicho katika mikutano ya aina yoyote.

Omary alisema kwa kuwa amekaa kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam anakifahamu Kiswahili vizuri, hivyo atakuwa mstari wa mbele kuwatafsiria wenzake kila neno lililokuwa likizungumzwa katika semina hiyo.

Kutokana na Waziri huyo kuchukizwa na kitendo cha wanunuzi hao, walikaa hadi saa 12:00 jioni juzi semina hiyo ya siku moja ilipofungwa.
 
mweh.. ningekuwa mimi wakati anaanza kufoka ningetoka tena nione polisi waje kunikamata na kunilazimisha kusikiliza, halatu ningeweka vidole masikioni kabisa..! duh.. madaraka matamu kweli!
 
Ndio Mawaziri wetu hao, ubabe ubabe.

Ndiyo tunavyojenga utamaduni wa kuvutia wawekezaji hivi? Waziri angeweza kuwaweka wawekezaji kwenye mkutano kama wangekuwa wanaelewa, kama angekuwa anawajali angeweza hata kuongea Kiswahili na kuhakikisha kuna mkalimani anayetafsiri kiingereza kwa manufaa ya wawekezaji.

Waziri amejionyesha hajali wawekezaji, hana diplomasia na amejaa ubabe, na anaweza kuikosesha Tanzania jina zuri.Kama mimi muwekezaji naenda Korea halafu Waziri wa Kikorea hataki kuongea lugha ninayoijua mimi na wala hafanyi mpango wa kunitafsiria unafikiri nitapoteza muda kumsikiliza? Ili iweje? Nitavuka kwenda kwenye nchi wanayonithamini.

Huyo bwana Omary alifanya diplomasia tu kuomba radhi lakini Waziri alitaka kuwafanya hawa Wakorea kama wanawe.
 
hahahaha, duh si mchezo!
ila mimi nafurahi jinsi alivyowapa laivu hawa jamaa, sometimes kiongozi lazima awe na uso wa mbuzi.
Kutoonyesha heshima kwa waziri, ni kutoonyesha heshima kwa wananchi,kama walitaka kuondoka wangeoonyesha ishara ya kumtaka radhi waziri ili kuonyesha heshima, then wangejiondokea.
otherwise waziri hawezi kufunga safari kuhudhuria function hiyo, halafu kumbe jamaa hawana interest
 
Mh! swala linawahusu halafu mnaongea kiswahili na wao hawajui kiswahili!

Niliwahi hudhuria mkutano zaidi ya robotatu wajumbe walikuwa hawajui kiswahili lakini wajumbe wote wanajua kiingereza, mgeni rasmi akalazimisha ahutubie kiswahili na hakujali kujua kama kuna mkalimani kwa wale wasiojua kiswahili!

utajisikiaje rafiki yako amekualika kwake then wakawa wanaongea kihaya muda wote nawewe ndo hakipandi, niwakati sasa wote tuheshimiane na tujue tz inakua, watu toka mataifa mbalimbali wanafika kujumuika nasi katika kuganga njaa.

Mwenyekiti wa kikao alipaswa kujua kuwa wajumbe wengine hawajui kiswahili na angeandaa utaratibu wa kupata mkalimani.
 
Ngeleja alisema anakielewa Kiingereza huenda kuliko wao na kusisitiza kwamba hawezi kukitumia kama wao wanavyotaka kwa sababu katika mkutano huo wengi wao wanazungumza Kiswahili ambacho ni lugha mama ya Tanzania.

''Nimechukizwa sana na kitendo cha ninyi kuondoka katika mjadala huu wakati mkijua kabisa kuwa hili linawahusu na ninyi nawaheshimu na kuwajali, lakini katika hili mmeniudhi sana siwezi kuvumilia ni lazima niseme,'' Ngeleje alisema na kuendelea kutoa dukuduku lake kwa akaongeza kuwa:

''Hamjui kuwa mimi ndie mwenye dhamana ya madini hapa Tanzania kwa niaba ya Watanzania wote, ninaweza kusema hapana au ndio kwani kutokujua sheria isiwe chanzo cha kuvunja sheria, hata katika nchi zenu kuna taratibu na sheria kwani muda wote mliokaa hapa hakuna mtu anayeweza kuwatafsiria Kiswahili ndio maana mkaamua kuondoka, naomba tuheshimiane.''

Aliwaambia wanunuzi hao kuwa ni lazima watafute wakalimani ili wanapokutana na umati katika hafla kama hizo, waweze kutafsiriwa kila kinachozungumzwa kuliko kutaka kulazimisha kiongozi kuzungumza Kiingereza katika nchi yake wakati kuna Kiswahili ambacho kinaeleweka na wananchi wengi wa vijijini.

.

Ubabe wa viongozi, yeye ndio mwenye kuamua hatima ya mambo ya madini Tanzania. Kayasema Innocent wa houston kwenye makala yake!
 
Ni ajabu sana, so alipenda hawa watu wakae tu hata bila kusikiliza au kutilia maanani aliyokuwa anaongea. Kwanini asijiulize ni kwanini hao watu waliondoka? inawezekana kuwa alikua anaongea mambo yasiyo na maana kwao. Hongera waziri, ungekaa kimya na kuchukia kimoyomoyo ingekuwa vizuri zaidi kuliko kujidhalilisha namna hii
 
Hujui sababu ya kuwatisha na huku akijilabu kwamba yeye ndio dhamana wa madini.
 
Mwehu! Au kwa vile nasikia ana undugu wa karibu na rais basi anajiona ni 'mwenye nchi'? Alafu jamani hawa waasia huwa wanafuata sana protokali, hasa wajapani na wakorea. sidhani wangeondoka kama wangeona ni kinyume cha protokali. Si walisubiri mpaka amalize hotuba? Sasa hao wengine blahblah yao wasikilize ya nini?
MWkjj is right, just keep walking and ignore the idiot!!!
 
Wale wakorea mnawaonea bure...walikuwa hawaelewi hata neno moja ukiacha yule Omary,anaesema anajua sana...sasa walisubiri wafungue mkutano...wakaona hakuna haja.."wakasepa"...nafikiriaa kupigania bei ndogo ingehusisha wachimbaji na wadau wote...pia semina endelevu toka wizara ili wachimaji wajue bei...za masoko mbali mbali,pia na ubora wa madini....sasa kupitia kwenye vyama vyao wangeweza kupigana na bei baada ya kuwa na ufahamu....mpana wa madini.....Kukaa hadi mwisho hakutabadilisha lolote kwenye kuwalalia na kuwanyonya wananchi kwa bei zao ndogo.....
 
Sasa kosa la WAziri liko wapi hapa,

Angekaa kimya ingeonekana anawanyenyekea Wawekezaji.wakati mwingine tusiwe na hoja zisizo na msingi.
 
Culture ya dudu CCM kazini.
Hawatengenezi mazingara ya kueleweka bali wanataka mtulinga. Kama waziri alijua Wakorea watakuwepo na ni wa muhimu kwetu na kama anajua kiingereza na basi akiongee ingalao kwa kutafusiri aliyoongea kwa kiswahili ili iwe win-win kwa wote.
Hata hivyo topic kama si muhimu kwa wakorea ama kama angeongea utumbo bado angesuswa kwani hawajavunja sheria yeyote ya nchi ili mradi biashara yao haidhuriki na hiyo semina.
Wakorea wangeamua kupiga usingizi je? wamgewaamsha? kwa sabau bado ni dharau.
 
The waziri alikuwa right jamani hawa watu as wana dharau...fanya nao kazi uone.
Sasa waliona taabu gani kukaa hata kama hawaelewi...wakijua ni waziri wa madini.

Hii ni dharau kwa kuwa wanafikiri wanapesa...leo hii tukikataa kuwauzi wata piga magoti.
They need us we need them...so ni two way trafic nyerere ingekuwa wakati wake wangepanda next dash to kwao....

Huwezi ukaja na kudharau viongozi wetu...kihorera horera....hata kama sie wanatutatiza.
 
Usikute jamaa hawakupita kumwona ofisini !!! Ukali huu si bure,wangekuwa wamempitia angeweza kweli kuwakoromea? Kama kweli mkali tusubiri tuone wale jamaa wa pale Ubungo kama watang`oa ile mitambo kama tulivyoimbiwa na Tanesco.
 
Usikute jamaa hawakupita kumwona ofisini !!! Ukali huu si bure,wangekuwa wamempitia angeweza kweli kuwakoromea? Kama kweli mkali tusubiri tuone wale jamaa wa pale Ubungo kama watang`oa ile mitambo kama tulivyoimbiwa na Tanesco.
Si ni maamuzi ya Serikali,Mie kwa upeo wangu watang'oka tu bila tatizo lolote,kama Mamvi alilng'oka kwanini wao wabaki?

Yes i said,The Minister was Right on this ,wewe ulitaka azungumzze kiingereza na wanachi wangemulewaje?haikuwa semina ya Wakorea bali ilikuwa wananchi na wawekezaji waliitwa pale ili na wao wasikilize,ili baadaye isije ikatokea migogoro.
 
kanisani kwetu ilibidi uanzishwe utaratibu wa kutafasiri ibada baada ya kuonekana familia moja tu isiyojua kiswahili. kwa hiyo kwa ajili ya hiyo couple ibada nzima inatafsiliwa je sembuse watu wengi namna hiyo.kwanza umewanyima uhuru wa kutoa mchango wao.watauliza nini wakati hawajui
 
The waziri alikuwa right jamani hawa watu as wana dharau...fanya nao kazi uone.
Sasa waliona taabu gani kukaa hata kama hawaelewi...wakijua ni waziri wa madini.
Hii ni dharau kwa kuwa wanafikiri wanapesa...leo hii tukikataa kuwauzi wata piga magoti.
They need us we need them...so ni two way trafic nyerere ingekuwa wakati wake wangepanda next dash to kwao....
Huwezi ukaja na kudharau viongozi wetu...kihorera horera....hata kama sie wanatutatiza.

Sina hakika kama ni lazima tujadili kila kitu lakini naona kama ndio trend yetu hapa JF.
Lakini inashangaza sana kuona habari za heshima zinaingia hapa. Kwangu mimi nadhani hawa ni wafanyabiashara kama wafanyabiashara wengine. La muhimu kwao ni tija na wala sioni sehemu heshima inapoingia. Kama wanafanya biashara wao wanaangalia jambo moja tu - je biashara iliyo mbele yao ina faida kwao. Kama hamna faida, basi hamna deal na sioni wapi swala la heshima linakuja.
Serikali inataka kufanya biashara nao - basi iandae win-win situation. Kinyume chake yeyote ana ruhusa ya ku-walk away kwani kwenye biashara yoyote muda ni muhimu na wala si heshima. Una faida gani kuweka heshima pasipo tija.
Nadhani Ngeleja anatakiwa kuwa waziri wa elimu - awe anawahutubia wanafunzi wa shule - kule ana haki ya kufoka na kutandika. Lakini kwenye swala la mikataba ya biashara ni sera safi au la.
 
Sasa mbona wabunge huwa bungeni hawakai,tena wengine hutoka wakati mijadala inaendelea? Mara nyingi ukiangalia kwenye tv utaona bunge liko nusu,sasa hio nayo sio dharau,maana ndio kazi waliyotumwa.Hao wakorea hio semina ingekuwa ina maana kwao,lazima wanagebaki.Wao ni wafanyabiashara,na wazungu husema time is money...Then hapohapo tunalilia wawekezaji.Semina zote hizi ni za ulaji tu,hao wakorea wameshtuka na kujiondokea,tena wameondoka baada ya yeye waziri kumaliza ufunguzi wake.
 
Date::7/31/2008
Waziri wa Nishati na Madini awawashia moto Wakorea kwa kumdharau
Na Habel Chidawali, Mpwapwa
Mwananchi

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, juzi aliwajia juu wanunuzi wa madini wakiwamo raia wa Korea akisema wamemdharau kwa kutoka nje katika semina ya madini wilayani hapa.

Ngeleja aliyasema hayo baada ya kutoa hotuba ya ufunguzi wa semina iliyokuwa imeandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mpwapwa kwa lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kujua thamani za madini na namna ya kuondokana na umasikini kwa kutumia rasilimali hiyo.

Waziri huyo alipomaliza kutoa hotuba yake ya ufunguzi juzi katika Ukumbi wa Sinema mjini Mpwapwa, wanunuzi hao walisimama na kutoka ukumbini wakati mada kuhusu madini ikitolewa na Afisa Madini Mkazi na kujikuta akiwa na wanachama wa CCM na wananchi.

Baada ya kuona hivyo, Ngeleja alimtuma Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Deogratius Rutta, kutoka nje kwenda kuwafuata wanunuzi hao ambao wengi wao ni raia wa Korea na kuwaambia warudi ukumbi.

Walipoingia ukumbini, aliwashambulia kwa maneno na kubadilika ghafla sura yake na kuwa mkali mithili ya mbogo.

Ngeleja aliomba kipaza sauti na kuanza kusema kwa ukali kuwa Wakorea hao, wameshindwa kumheshimu kwa kuonyesha kumdharau hizo mbele yake na kusisitiza kuwa anaamini wageni hao wanawadharau zaidi raia wa kawaida wanaowauzia madini.

Aliendelea kusisitiza kuwa, dharau zao hizo zinaonyesha kuwa huenda zinatokana na kuwanyonya Watanzania wanaowapelekea madini hayo kwa kununua kwa bei ndogo.

Ngeleja alisema anakielewa Kiingereza huenda kuliko wao na kusisitiza kwamba hawezi kukitumia kama wao wanavyotaka kwa sababu katika mkutano huo wengi wao wanazungumza Kiswahili ambacho ni lugha mama ya Tanzania.

''Nimechukizwa sana na kitendo cha ninyi kuondoka katika mjadala huu wakati mkijua kabisa kuwa hili linawahusu na ninyi nawaheshimu na kuwajali, lakini katika hili mmeniudhi sana siwezi kuvumilia ni lazima niseme,'' Ngeleje alisema na kuendelea kutoa dukuduku lake kwa akaongeza kuwa:

''Hamjui kuwa mimi ndie mwenye dhamana ya madini hapa Tanzania kwa niaba ya Watanzania wote, ninaweza kusema hapana au ndio kwani kutokujua sheria isiwe chanzo cha kuvunja sheria, hata katika nchi zenu kuna taratibu na sheria kwani muda wote mliokaa hapa hakuna mtu anayeweza kuwatafsiria Kiswahili ndio maana mkaamua kuondoka, naomba tuheshimiane.''

Aliwaambia wanunuzi hao kuwa ni lazima watafute wakalimani ili wanapokutana na umati katika hafla kama hizo, waweze kutafsiriwa kila kinachozungumzwa kuliko kutaka kulazimisha kiongozi kuzungumza Kiingereza katika nchi yake wakati kuna Kiswahili ambacho kinaeleweka na wananchi wengi wa vijijini.

Mmoja wa wanunuzi hao alisimama na kutuliza mzuka wa Waziri kwa kuomba radhi kwa niaba ya wenzake.

Mnunuzi huyo aliyejulikana kwa jina moja la Omary alimwomba Waziri Ngeleja kuwasamehe na kuahidi kuwa hawatarudia kitendo kama hicho katika mikutano ya aina yoyote.

Omary alisema kwa kuwa amekaa kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam anakifahamu Kiswahili vizuri, hivyo atakuwa mstari wa mbele kuwatafsiria wenzake kila neno lililokuwa likizungumzwa katika semina hiyo
.

Kutokana na Waziri huyo kuchukizwa na kitendo cha wanunuzi hao, walikaa hadi saa 12:00 jioni juzi semina hiyo ya siku moja ilipofungwa.

Alaa! KUMBE KISWAHILI baadhi walikuwa wanakijua,mmh ngeleja hapo umetema cheche live
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom