Waziri wa elimu - mulungo ni muongo - wakufunzi vyuo vya ualimu wagoma

NGOSWE.120

JF-Expert Member
Jul 9, 2011
219
233
Naibu waziri wa Elimu bwana Mulugo amewadanganya wakufunzi wa chuo cha Ualimu Songea kuwa madai yao yote yanayohusu upandishwaji wa madaraja/vyeo, malipo ya malimbikizo ya mshahara, likizo, na mengineyo yatalipwa ndani ya quarter ya kwanza ya mwaka wa fedha yaani btb July and September.

Hata hivyo kuanzia jana wakufunzi wote wa vyuo vya Ualimu Tanzania ambavyo vipo chini ya Idara ya Ualimu wameanza mgomo wa kutoingia madarasani kufundisha hadi pale madai yao yatakapolipwa hata ikiwa ni mwakani lakini darasani haingii mtu hata kwa mtutu wa bunduki.

Aidha wameishinikiza serikali kuanza kulipa mishahara kwa scale mpya stahiki za wakufunzi kutokana na waraka mpya uliosainiwa na katibu mkuu utumishi bwana yambesi lakini hadi leo hawajaanza kulipwa mishahara hiyo .

NB: Wanachuo wa chuo cha Ualimu Songea nao leo hii wameanza mgomo kwa kutoingia darasani kuishikiza serikali wawalipe wakufunzi ili wao wapate elimu walio ifuata hapo chuoni.
 
Kazi ipo. Hivi mishahara ya mwezi Oktoba hapo Matogoro wamepata tarehe ngapi vile?
 
Kazi ipo. Hivi mishahara ya mwezi Oktoba hapo Matogoro wamepata tarehe ngapi vile?


Mkuu mishahara wengine ndio leo hii imeingia ktk account zao, na wengine jana saa 1 usiku.


Leo hii kulikuwa na kikao cha usuruhishi ambapo mkuu wa mkoa alimtuma Afisa elimu mkoa aje kutuliza hii hali tete lakini moto umemshinda kuuzima. Yeye anadai serikali haina pesa hivyo tuvumilie tu hadi hapo serikali itakapo pata pesa za kutulipa madeni yetu na madai mengine ya kupandishwa madaraja stahiki.

MAAZIMIO YA WAKUFUNZI

1. Tunaendelea kuja kazini na kusaini kitabu cha mahudhurio cha kila siku kazini.
2. Hakuna kufundisha darasani hadi hapo madeni yetu yatakapo lipwa hata ikiwa mwaka 2015.
3. Kuendelea kusimama pamoja bila kutetereka wala kuogopa kufukuzwa kazi.
4.Tupo tayari kufukuzwa kazi wakufunzi wote hata ikiwa ni kesho, na wakifanya hivyo basi sheria zipo na tutaiburuza serikali mahakamani na tuna uhakika tutashinda.

NB: Wanachuo wetu hapa chuoni wanaanza mgomo/movement jumatatu kuushinikiza uongozi wa chuo ili wafundishwe madarasani. Kwetu sisi hiyo ni golden chance coz sauti zao zitatufanya kilio chetu kisikike Tanzania nzima.

Mwisho wakufunzi kama hawatalipwa chuo kitafungwa na wanachuo wapatao 1105 hawatafanya mtihani wa muhula hivyo kukosa continous assessment zao (CA) na kuwaandalia mazingiza ya kufeli mtihani wa taifa hapo may, 2012.

Ni hayo mkuu, pia tuchangieni mawazo yenu ili kuboresha hii kitu.
 
Kazi kweli kweli!!! Katika mikakati yenu CWT wanashirikishwa vipi? Kama hawana sauti yoyote muwaunganishe nao kwenye mgogoro kwa kukata kuchangia michango ya CWT maana inaonekana hawana kazi yoyote
 
Back
Top Bottom