Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Nimesoma mahala kuwa Sofia Simba alikutana na Kitwana na wakiwa wanafunzi wa Kikwete Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Nadhani siyo kweli; huyu Sofia Simba alisoma na akina Lawrence Masha pale sheria akiwa "CHUA" mwishoni mwa miaka ya 80. Nadhani alikuwa intake moja na mama Sita au walipishana kidogo. Wakati huo Kitwana Kondo alikuwa ni Meya wa jiji la Dar na Kikwete alikuwa kwenye siasa siku nyingi sana. Inawezekana Mzee Kitwana Kondo alianza kumkamua mama huyu wakati angali akifanya huko MEIDA kabla ya kuingia chuo.

Ingawa ni kweli kuwa mama Sofia Simba "kashinda uchaguzi huo kihalali kulingana na taratibu za chama chake" yeye kama kiongozi alitakiwa atumie effort kubwa kuunganisha jumuia yake mara moja badala ya kuanza kujibarangua na mapati ya gharama ambayo yanazidi kusambaratisha jumuia yake hiyo. Angejifunze kwa mwenzake Obama aone jinsi alivyomtunza mpinzani wake mkuu Hilary, na yeye amtunze mpinzani wake mkuu Janeti ili wajenge jumuia yao. Angalia kuwa sehemu kubwa ya kabinet ya Obama imetokana na kabineti ya Clinton.

Kichuguu wewe unadhani viongozi wetu wanajua hayo? kwani atamlingishia saa ngapi opponent wake?
Haya ndio matokeo ya viongozi tulo nao leo.
Nasita hata ninapowaita viongozi. In actual sense hawa ni watawala wetu!
 
Hurry up.....

Nimebadilisha mawazo. Tutabanana tu siku moja. Kama Cha Nkapa alivyo, itafika siku mtazomewa wote na ku............... Hapo ndipo mtaona wivu wetu ukoje. Maisha mazuri sana ili kujinyonga. Kuna ule msemo waingereza wanasema "Heri Tembo aku-CHASE wewe au simba?" Mie nasema Heri afukuzwe Simba. Kwa hiyo inapokuja wa kujinyonga, siku itafika mtu atajichimbia shimo au kweli kwenda kujinyonga, but not me. Ngoja nikapate wanzuki langu..........
 
But on a serious note - do we really really need these jumuiya ?- wanawake wa CCM, wazazi wa CCM, vijana wa CCM and all this nonsense ! This is another reason why I can not understand CCM and its national priorities. Divide and rule politics - hasa kama unaowatawala wamelala kama watanzania walio wengi.
 
But on a serious note - do we really really need these jumuiya ?- wanawake wa CCM, wazazi wa CCM, vijana wa CCM and all this nonsense ! This is another reason why I can not understand CCM and its national priorities. Divide and rule politics - hasa kama unaowatawala wamelala kama watanzania walio wengi.




Mkuu Meg hakika, bila shaka yeyote hizo ni PWENTI kabambe!!!!
 
Ni uchu wa madaraka na kulinda maslahi ya makundi ndo yanayoleta shida....the behavior shows lack of leadership skills for both of them. Ni tatizo kubwa tulilonalo kama nchi sasa hivi. Viongozi wakweli ni wachache sana..wamejaa wababaishaji kibao
 
The bottomline as per trends in leadership position is - you have to belong.It is "know who and not know how"! Kama wewe siyo mwenzao na huna wa kukushika mkono kukuvuta, hufiki popote. Otherwise kusingekuwa na kurundikiana vyeo na nafasi kwa kiwango kikubwa hivi.Mtu mmoja unakuta ni Waziri, mbunge,mjumbe wa bodi kadhaa,mwenyekiti wa Tume,mjumbe wa kamati fulani n.k.Kwani ina maana katika watanzania say hata milioni 5 kati ya wananchi milioni zaidi ya 34 ( idadi ya watu - ikijumlisha watoto,wazee,walemavu na wanafunzi ambao bado hawajafikia kiwango cha kushiriki uongozi) wenye elimu na sifa nyingine wasingeweza na wao kupewa nafasi katika hizi taasisi? Fikiria hata marupurupu yaendanayo na teuzi hizo, kwanini yafaidishe familia moja tu? Hivi tusingeweza kupunguza umaskini wa watanzania wengi zaidi kwa kugawana hizi fursa?Serikali ingeliangalia hili nalo kama kweli inawajali wananchi wake.
Kuna hata suala la diversity - kwa maana ya watu wa dini tofauti, jinsi,umri, sifa na ujuzi, uzoefu n.k mara nyingi huchangia ufanisi na ndiyo maana nchi nyingine wanahimiza sana diversity kwani wanaelewa faida zake.
 
The bottomline as per trends in leadership position is - you have to belong.It is "know who and not know how"! Kama wewe siyo mwenzao na huna wa kukushika mkono kukuvuta, hufiki popote.

- Hii works kwa vyama vyote bongo, hivi unaweza kushinda Chadema bila kushikwa mkono? au!
 
wakuu

nilikua natazama picha za mapokezi ya huyo mwenyekiti mpya UWCCM hapa http://dailyhabari.wordpress.com/special dailyhabari events/,
nikitazma naona kuna watu wanajiposition kama secret service body guards wake
(Ref. thread maarufu ya Mkuu Icadon).

Ninachojiuliza, je(kama ni bodyguards in plain clothes) kuna anayeweza kuwatambua
kama ni watu wa TISS? na kama ndio wanaingiaje kwenye cherekochereko za ushindi wa jumuiya za chama? au kwa vile ni Waziri wao?.... Just curious.
 
Tunapomrundikia vyeo/nafasi nyingi mtu mmoja ndio chanzo cha mtu kutoka mkutano mmoja kwenda kwenye mwingine (BILA MATAYARISHO) halafu anachangia nini???? Angalia wanapokuwa bungeni, unaona mtu amelala, wenzake wakipiga meza nae anaamka anaanza kupiga meza, je anajua anachoshangilia au mkumbo to. Labda jana yake alikuwa kwenye mkutano wa siri nusu ya usiku wote akatoka huko akaingia bungeni. Je utasoma "board papers ngapi na ufanye thathimini vizuri kabla ya kuingia kwenye "board meeting" ili umpime CEO vizuri. Ndio maana kampuni mpaka inafilisika na Baraza la Wakurugenzi lipo halijasema chochote.................. inakuwaje???
Tuwape madaraka watu kwa kupima muda wanaoweza kuweka kwenye kazi hizo, SIKU INA MASAA 24 TU.
 
Nimebadilisha mawazo. Tutabanana tu siku moja. Kama Cha Nkapa alivyo, itafika siku mtazomewa wote na ku............... Hapo ndipo mtaona wivu wetu ukoje. Maisha mazuri sana ili kujinyonga. Kuna ule msemo waingereza wanasema "Heri Tembo aku-CHASE wewe au simba?" Mie nasema Heri afukuzwe Simba. Kwa hiyo inapokuja wa kujinyonga, siku itafika mtu atajichimbia shimo au kweli kwenda kujinyonga, but not me. Ngoja nikapate wanzuki langu..........

Now ur talking... welcome back on board and kindly fasten ur belt!
 
Yaani humu ndani nikianza kusoma huwa nacheka sana. Hivi walitukanana hadharani, mimi niko mbali na mji wa dsm.

Sophia anaonekana na mdomo mrefu, sijui kama mama kahama anamuweza kwa maneno. Anyway tuliahidiwa kwamba wanawake watapewa nafasi za juu sasa kigezo kilichotumika kuwapa ndiyo kinakosekana.

Watu wazima wameenda shule ikifikiakwenye uongozi au ulaji akili inawatoka wanabehave kama vichaa.

Mambo hayo!
 
Back
Top Bottom