Bakari Maligwa
Member
- Aug 18, 2010
- 65
- 22
...Hii sasa inaonesha ni kweli, "Sitta alichakachuliwa kwenye nafasi ya Uspika". Ni dhahiri kwa vile inaonesha jinsi gani "Genge la Mafisadi" waliyomo kwenye "Mfumo-tata wa Ufisadi wa CCM" unavyoweza kutumia mbinu za kimkakati na au kisera katika kufanikisha ufisadi na ujambazi wa kiserikali. Kuna mambo matatu (3) muhimu ambayo Mh. Sitta anawajibu wa kuyatolea maelezo, nayo ni:
- Inaonesha yeye (Mh. Sitta) anawajua wamiliki wa Richmond (cum Dowans) na ndiyo maana anasema kwamba wanajiandaa kwa Urais 2015;
- Nini kilifichwa na Mh. Mwakyembe wakati hoja ya Richmond ilipokuwa inajadiliwa Bungeni; na
- Kwa nini Serikali (na Wabunge wa CCM) waliifunga hoja ya Richmond ilhali hatma yake ilikuwa inatokota na sasa tunaona matokeo yake?