Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Katika kukithiri kwa rushwa ndani ya shirika la Umeme Tanesco, meneja wa Tanesco Tabata bwana Richard Swai na wafanyakazi wote wapatao 28 wamesimamishwa jana na leo mda huu ndio maamuzi yanasubiriwa,
Inatajwa kuwa meneja huyo na watendakazi wake walifika nyumbani kwa mama yake na Emanuel Nchimbi Tabata na kumuwekea umeme kinyume na taratibu za Kitaneso bila waziri huyo kujua kuwa umeme aliofungiwa ni wamagumashi, baada ya mda kupitia kikosi maalumu cha Tanesco (RPU) kilifika nyumbani kwa mama huyo na kuukata umeme ambapo waliuomba wapewe pesa ili waurudishe na waziri Nchimbi alikataa na kutaka kulifuatilia suala hili yeye mwenyewe makao makuu ya Tanesco,
Kwakuwa Waziri huyo haishi hapo, bali hushi Masaki, wiki iliyopita alikwenda kumjulia hali mama yake na ndipo aliposhangaa kuona umeme unawaka, akawahoji ndugu zake wakasema walijichanga pesa na kuwapa tanesco wakarudishiwa umeme,
Hapo waziri ndipo alipocharuka na kumuona mojakwamoja Mkurugenzi wa Tanesco ndugu Mhando, kufumba na kufumbua jana Mhando amekisimamisha kazi kituo kizima na leo tangu asubuhi kikako cha dharula na wafanyakazi hao chini ya Katibu mkuu wa Wizara ya Nishati na madini, Mkurugenzi wa Tanesco na maafisa wote watanesco kimekuwa kikiendelea na ndipo sasa wamepewa mda mpaka saa kumi jioni wawe wametoa maelezo kwanini wasiwajibishwe (wafukuzwe) kwa kosa hilo!
Hapa wizarani ni hofu tupu imetanda wakisubiri hatima hiyo ya saa kumi leo!
UDATES:
Mpaka naondoka eneo la tukio saa 12:30 watuhumiwa wote walikuwa hawajatoa maelezo waliyotakiwa kuyatoa, na walikuwa na kikao na ofisa mwajiri wa tanesco mkoa Ilala,
Hatima yao tutaijua asubuhi ya kesho!
UDATES:
Taarifa zinajuza kuwa wafanyakazi na uongozi wao wote wamerudishwa kazini, inatajwa kuwa hayo yametokea baada ya kutokuwa na ushahidi wa wazi kuwa walipokea rushwa na walimfungia umeme feki,
Taarifa zinazidi kusema wataalamu wa Manuvazi ndani ya tanesco walifanikiwa jana kuhuisha nyaraka zote feki za kuingizia umeme za mama Nchimbi na kuwa halali kabisa,
Ndipo mwisho wa siku imeonekana ni majungu tu hakuna cha rushwa wala umeme wa magumashi!
Hehee hiyo ndio Dar na wadarslam wenyewe!
Inatajwa kuwa meneja huyo na watendakazi wake walifika nyumbani kwa mama yake na Emanuel Nchimbi Tabata na kumuwekea umeme kinyume na taratibu za Kitaneso bila waziri huyo kujua kuwa umeme aliofungiwa ni wamagumashi, baada ya mda kupitia kikosi maalumu cha Tanesco (RPU) kilifika nyumbani kwa mama huyo na kuukata umeme ambapo waliuomba wapewe pesa ili waurudishe na waziri Nchimbi alikataa na kutaka kulifuatilia suala hili yeye mwenyewe makao makuu ya Tanesco,
Kwakuwa Waziri huyo haishi hapo, bali hushi Masaki, wiki iliyopita alikwenda kumjulia hali mama yake na ndipo aliposhangaa kuona umeme unawaka, akawahoji ndugu zake wakasema walijichanga pesa na kuwapa tanesco wakarudishiwa umeme,
Hapo waziri ndipo alipocharuka na kumuona mojakwamoja Mkurugenzi wa Tanesco ndugu Mhando, kufumba na kufumbua jana Mhando amekisimamisha kazi kituo kizima na leo tangu asubuhi kikako cha dharula na wafanyakazi hao chini ya Katibu mkuu wa Wizara ya Nishati na madini, Mkurugenzi wa Tanesco na maafisa wote watanesco kimekuwa kikiendelea na ndipo sasa wamepewa mda mpaka saa kumi jioni wawe wametoa maelezo kwanini wasiwajibishwe (wafukuzwe) kwa kosa hilo!
Hapa wizarani ni hofu tupu imetanda wakisubiri hatima hiyo ya saa kumi leo!
UDATES:
Mpaka naondoka eneo la tukio saa 12:30 watuhumiwa wote walikuwa hawajatoa maelezo waliyotakiwa kuyatoa, na walikuwa na kikao na ofisa mwajiri wa tanesco mkoa Ilala,
Hatima yao tutaijua asubuhi ya kesho!
UDATES:
Taarifa zinajuza kuwa wafanyakazi na uongozi wao wote wamerudishwa kazini, inatajwa kuwa hayo yametokea baada ya kutokuwa na ushahidi wa wazi kuwa walipokea rushwa na walimfungia umeme feki,
Taarifa zinazidi kusema wataalamu wa Manuvazi ndani ya tanesco walifanikiwa jana kuhuisha nyaraka zote feki za kuingizia umeme za mama Nchimbi na kuwa halali kabisa,
Ndipo mwisho wa siku imeonekana ni majungu tu hakuna cha rushwa wala umeme wa magumashi!
Hehee hiyo ndio Dar na wadarslam wenyewe!