Waziri Nchimbi akimbia na sanduku la kura wakati madiwani wakigombana

Saf saanaaa hii ndio democrasia. tumechoka kuchakachuliwa kila siku.. Hongereni madiwani wote
 
Naibu Meya kufichakura kwenye chupi!!! hii kali. Hivi madiwani wangeamua kumsachi sijui ingekuwaje, inamana hata Bakwata na Shura ya Maimamu nao wangeandamana kupinga kudhalilishwa kwa Naibu Meya wa CCM??.
 
Nilikuwa ukumbini na kushuhudia sakata hili,baada ya kupigwa kura,kura za Hapana zilipatikana 14 na kura za Ndio zilikuwa 12,baada ya Nchimbi kuona meya aliyekuwa akimtaka yeye apita amekataliwa akaamua kutumia umafya wa kuforce matokeo na kwa kushirikiana na naibu meya wakatangaza matokeo kinyume,ndipo moto ulipoanza kuwaka,wakaitwa madiwan wawil pale mbele wahesabu kura zile na baada ya kuhesabu tena kura zile,matokeo yalionesha Hapana ni 14 na NDIO ni 12,hapo ndipo naibu Meya Marium Dizumba alipoiba kura na kuzificha kwenye Chupi na sio kwenye pochi waandish wanapotosha,hali ilikuwa tete na kusababisha Diwan wa kata ya misufin(chadema)salumu mfamaji kugongwa na gar na kada wa chama cha mapinduz,bwana Nchimbi wazir aliamua kukimbia na sanduku la kura baada ya kuona wameshikwa pabaya.wanachokifanya ccm ni kulazimisha kumpitisha meya jambaz ambaye sio wananch tu hata madiwan wenzake wa ccm hawamtaki.Wanaharakat wote tuungane kote tz kusimamia hak na kupinga wale wote naotaka kutupeleka watanzania kubaya kwa maslah yao binafsi.
Jamani hebu Wanasheria humu JF tusaidieni kwa hili" Naibu Meya kuficha kura kwenye chupi" je ni kosa gani katika sheria za nchi ambalo mtuhumiwa anaweza kushitakiwa nalo. Maana mimi kwa mawazo yangu tendo hilo ni sawa na kukanyaga katiba ya nchi kwa makusudi. Huyu tayari keshajidhalilisha mwenyewe.
 
Naibu meya wa songea mjini Marium Dizumba jana alisababisha uchaguzi wa umeya wa manispaa ya songea kuvurugika baada ya kuiba kura na kuzificha kwenye chupi,ili kumuwezesha ndugu Charles Mhagama kushinda nafas hiyo.

Wananchi na madiwan wengi wakiwemo na wa ccm hawamtaki bwana Mhagama awe meya wa manispaa yetu ya songea kwa kuwa hana sifa za uhadilifu hata kidogo na alipitishwa ili akasimamie maslahi ya wachache akiwemo mbunge Emanuel Nchimbi, kilichofanyika ni madiwani wa chadema kuungana na baadhi ya madiwan wa ccm na kupiga kura ya hapana,zoez hil liliwezekana na kura za hapana zilipatikana 14 na za Ndio 12. Hapa ndipo walipotaka kufanya njama za kubadil matokeo ili yawe kinyume, hali iliyosababisha naibu meya Marium Dizumba bila aibu kuiba kura na kuzificha kwenye chupi, huku wazir Nchimbi akikimbia na sanduku la kura nje ya ukumbi.

Wakati hali hii ikiendelea madiwan wa ccm na chadema wakazipiga kavu kavu ndan ya ukumbi huo wa manspaa huku kada mmoja wa chama cha mapinduzi Hamisi abdalar Ally akimgonga na gari nje ya ukumbi, diwani wa kata ya misufin chadema bwana Salumu Mfamaji na kumsababishia maumivu makali.

historia inaonesha ukombozi hupatika kwa damu kumwagika, siyo kichawichawi
 
Naona sasa hivi kipengele cha wizi kimeongezwa kwny katiba ya ccm, maana naona kila mwana chama anajitahidi kutokuivunja katiba kwa kuiba chochote alich na acces nacho! kwenye wizi wa kura huko wana phd kabisa kugushi, kutapeli, kuiba vitu vya kawaida mf. mataulo wamo pia.nk...... Napendekeza neno wizi libadilishwe na neno ccm kwny kamusi, mf. yule mwizi = yule ccm, tumemkamata akijalibu kuiba= tumemkamata akijaribu ku ccm, wizi = u- ccm, nk
 
Katika matizo yote tuliokuwa nayo ni cha mtoto kulinganisha na tatizo la CCM ni adui wa taifa.
 
Mwandishi wa thread ameishafanya judgement sasa tunadiscuss nini?.anasema madiwani wa ccm na cdm wazichapa,huku anasema madiwani wa ccm na cdm wameungana kumkataa mgombea umeya wa ccm.tayari taarifa yake inaonesha ushabiki wa kijinga.
 
Hii thread imejaa umajitaka sana kwahiyo siwezi kupoteza muda wangu kuichangia hata neno moja. Upuuzi mtupu tena haina mashiko kabisa.
 
Hii thread imejaa umajitaka sana kwahiyo siwezi kupoteza muda wangu kuichangia hata neno moja. Upuuzi mtupu tena haina mashiko kabisa.

Mwita26 kweli akili zako hazina akili .Tayari kwa kuandika haya mchango wako ndiyo huo kwani nani alitegemea useme zaidi haya ambayo ni michango ya kila siku ?Sijui ukisha kuwa CCM na umri mdogoo unakuwa na laana ?
 
Naibu Meya hana mamlaka kisheria ya kutangaza matokeo ya uchaguzi. Mamlaka hiyo iko chini ya msimamizi wa uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri!
 
CCM kwa wizi ni nomaaaaa!sijui mafunzo ya wizi walipatia wapi!wanaiba fedha-kagoda,kura,madini,vyeti feki wanyama pori na wake za watu
 
Back
Top Bottom