Waziri Mwijage: Kufungwa kwa kiwanda cha Dangote hakutaathiri upatikanaji wa sementi nchini

Mbona hii serikali inekuwa na ndimi nyingi?

Jana 30/11/2016 taarifa ya habari ya ITV saa 2.00 usiku, huyu Mwijage nilimuona ITV, tena kwa kutuaminisha Watanzania alishika barua ambayo alidai kwamba imetoka kwa CEO wa Dangote. Eti barua hiyo ikieleza kwamba kiwanda cha Dangote, hakijasimamisha uzalisha wa cement. Ila kwasasa wanafanya matengenezo ya mitambo yao na kwamba hili ni jambo la kawaida kwa viwanda vinayoanza uzalishaji.

Sasa iweje leo 1/12/2016 hata kabla ya masaa 24 kupita, huyu huyu Mwijage anakuja tena na SOUND nyingine kwamba kiwanda cha Dangote kimesimamisha uzalishaji?

Ni waji.nga tu ndiyo wataamini kwamba Dangote akisimamisha uzalishaji, haitaathiri soko ya cement. Wakati huko Mtwara Dangote alipokuwa anazalisha cement, mfuko mmoja wa cement ulishafikia Tsh 11,500/-. Kusimamisha uzalishaji tu kwa week 1 tayari mfuko wa cement huko Mtwara umeshafikia Tsh 15,000/-.

Huyu huyu Mwijage ndiye anayesema kwamba ukiwa na cherehani 1 tayari ni kiwanda, ukiwa na mashine 1 ya kufyatua matofali tayari ni kiwanda. Kweli Tanzania tumempata Waziri wa Viwanda!
Inasikitisha sana watanzania kutudanganya kila Siku na hawa watawala wetu.Yaani Leo waziri anaongea Kwa hasira kabisa,eti anatetea viwanda vingine.Anaturudisha kule pa cement kuuzwa sh 20,000 tabora mwanza
 
Nakataa,kubwa hapa ni kutungwa kwa sheria za kudhibiti na kuongoza viwanda,hao hao unao waita wafanya biashara wazoefu,watatumiwa na wafanya biashara walafi au wao wenyewe kugeuka kunguni.
Sijasema wao ndo wa make izo deals....
nimesema watumike kama consultants during negotiations! serikali ndo itakua na final say but watakua wameona sides nyingi za deal husika.
Vitu viwili tofauti...
kama mfanyabiashara, at some point of your business lazima uwahitaji hawa watu!! Serikali inatumia same same people ambao wanabadilishiwa wizara na vyeo tuu!! na wengi wao si wafanyabiashara, wanategemea mishahara na commissions na dili...
 
Nani Alikwambia Makaa Yetu Ya Nawe Hayana Ubora? hivi Na Wewe Unaamini maneno ya Mitaani ya Uzushi?

Hii Nchi vipi? Mbona kizazi hiki hakifikirii sawa sawa?

Hayo Makaa ya Mawe Yana Ubora Sawa na Yale Ya South na Kwingineko Duniani...

Kumbuka hapa tunapigana vita na Mabepari wa South Afrika ambao wana leseni ya kuchimba Makaa ya Mawe South Afrika, Hawa ndio wanaotusumbua kwa kushinikiza Dangote aendelee Kuagiza Makaa kwao huko, ambapo ikiwa Dangote atawaacha hao Mabepari wa South Afrika, mapato yao hao Mabepari yataporomoka, hivyo wanashawishi ili kamgomo baridi kaendelee ili serikali ilegeze kamba.

Kama Huamini, Ingia kwenye mtandao tafuta makampuni yanayochimba Makaa ya Mawe South Afrika, Utashangaa.
Labda nkupe ufafanuzi kidogo wa kitaalam uelewe nachokisema nakijua ,coal ya SA na TZ na ya mozambique na nyngine nyingi duniani zinapatikana kwenye karoo formations strata sequence ya K2 au K4 mostly K2,hivyo unavyosema ni sawa upo sahihi lakini kiubora zinatofautiana in terms of level of maturity(rank),coal zipo aina tofauti kulingana na carbon,ash,sulfur contents etc bila kusahau heat content,
Ya kwetu hasa ya ngaka mine ipo less matured iko kwenye bituminous coal ,wakati ya SA nahisi ni anthracite rank ya juu ya coal....sasa kampuni kama ya dangote inakuja na specifications ya coal inayohitaji in terms of ash content,heat content na sulfur content na pia price sasa kama wauzaji wetu hawajakidhi hizo specifications ,ndo unaona matatizo kama haya yanatokea ,
Asante
 
Habari wakuu,..


Huu ni muendelezo wa kauli tata za viongozi wetu juu sintofahamu kubwa iliyopo kati ya Serikali na kiwanda cha mfanyabiashara mkubwa Dangote.


Kauli hiyo ameisema Waziri mwenye dhamana ya viwanda, Bw Charles Mwijage.

Nimeshangaa kuona kiongozi kama huyu kukosa hata simple theory ya mambo ya uchumi, yaani suala la Demand/Supply/Price.



Ameshindwa kujua kiwanda cha Dangote kinachozalisha sementi kilifanya Suppy ya sementi uraiani kuwa kubwa, hali iliyopelekea Price au bei ya sementi hata kwa viwanda vingine kushuka kutokana na ushindani hivyo kupelekea watu wengi kumudu kununua sementi.


Badala yake ametujia na "NGONJERA" Ati kwamba sementi inapatikana tusijali, ameshindwa kutafakari kwamba baada ya Dangote kuondoka sokoni bei ya sementi iliyokuwa imeshuka itapanda na hata wananchi waliokuwa na matumaini ya kujenga watakwama.


Wananchi ndiyo tunaumia, tunaomba serikali imalize mvutano na huyu mfanyabiashara..



Chanzo : TBC Taifa.
Arusha tuna kiwanda chetu cha cementi na bado kipya!!! Ya Dangote ????
 
Mwijage ajaribu kuweka mawasiliano kati ya mdomo wake na ubongo
Matamshi anayotoa SI ya mtu mwenye kufikiri japo kidogo
 
Tusijadili mada hii kwa ushabiki. Tuanhalie faida na hasara kwa Dangote kununua coal nje ya nchi na kutaka apunguziwe bei ya nishati. Lakini pia tuangalie hasara kwa taifa ikiwa atasitisha uzalishaji. Mijadala yetu iwe constructive badala ya destructive. We all live in the sama house that is Tanzania
 
Hivi hakuna jambo lingine Muhimu Zaidi ya hili la Dangote? Tumechoka kujadili hili swala la Dangote, anunue Makaa yetu ya hapa ndani hataki aache, ulishaona mtu unajipangia bei unayotaka kuuziwa bidhaa? yaan anajipangia bei ya gas yetu eti auziwe kwa $ 4 :75? bei hii ni ya kuchimbia gas visimani sasa yeye anataka auziwe.

Ninachokiona hapa ni kwamba, Kuna Mawaziri wa serikali iliyopita na baadhi wa ya sasa ambao wana hisa huko ndio wanaotaka kumtikisa JPM, bwanae, hataki afunge kiwanda, hatuwezi kumbembeleza mtu kwa raslimali zetu, hataki afunge, kabla yake kwani tulikuwa hatujengi nyumba?

Kwanza, Nyati wanajenga kiwanda kingine Bagamoyo cha tani Milioni 3 kwa mwaka, hataki kutusikiliza na sisi aondoke...
THIBITISHA
 
Huna adabu wewe,

Unataka serikali impe Dangote Makaa ya mawe bure? au Gas bure? Serikali ikikubali kumpunguzia bei ya makaa ya mawe au gas wengine nao watalalamika.

Sasa, kipi nafuu, Ununue Makaa hapa nchini au uagize Afrika kusini wakati sisi tunayo?

Acheni ushamba,,,, Huyo Dangote amekuwa Mungu sasa?
Unamfaham mmliki wa makaa ya mawe yaliyopo Tanzania??
Au bado unafikiri kwamba yakiuzwa kuna chochote kinaingia serikalini , bora wamuache alete makaa yake ili tupate sementi kwa unafuu
 
so kikwete alimuingiza mkenge Dangote???sio vizuri nainatishia usalama wa uwekezaji hatuoni mbali kwanini kila serikali inayokuja toka ccm nikubadili sera tu kila anae kuja anajenga kibanda chake main road
 
A holder of MBA
Yaani jaman huyu kapitia form six kweli?
Maana pale angesoma hata ECA au EGM au HGE asingejaribu kuongea sentensi ya ajabu kiasi hiki.
Hivi inawezekanaje mtu mwenye dhamana hii anaongea kama lay-man jaman!!!
Inaitwa the power of 10%
 
Back
Top Bottom