CHAKA CHUWA
Member
- May 26, 2011
- 69
- 10
maaigizo tu haya!!!!!!
Waziri mpya wa Ofisi ya Rais(Asiye na Wizara Maalum),Prof.Mark Mwandosya amekaririwa akisema kuwa kama Mhe.Rais angezingatia hali yake ya kiafya na ushauri aliopewa na Madaktari juu ya kupata mapumziko,angemuacha apumzike.Akizungumza na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda,jana nyumbani kwake Kunduchi-Dar es Salaam,Prof Mwandosya alionyesha kutoridhishwa kwake na uteuzi wa Rais juu yake.
'Nahitaji mapumziko makubwa Mkuu' alisema Prof.Mwandosya akimueleza Pinda aliyeonekana kukubaliana naye. 'Niheri nirudi UDSM nikafundishe Wahandisi wangu' aliongeza Prof Mwandosya.Mimi tu kuwaletea habari...
Aaa wapi anatii masharti ya akina "MWANAFYALE" waliompa kuwa "usipokuwa na huyu (Mwandosya) hatukupi kura.mchango wa mtu mwenye busara na hekima au mchapakazi mara nyingi huwa unahitajika siku zote, nadhani kikwete kwa kuzingatia uzoefu wa Profesa mwandosya uchapakazi wake na hata hekima zake ameona bado anamuhitaji sana katika baraza lake la mawaziri. kumpa uwaziri usio na wizara ni kumpunguzia majukumu pia kwani hatokuwa bounded na kazi flani flani na nadhani kazi yake kubwa ni kuangalia mahala palipo na mapungufu katika wizara mbali mbali na kutoa mchango wake.
hebu tuangalie enzi zile MREMA akipewa unaibu waziri mkuu chao ambacho hakipo kwenye katiba yatu but kutokana na uchapakazi wake na umuhimu wake Mwinyi aliona mtu huyu anahitajika kupewa nafasi ambayo itamfanya aweze kuingia katika wizara zingine na kutoa mchango wake pia
pia sitaki kuamini kuwa Mwandosya hakupewa taarifa awali, maana nachokifahamu kabla ya kutangazwa lazima muhusika (hasa wale katika nafasi muhimu na nzito), aelezwe kisha atoe maoni na akubali. So nahisi ili nalo limekuzwa tuu.
Teuzi hizi wateuliwa huwa hawafahamishwi kabla isipokuwa WAZIRI MKUU tu. Wengine hawa hatuna ubavu wa kukataa ulaji. Mimi nilisubiri weeee, hola, sikuambulia kitu kama mamilioni ya voda yanavyonipiga chenga!Mleta thread inabidi aweke source. Otherwise ni majungu tu. Haiingii akilini kwamba Prof Mwandosya hakujua uteuzi wake. Lazima alifahamishwa kabla. Kama alikubali na wakati hawezi kufanya kazi, hiyo ndo tamaa ya fedha na madaraka sasa. Kwenye uwaziri kuna Chenji ya kumwaga ndo maana hakukataa.
KIRAKA kwa tafsiri nyepesi. Muhimu ni jeneza kufunikwa bendera kuubwa ya Taifa likitokea lisilotarajiwa.waziri asiye na winzara maalumu du hii nayo kali
Kwani kufundisha wahandisi ndio kupumzika?
Kwa heshima hiyo aloopewa na JMK, ni yeye mwenyewe aseme sasa rasmi kwamba apumzishwe sio tu uwaziri bali na ubunge pia. Hata U-NEC wa CCM angewaachia wengine. Hofu yake labda ni kutelekezwa akifanya hivo lakini ana tumiradi twa hapa na pale twa kumsukumia siku.Another gaffe by JK!! kumbe hakufanya consultation na prof kabla ya kumteua?! after all hali ya prof imefahamika siku nyingi kwama ni tete kidogo, hapakuwa na haja ya JK kufanya uteuzi wa huruma eti asionekana amemtupa ilihali akiwa mgonjwa, uteuzi wa aina hii hauna tija na asisahau mlipa kodi atakamuliwa kumlipa mtu asiyefanya kazi to the full.
Mwachie prof apumzike kama ni ushauri anaweza akatoa hata akiwa UDSM, na hiyo nafasi ya MInister without portfolio ni kuchoma pesa za wanyonge bila sababu, futilia mbali.
ndo amejua leo kuwa anatakiwa kurudi kufundisha wahandisi....akaae humo humo kudadadeki hakuna kutoka
ndo amejua leo kuwa anatakiwa kurudi kufundisha wahandisi....akaae humo humo kudadadeki hakuna kutoka