Waziri Mkuu Pinda na Spika Anne Makinda wajiuzulu kwa Rushwa!

makoye2009

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,638
1,218
Baada ya sakata la TANESCO kutinga Bungeni kufuatia Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini Prof.Muhongo sasa imebainika wazi kuwa kulikuwa na Wabunge kadhaa wa CCM na wachache toka upinzani ndani na nje ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini walikuwa wakipokea Rushwa kutoka kwa Mafisadi ili kundelea kuwanyonya Watanzania kupitia TANESCO!

Kutokana kashfa hii nzito ya Rushwa sasa ni wakti mwafaka kwa Viongozi wakuu wa Bunge letu kujiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya Bunge la Tanzania. Viongozi hawa wakuu wanaohusika na Bunge ni Spika Anna Semamba Makinda na Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda ambaye ni Kiongozi Mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni.

Hili siyo tukio la kwanza kwa Bunge la Tanzania kukumbwa na kashfa tuhuma za rushwa. Kuna matukio ya Rushwa ambayo yametokea mfululizo kwa kufuatana ndani ya bunge lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na viongozi hawa. Yafuatayo ni matukio hayo:

1. Mbunge David Kafulila kupitia NCCR-Mageuzi aliwahi kuibua kashfa ya Rushwa kwenye Kamati ya Fedha Serikali za Mitaa (LAAC)inayoongozwa na Mhe.Mrema kuwa wajumbe wa Kamati hiyo walikuwa wakijihusisha na Rushwa kwa kuidai ili wawaandikie ripoti safi viongozi wa Halmashauri za Wilaya. Taarifa hii ilipelekwa kwa Spika makinda lakini mpaka leo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

2. Mbunge wa Jimbo la Bahi (CCM), Omary Badwel kwa tiketi ya CCM alikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) kwa tuhuma ya kupokea rushwa ya Sh1 milioni kutoka kwa kiongozi wa Serikali toka mojawapo ya Halmashauri za nchi hii.

3. Mbunge Andrew Chenge kupitia CCM alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge Fedha na Uchumi ilhali inajulikana kuwa Chenge ni kinara wa Rushwa ya Rada ya waingereza toka BAE system. Kwa Spika makini na Waziri Mkuu makini Chenge hakupashwa kupewa Umwenyekiti wa Kamati ya Bunge tena ya Fedha na Uchumi kwa uchafu alionao. Lakini kwa vile tuna Spika dhaifu,Waziri Mkuu dhaifu na Serikali goigoi ndiyo maana haya yaliruhusiwa.

4. Wakati wa Uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALC)kulikuwa na Rushwa kubwa sana iliyofanyika pale Dodoma. Wagombea wa nafasi hizo hasa kutoka CCM walitembeza rushwa fedha na hata ngono kwa Wabunge ili waweze kupigiwa kura ya kuingia kwenye EALC. Matokeo tuliyaona na ndivyo ilivyokuwa. Habari hizo zilikuwa zinajulikana kwa kila mtu lakini Spika mwanamke dhaifu na PM mwanamme dhaifu walikaa kimya na wakaruhusu uchafu huo ufanyike.

Kwa matukio haya yasiyo na shaka yoyote ya kuwa ni Rushwa tunaomba kwa heshima na taaadhima Spika Anne Makinda na Waziri Mkuu Mizengo Pinda sasa wajiuzulu ili kulinda Heshima na Hadhi ya Bunge letu ili lisiendelee kuchafuliwa na kashfa za rushwa.

Nawasilisha
 
Na mbowe na wabunge wa CDM watajiuzulu kama itathibitika kuwa Zitto alipokea mlungura?
 
Na mbowe na wabunge wa CDM watajiuzulu kama itathibitika kuwa Zitto alipokea mlungura?

kwani Pinda na Makinda wanatakiwa kujiuzuru kwa sababu ni viongozi wa ccm? Tunazungumza bunge, we unaleta ulevi hapa. Kwanza omba msamaha kuwaweka Pinda na Makinda level moja na Dr. Slaa na Mbowe.
 
kwani Pinda na Makinda wanatakiwa kujiuzuru kwa sababu ni viongozi wa ccm? Tunazungumza bunge, we unaleta ulevi hapa. Kwanza omba msamaha kuwaweka Pinda na Makinda level moja na Dr. Slaa na Mbowe.

Acha uvivu, Mbowe ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, mawaziri vivuli wawili wanatuhumiwa kwa rushwa. Ni collective responsibility.
 
WM na Madame Speaker wao siyo suala la uwajibikaji wa pamoja.
Kila mmoja wao hajawa mkweli katika mambo yaliyokwisha wasilishwa Bungeni tena kwa ushahidi mzuri kabisa.
Wana wajibu binafsi wa kuondoka japo utamaduni wa kukubali kuwajibika hatuna.
 
Wawajibike kwanza watuhumiwa.....haiwezekani kuwajibisha viongozi Kabla ya Wezi husika hawajakamatwa......hawa Wezi kwa umoja wao (wabunge ofcoz) Yaaani Wezi kutoka CCM na Wezi kutoka CHADEMA kwanza watangazwe hadharani, Kama ni kunyong'wa wanyongwe Kama ni kupigwa mawe hadi wafe tuwapigwe mawe hadi kufa......Maana tushachoshwa na Wezi WA aina hii.
Yani hadi wabunge WA UPiNZANi (Chadema?)? Mimi nilidhani ni Magamba pekee ndio mafisadi!!
Likishakamilika zoezi la kuwaadabisha hao Wezi then ndio turudi kwa hawa viongozi wakuu na kuona Ushiriki wao katika kashfa husika. Ndio tutajua Kama NAo wawajibike au la. Usilete Harakati zako hapa.

Karibu ADC.

ADC - DIRA ya Mabadiliko.
 
Nyambafu na hii heading yako,unaandika as if wameshajiuzulu,moods au mleta mada change nane wajiuzulu,weka kujiuzulu,tena iwe ni tetesi na si breaking news.
 
Baada ya sakata la TANESCO kutinga Bungeni kufuatia Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini Prof.Muhongo sasa imebainika wazi kuwa kulikuwa na Wabunge kadhaa wa CCM na wachache toka upinzani ndani na nje ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini walikuwa wakipokea Rushwa kutoka kwa Mafisadi ili kundelea kuwanyonya Watanzania kupitia TANESCO!

Kutokana kashfa hii nzito ya Rushwa sasa ni wakti mwafaka kwa Viongozi wakuu wa Bunge letu kujiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya Bunge la Tanzania. Viongozi hawa wakuu wanaohusika na Bunge ni Spika Anna Semamba Makinda na Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda ambaye ni Kiongozi Mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni.

Hili siyo tukio la kwanza kwa Bunge la Tanzania kukumbwa na kashfa tuhuma za rushwa. Kuna matukio ya Rushwa ambayo yametokea mfululizo kwa kufuatana ndani ya bunge lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na viongozi hawa. Yafuatayo ni matukio hayo:

1. Mbunge David Kafulila kupitia NCCR-Mageuzi aliwahi kuibua kashfa ya Rushwa kwenye Kamati ya Fedha Serikali za Mitaa (LAAC)inayoongozwa na Mhe.Mrema kuwa wajumbe wa Kamati hiyo walikuwa wakijihusisha na Rushwa kwa kuidai ili wawaandikie ripoti safi viongozi wa Halmashauri za Wilaya. Taarifa hii ilipelekwa kwa Spika makinda lakini mpaka leo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

2. Mbunge wa Jimbo la Bahi (CCM), Omary Badwel kwa tiketi ya CCM alikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) kwa tuhuma ya kupokea rushwa ya Sh1 milioni kutoka kwa kiongozi wa Serikali toka mojawapo ya Halmashauri za nchi hii.

3. Mbunge Andrew Chenge kupitia CCM alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge Fedha na Uchumi ilhali inajulikana kuwa Chenge ni kinara wa Rushwa ya Rada ya waingereza toka BAE system. Kwa Spika makini na Waziri Mkuu makini Chenge hakupashwa kupewa Umwenyekiti wa Kamati ya Bunge tena ya Fedha na Uchumi kwa uchafu alionao. Lakini kwa vile tuna Spika dhaifu,Waziri Mkuu dhaifu na Serikali goigoi ndiyo maana haya yaliruhusiwa.

4. Wakati wa Uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALC)kulikuwa na Rushwa kubwa sana iliyofanyika pale Dodoma. Wagombea wa nafasi hizo hasa kutoka CCM walitembeza rushwa fedha na hata ngono kwa Wabunge ili waweze kupigiwa kura ya kuingia kwenye EALC. Matokeo tuliyaona na ndivyo ilivyokuwa. Habari hizo zilikuwa zinajulikana kwa kila mtu lakini Spika mwanamke dhaifu na PM mwanamme dhaifu walikaa kimya na wakaruhusu uchafu huo ufanyike.

Kwa matukio haya yasiyo na shaka yoyote ya kuwa ni Rushwa tunaomba kwa heshima na taaadhima Spika Anne Makinda na Waziri Mkuu Mizengo Pinda sasa wajiuzulu ili kulinda Heshima na Hadhi ya Bunge letu ili lisiendelee kuchafuliwa na kashfa za rushwa.

Nawasilisha

With this level of thinking and analysis kweli kazi ipo!
Viongozi wakuu wa Bunge mbona unamuacha KUB na mawaziri vivuli? Do you think wako pale kwa ushahidi tu.
If kuna watu wa kujiuzulu sio PM na Spika tu, ingependeza zaidi hata Bunge lote likivunjwa ili tuanze upya.

Go back to analytical thinking na jifunze logic kabla hujaandika madudu kwenye JF as it is quite a respected forum in Tanzania.
Another thing, badilisha heading ya thread yako!
 
Na mbowe na wabunge wa CDM watajiuzulu kama itathibitika kuwa Zitto alipokea mlungura?
Usiongee pumba na kuleta ushabiki mleta mada aliowazungumzia ni voingozi wa Bunge Mbowe kama M/kiti anahusika vipi na hao wabunge wa CDM? ukizungumza hivyo unamaanisha JK ajiuzuru na pia Bunge livunjwe.Tumia akili yako vizuri ndugu usikubali itumiwe na wengine.
 
Mbona hawa wa CCM wametajwa mbona umwambii Pinda na wenzie wajiuzulu?

Ina maana hata heading ya thread huwezi kusoma? hivi watanzania tuna tatizo gani jamani?????!!!!


grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Ina maana hata heading ya thread huwezi kusoma? hivi watanzania tuna tatizo gani jamani?????!!!!


grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr

Wewe umesoma hapo nilipomjibu huyu aliyeandika ? Au uvivu wako ndio unakufanya kuropoka?
 
Usiongee pumba na kuleta ushabiki mleta mada aliowazungumzia ni voingozi wa Bunge Mbowe kama M/kiti anahusika vipi na hao wabunge wa CDM? ukizungumza hivyo unamaanisha JK ajiuzuru na pia Bunge livunjwe.Tumia akili yako vizuri ndugu usikubali itumiwe na wengine.

We Kiboga, wapi umeona mwenyekiti? Kwani baraza kivuli linaongozwa na nani?
 
makoye2009 What a wonderful analysis...this is the kind of government that wants to liberate Tanzania anguish poverty....
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom