Waziri Mkuu Pinda na Punguzo la kodi

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Katika vyombo vya habari nimesikia tamko la Waziri Mkuu Pinda kutoa kauli ya kutaka kodi ipunguzwe kwenye mishahara. Kwangu nimeona Waziri Mkuu amewakumbuka wafanyakazi. Kwa sasa kodi ni kubwa sana kiasi inafikia robo ya mshahara wa mfanyakazi wa serikali. Kwa kauli hiyo naomba ifanyiwe kazi mara moja ili kutunusuru sisi waajiriwa.
 
Katika vyombo vya habari nimesikia tamko la Waziri Mkuu Pinda kutoa kauli ya kutaka kodi ipunguzwe kwenye mishahara. Kwangu nimeona Waziri Mkuu amewakumbuka wafanyakazi. Kwa sasa kodi ni kubwa sana kiasi inafikia robo ya mshahara wa mfanyakazi wa serikali. Kwa kauli hiyo naomba ifanyiwe kazi mara moja ili kutunusuru sisi waajiriwa.

Waziri Mkuu anaonekana yuko reasonable sana. God bless you mheshimiwa kwa kukukumbuka walalahoi. Sijui Raisi yuko wapi?
 
Waziri Mkuu anaonekana yuko reasonable sana. God bless you mheshimiwa kwa kukukumbuka walalahoi. Sijui Raisi yuko wapi?

Swali ni kwamba hiyo kodi atabambikwa/itahamishiwa kwa nani! Kwa vyovyote huyo atakayebebeshwa hatamuona kwamba yuko reasonable, isn't it?
 
Kama litafanyiwa kazi basi itakuwa ni jambo jema kwa wafanyakazi. Kwa muda mrefu wameendelea kulipa kodi kubwa kuliko mtu yeyote. Wafanya biashara wengi wanakusanya kodi ya vati kwa niaba ya selikari kutoka kwa wananchi lakini hawaiikishi yote kama inavyotakiwa hivyo kodi huigeiza kuwa ni faida yao pia. Huo ni wizi mkubwa unaofanywa na kundi la baadhi ya wafanya biashara. Huko ndiko nguvu zielekezwe ili huhakikisha kodi wanayoilipa wananchi kwa kununua bidhaa mbalimbali isiishie mikononi mwa wafanyabiashara tu bali ikusanywe ipasavyo kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi
 
Du kweli jamani kodi kubwa sanasana...tunaumiasana mmnikiona stk huwa nachukia sana hasa uck yakiwa na madereve uswahilini wanatanua au kuibamafuta nasikia hasira sana....ni kodi zetu zzinatumiwa vibaya...derreva anakaa tegeta boss masaki au oysterbay...gari anakaa nalo dereva.
 
Katika vyombo vya habari nimesikia tamko la Waziri Mkuu Pinda kutoa kauli ya kutaka kodi ipunguzwe kwenye mishahara. Kwangu nimeona Waziri Mkuu amewakumbuka wafanyakazi. Kwa sasa kodi ni kubwa sana kiasi inafikia robo ya mshahara wa mfanyakazi wa serikali. Kwa kauli hiyo naomba ifanyiwe kazi mara moja ili kutunusuru sisi waajiriwa.

Yuko sahihi lakini kodi Tanzania zina matatizo makubwa mno.Mfano kodi ikiwa kubwa sana na serikali ikakusanya mipesa mingi nyingi zinaishia kwenye ufisadi wa miradi kama Ya Dowans na kununua migari ya kifahari kama mabenzi na ma Toyota prado na maposho ya semina na warsha za waheshimiwa walioko serikalini na hivyo kupoteza maana nzima ya kukusanya kodi kubwa ili kuinua maendeleo.

Wafanyakazi nao wakipunguziwa kodi balaa lingine linakuja.Nchi zilizoendelea kodi ya wafanyakazi ikipungua ina maana Savings zao zinaongezeka katika benki wanazoweka pesa zao na savings hizo zinazoongezeka wafanyakazi wengi huzitumia kwa kuwekeza katika investments kama kununua shares kwenye makampuni na hivyo kuchochea kukua kwa uchumi.Tanzania wafanyakazi wengi wakipunguziwa kodi na pato lao likawa kubwa kile kiwango kinachoongezeka hupelekwa kwenye matumizi ya matanuzi ya kifahari badala ya kuingizwa katika uwekezaji au uzalishaji utakaoinua uzalishaji na uchumi;/

Nadhani ni wakati wa serikali kuwa na adabu.Kama inataka kuongeza kodi wajiulize hizo pesa wanataka ziongezeke ili iwe nini na wafanyakazi kama inapungua kodi waelimishwe sababu ya punguzo hilo na nini matarajio ya serikali kwa wafanyakazi.Vinginevyo kuongeza kodi au kupunguza kwaweza kuwa hakuna maana yoyote kama nchi inaendelea tu na kuwa maskini yuleyule.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom