Waziri Mkuu kukutana na madaktari kesho

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda kesho (Jumapili, Januari 29, 2012) atakutana na madaktari waliofanya mgomo kwenye ukumbi wa Karimjee kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Madaktari hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wanaomba kuonana na Waziri Mkuu na mara zote Waziri Mkuu amekubali kuonana nao lakini hawakutokea. Pamoja na kukubali huko kwa Waziri Mkuu, tarehe 25 Januari 2012 katika Mkutano wake na Wahariri wa Vyombo vya Habari aliwaomba Madaktari kuwa alikuwa tayari kuonana nao lakini hawakutokea.

Ili kuendeleza jitihada za kutaka kuonana na madaktari hao, Waziri Mkuu alituma Uongozi wa Serikali ukiongozwa na Mawaziri wa Afya na Ustawi wa Jamii; na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kuonana na Madaktari kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Starlight tarehe 27 Januari 2012. Kwenye Mkutano huo madaktari waliwasilisha malalamiko yao na kuomba kuonana na Waziri Mkuu. Kufuatia maombi hayo, Waziri Mkuu amewaandikia madaktari hao barua ya kuwataka kuonana nao Kesho, tarehe 29 Januari 2012 kwenye Ukumbi wa Karimjee, saa 4:00 asubuhi.

Kabla ya kufikia uamuzi huo, kulikuwa na mawasiliano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Uongozi wa Medical Association of Tanzania (MAT) na baadaye Mwenyekiti wa Muda wa Kamati ya Madaktari kuhusu mgomo wa Madaktari unaoendelea.

Aidha, Viongozi mbalimbali wa Serikali wamefanya mazungumzo na Wawakilishi wa Madaktari na Madaktari wenyewe kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Starlight ili kuweza kupata ufumbuzi wa matatizo yaliyowasilishwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu anawasihi Madaktari wote kuhudhuria mkutano.


IMETOLEWA NA:
OFISI YAWAZIRI MKUU
SLP 3021,
DAR ES SALAAM
JUMAMOSI, JANUARI 28, 2012
 
sasa siku zote hizo alikua anajivutavuta nini mpaka ndugu zetu na watanzania wenzetu wamepoteza maisha?
 
Kwa kauli aliyotoa kuhusu posho za wabunge tar 25, huyu naye ni sehemu ya tatizo la madaktari. Sioni ni vipi anaweza kuja na suluhisho.
 
Baada ya kutikisa kiberiti na kukuta kimejaa ameamua kuwafata....hahaha au alifikili akina Mgaya
 
dah! Ndugu zangu habari hizi vp tena? Makubaliano kwenye kikao leo ni kukutana j3, walikuwa wapi muda wote?
 
Madaktari wasikubali porojo zozote ambazo hazitalenga kutatua matatizo yao na ya jamii in general! Azungumze vitu black an white bila kumung'unya maneno. Wala asithubutu kulia pale ukumbini
 
Mimi linaloniuma ni wagonjwa kulala chini,tusubiri kesho PM atatoa majibu gani
 
Madaktari wasikubali porojo zozote ambazo hazitalenga kutatua matatizo yao na ya jamii in general! Azungumze vitu black an white bila kumung'unya maneno. Wala asithubutu kulia pale ukumbini
inaonekana hutaki muafaka na unaomba waziri mkuu asifanikiwe mgomo uendelee,kuna watu na viatu duniani
 
Madaktari wasikubali porojo zozote ambazo hazitalenga kutatua matatizo yao na ya jamii in general! Azungumze vitu black an white bila kumung'unya maneno. Wala asithubutu kulia pale ukumbini

Wasipokubali unafikiri ni nini kitafuata? amini usiamini, PM atawaambia serikali itayafanyia kazi madai yao, sioni jibu la tofauti. Madai mengi ni ya kisera zaidi na yanahusu na watumishi wengine pia. Huwezi kuongeza mishahara kiholela bila kuamsha madai kwingine. Mimi ningewashauri wakubaliane naye kuwa baada ya miezi 4-6 wanatarajia kuona utofauti katika yale wanayodai. Migomo ni migumu kuisustain kwa sababu ya tofauti nyingi zilizopo kati ya wagomaji, kuna wengine kati ya madaktari wameshachoka sasa wanatamani tu kurudi kazini, kuna wengine bado ari iko juu. Subiri uone baada ya kesho watakavyogawanyika.

Wakimkatalia PM tu wataambiwa wanaokubaliana na serikali warudi kazini wasiokubali waendelee kugoma. Waziri mkuu ndio serikali yenyewe na wanatakiwa walitambue hilo. Wakipewa option hizo mbili mgomo ndio umekwisha hivyo. Wawe wastaarabu na kukubaliana deal fulani na PM then waendelee kufuatilia kwa ukaribu, kama Ulimboka unasoma hii msg nafikiri utanielewa what to do. PM hawezi kumfukuza waziri au secretary wa wizara kienyeji enyeji, lazima wamlinde na kumuondoa ili kuondoa taswira ya kushinikizwa. Ni hilo tu.
 
Ataishia kumwanga chozi tu!
Maana kuongeza mafao kwa ss ni ngumu, mishahara ya January imelipwa nusunusu!
 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda kesho (Jumapili, Januari 29, 2012) atakutana na madaktari waliofanya mgomo kwenye ukumbi wa Karimjee kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Madaktari hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wanaomba kuonana na Waziri Mkuu na mara zote Waziri Mkuu amekubali kuonana nao lakini hawakutokea. Pamoja na kukubali huko kwa Waziri Mkuu, tarehe 25 Januari 2012 katika Mkutano wake na Wahariri wa Vyombo vya Habari aliwaomba Madaktari kuwa alikuwa tayari kuonana nao lakini hawakutokea.

Ili kuendeleza jitihada za kutaka kuonana na madaktari hao, Waziri Mkuu alituma Uongozi wa Serikali ukiongozwa na Mawaziri wa Afya na Ustawi wa Jamii; na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kuonana na Madaktari kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Starlight tarehe 27 Januari 2012. Kwenye Mkutano huo madaktari waliwasilisha malalamiko yao na kuomba kuonana na Waziri Mkuu. Kufuatia maombi hayo, Waziri Mkuu amewaandikia madaktari hao barua ya kuwataka kuonana nao Kesho, tarehe 29 Januari 2012 kwenye Ukumbi wa Karimjee, saa 4:00 asubuhi.

Kabla ya kufikia uamuzi huo, kulikuwa na mawasiliano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Uongozi wa Medical Association of Tanzania (MAT) na baadaye Mwenyekiti wa Muda wa Kamati ya Madaktari kuhusu mgomo wa Madaktari unaoendelea.

Aidha, Viongozi mbalimbali wa Serikali wamefanya mazungumzo na Wawakilishi wa Madaktari na Madaktari wenyewe kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Starlight ili kuweza kupata ufumbuzi wa matatizo yaliyowasilishwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu anawasihi Madaktari wote kuhudhuria mkutano.


IMETOLEWA NA:
OFISI YAWAZIRI MKUU
SLP 3021,
DAR ES SALAAM
JUMAMOSI, JANUARI 28, 2012


Duh!! SIASA ZISHAINGIA HUMU....
 
pinda ana nini huyo....?ni mmoja wa watu walioshidhwa kutekeleza wajibu wake.yupo yupo tu......
 
Wasipokubali unafikiri ni nini kitafuata? amini usiamini, PM atawaambia serikali itayafanyia kazi madai yao, sioni jibu la tofauti. Madai mengi ni ya kisera zaidi na yanahusu na watumishi wengine pia. Huwezi kuongeza mishahara kiholela bila kuamsha madai kwingine. Mimi ningewashauri wakubaliane naye kuwa baada ya miezi 4-6 wanatarajia kuona utofauti katika yale wanayodai. Migomo ni migumu kuisustain kwa sababu ya tofauti nyingi zilizopo kati ya wagomaji, kuna wengine kati ya madaktari wameshachoka sasa wanatamani tu kurudi kazini, kuna wengine bado ari iko juu. Subiri uone baada ya kesho watakavyogawanyika.

Wakimkatalia PM tu wataambiwa wanaokubaliana na serikali warudi kazini wasiokubali waendelee kugoma. Waziri mkuu ndio serikali yenyewe na wanatakiwa walitambue hilo. Wakipewa option hizo mbili mgomo ndio umekwisha hivyo. Wawe wastaarabu na kukubaliana deal fulani na PM then waendelee kufuatilia kwa ukaribu, kama Ulimboka unasoma hii msg nafikiri utanielewa what to do. PM hawezi kumfukuza waziri au secretary wa wizara kienyeji enyeji, lazima wamlinde na kumuondoa ili kuondoa taswira ya kushinikizwa. Ni hilo tu.

Pax, maelezo yako yana hisia ndiyo, lakini hayo unayoyasema ndiyo siasa halisi za Tanzania na Afrika ambazo matokeo yake ndiyo nchi ipo hapa ilipo. Haya madai ya madaktari ambayo mengi yanalenga kuboresha mazingira ya wagonjwa hayajaanza juzi, serikali inajua fika wajibu wake lakini inapuuzia kwa makusudi. Huwezi kuharibu halafu ukatatua tatizo kwa mabavu.
 
Pax, maelezo yako yana hisia ndiyo, lakini hayo unayoyasema ndiyo siasa halisi za Tanzania na Afrika ambazo matokeo yake ndiyo nchi ipo hapa ilipo. Haya madai ya madaktari ambayo mengi yanalenga kuboresha mazingira ya wagonjwa hayajaanza juzi, serikali inajua fika wajibu wake lakini inapuuzia kwa makusudi. Huwezi kuharibu halafu ukatatua tatizo kwa mabavu.

Massenberg sisi tuna viongozi wabovu kupita hata watu wanavyoelewa, kuboresha mazingira ya kazi ni vitu basic kabisa vinavyotakiwa vifanywe kila mwaka na serikali. Haingii akilini ati mtu akeshe usiku kucha umlipe buku 10, huu ni usanii uliopitiliza mipaka. Nategemea jambo hili PM kama atatumia hekima alitolee uamuzi wa papo kwa papo, angalau kiasi cha chini kabisa kisipungue nusu ya per diem = 40,000. Hayo mengine nafikiri wangekubaliana kuwe na team ya kuyafanyia kazi, baada ya miezi kama 4 hivi kuwe na mkutano wa madktari wapewe feedback, kama kuna usanii unaendelea wanagoma tena.
 
Back
Top Bottom