Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Leo katika mahojiano na TBC1, Waziri Masha amesema kuwa Mengi hakuleta uthibitisho wake kuhusu tuhuma alizozitoa za kutishiwa kufilisiwa na Waziri kijana. Lakini hawatamchukulia hatua na suala hilo wameachana nalo badala yake wanashughulikia SMS alizotumiwa. Hata hivyo amesahau kuwa katika maelezo yake ya awali alisema endapo hataleta uthibitisho ndani ya siku saba atamchukulia hatua. Sasa hapa kuna nini? Nadhani anatakiwa kutupa maelezo zaidi kwa nini amebadili msimamo. Vinginevyo ni hatari sana kwa waziri (serikali) kushindwa kutekeleza maagizo aliyoyatoa mwenyewe.